Jack Daniel
JF-Expert Member
- Sep 23, 2021
- 4,042
- 16,872
Habari JamiiForums
Siku zinakimbia, miaka inageuka, na umri unasogea.
Nakumbuka ni kama juzi tu Mh. Lowasa alivyotikisa Tanzania kwenye kampeni za Urais 2015.
Ni kama juzi tu tangu hayati Magufuli na itikadi zake, pamoja na misimamo mikali kwenye uongozi.
Miaka inakimbia, watu waliozaliwa mwaka 2000 ni watu wazima, si watoto tena; wengi wao wanafamilia kabisa.
Mtoto aliyezaliwa 2005, wakati Mh. Kikwete anachukua nchi kama kiongozi wa awamu ya nne, tayari ukimzingua anakuzingua, haogopi tena. Sasa ewe mtu mzima mwenzangu, fanya haya:
Siku zinakimbia, miaka inageuka, na umri unasogea.
Nakumbuka ni kama juzi tu Mh. Lowasa alivyotikisa Tanzania kwenye kampeni za Urais 2015.
Ni kama juzi tu tangu hayati Magufuli na itikadi zake, pamoja na misimamo mikali kwenye uongozi.
Miaka inakimbia, watu waliozaliwa mwaka 2000 ni watu wazima, si watoto tena; wengi wao wanafamilia kabisa.
Mtoto aliyezaliwa 2005, wakati Mh. Kikwete anachukua nchi kama kiongozi wa awamu ya nne, tayari ukimzingua anakuzingua, haogopi tena. Sasa ewe mtu mzima mwenzangu, fanya haya:
- Punguza ulevi na kujiamini kupita kiasi.
- Acha kupost status za WhatsApp zisizoeleweka; mara nyingi hushusha heshima yako.
- Punguza kutongoza ovyo, haswa mabinti wadogo.
- Tenga muda wa kusimamia miradi yako binafsi kuliko kubase sana na hiyo ajira.
- Mke ni muda wa kumuheshimu na kumpenda mume; na mume mjali na kumpa heshima mkeo.
- Epuka kuamua mambo magumu peke yako, kama vile ukidhulumiwa au kutapeliwa; badala yake shirikisha mamlaka za utetezi au usuluhishi.
- Kwa wenye vipato vikubwa, ajiri dereva akuendeshe, pamoja na kuwa na mwanasheria, japo si lazima.
- Jitoe, acha kiburi, shiriki kwenye misiba, makongamano na vikao mbalimbali; shiriki mambo yote ya kijamii ikiwa nafasi inaruhusu.
- Anza kusali au kuswali.
- Ishi maisha yako uliyochagua, ila usivunje sheria za nchi.