Siku zote ukitaka watu wakusikilize kuwa fair kwenye kukemea mabaya na kusifia mazuri usiwe na any kind of biasness vinginevyo utaonekana mnafiki kama wanafiki wengine tu, na kingine nilishakuambia kwenye suala la ngono na mahusiano hakuna namna unaweza ukaihukumu jinsia moja ukaiacha nyingine, kwa sababu hilo ni tendo ambalo ili lifanyike linahitaji uwepo wa jinsia zote mbili huwezi kusema eti jinsia moja ikilifanya ni sahihi ila jinsia nyingine ikilifanya ni kosa
Yani logically ni either hilo tendo liwe sahihi kwa wote au liwe kosa kwa wote kulingana na mazingira na siyo mnasingizia eti ni nature ilihali ni social constructs tu, jamii nyingi hasa za kiafrika zimekuwa na mitazamo fulani ambayo haitumii logic bali lengo lake ni ili mradi kuwakandamiza tu wanawake na kuwanufaisha wanaume, maana ukitumia common sense tu ukaangalia hiyo mitazamo unaona mingi haina uhalisia bali ni hisia na mihemko tu kitu ambacho ni far from nature