Mapinduzi ya kiuchumi nchi hii yanaitaji mabadiliko ya haraka katika sekta tatu

Thailand

JF-Expert Member
Nov 15, 2019
262
778
1. Kuinua na kuhimiza kilimo cha umwagiliaji.

Hiki ni kitu muhimu kutoka kutegemea mvua za msimu, serikali iweke na kuwezesha UKUAJI WA SEKTA YA KILIMO.

Tanzania tuna fursa ya maeneo bora ambayo sasa yametelekezwa kama mapori, yana udongo wa rutuba vyanzo vya maji ya mito na underground. Kinachotakiwa ni serikali kuwezesha channel ya upatikanaji wa maji hayo huko mashambani ili kilimo kiweze kuwa ni non stop in Tanzania.

Tanzania ina kopa pesa nyingi nje lakini pesa yote hiyo maranyingi inakwenda kwenye matumizi yanayochochea mwishoni mfumuko wa bei na hivyo ongezeko la gharama za maisha unakuwa mkubwa, lakini kama serikali ingejitaidi kununua hata tractors na mashine kama hizi za kilimo.

combine-flickr-David-wright.jpg

67a1068c57b89d6dfef94490577cd113.jpg

Vifaa hivyo ndo vingekuwa vipau mbele vyetu kila tunapopata pesa za mikopo kutoka nje. Kwa maana katika Uchumi kama mkopo unaupeleka kwenye uzaliahaji ina maana kiuchumi haina shida kwa sababu hivyo utakavyozalisha hapo kwenye kilimo vitasaidia nchi kujikwamua kutoka utegemezi wa nchi tajiri.

Mfano wa hivi karibuni, masokoni bei ya vyakula inazidi kupanda na endapo kama hakutakuwa na serious measure wananchi wanaenda kuteseka sana kwa kukosa chakula, ukosefu wa chakula hauumizi wapinzani pekee hata wana chama wa Ccm wanapitia kipindi hichohicho. Maumivu yakiendelea hivi kwa wananchi hata serikali iliko madarakani haitakuwa na amani maana kila kona ni kilio cha njaa kima ilivyo somalia inavyoteseka now.


2. Serikali wezesha upatikaji wa nishati ya umeme kwa urahisi.

Hakuna ndoto ya nchi ya viwanda pasipo UMEME WA UHAKIKA. Fikiria baada ya kutoka kwenye kilimo kikubwa( Agrarian Revolution kama Europe na USA walivyoanza ndo wakaja kwenye Industrial revolution) kama tulivyo ona hapo juu unahitaji umeme wa uhakika ili kuwezesha usindikaji wa bidhaa za kilimo katika ubora unaofaa kwa ajili ya masoko ya kimataifa. Hatuwezi kwenda kimataifa kama nchi, kama umeme wetu ni wa kusua sua kama ilivyo sasa.

Hivyo kwa kuwa bwawa la nyerere limeshakula pesa zetu watanzania, NAKUOMBA SANA SANA MAMA SAMIA PIGA KAMBI HAPO BWAWANI ILI KUONA LINAKAMILIKA KWA WAKATI. Pinga siasa kwenye jambo hilo, umeme sio swala la mwendanzake hilo ni jukumu lako likifanikiwa sifa zitarudi kwako na watanzania wote. Watanzania tunaitaji umeme wa uhakika kwa bei nafuu japo najua kuna shinikizo bei ya umeme kupandishwa juu na kukatika hovyo hovyo, HII INAUWA UCHUMI WA NCHI NA WA WAJASIRIAMALI WADOGO kama vinyozi na mashine za kusaga na viwanda vidogo.


3. ELIMU, ELIMU, ELIMU.

Nchi ya Tanzania inaitaji maabadiliko ya Elimu ya haraka ili kuona nchi inapiga hatua,
Kama nchi haitakiwa kuendelea kulea mifumo mibovu ya elimu kama iliyopo hivi sasa. Mfano haiwezekani nchi ikaruhusu wananchi wake wakawa na mifumo miwili tofauti katika kutoa elimu kwa watoto wake.

Kama taifa inabidi kufuta hiki kitu kinachoitwa shule za English medium na kayumba au Swahili medium.

Napendekeza tuwa na ENGLISH MEDIUM kwa shule zote za serikali na binafsi ili kufuta matabaka yanayozalishwa kwenye elimu yetu na elimu mbovu kwa watoto wanaotoka shule za serikali. Kiswahili libaki kama somo wakati English itamalaki kwenye ufundishaji wa masomo yetu hasa ya sayansi. Nasisitiza English kwa sababu kama nchi bado tunategemea biashara na technology kutoka katika nchi zilizoendelea.

Elimu yetu ya kidato cha sita inaitaji mabadiliko makubwa sana. Haiwezekani mwanafunzi aliyefeli kidato cha nne anakutwa kazini baada ya kusoma certificate na diploma huku aliefaulu na kwenda kidato cha tano na sita hana ujuzi wowote anaorudi nao mtaani.

Ikibidi elimu ya kidato cha tano na sita inaweza badilishwa iwe ni ya practical base, mfano unakuta shule kama ya Bagamoyo Sec ipo pembezoni mwa bahari kwanini elimu ya watoto isiwe either kutengeneza mangalawa, meri, uvuvi baharini, uwekezaji kwa kutengeneza vyombo vya utalii kwenye fukwe.

Nadhani tusaidie elimu yetu iwe inayowasaidia vijana kuona fursa zinazowazunguka kwenye mazingira yenye practical case nyingi sana. Hapo tutakuwa tumetoka kwenye ile elimu ya kikoloni ambayo haisapoti mazingira sasa na mwisho watoto wetu wanapitia wakati mgumu wa ukosefu wa ajira kisa maamuzi ya viongozi wetu.

Kwa leo naomba kuishia hapo karibu kwa mjadala.
 
Thailand mchango wako ni mzuri..ni jambo la kusikitisha kwa nchi yenye miaka 60 baada ya uhuru, ukame wa mwaka mmoja maisha yamekuwa magumu na hasa upatikanaji wa chakula, tafsiri ya hali hii ni kwamba bado hatujaweza kufanya kile kinachotakiwa kufanyika kwenye kilimo, wakati mwingine unawaza pengine ni kutokana na uongozi kutojua nini cha kufanya kwa ajili ya wilaya, mkoa na taifa..nchi yetu unaweza igawa katika makundi mawili, kuna wale wamezaliwa pwani au mjini na wale wamekulia kijijini au bara, ni ukweli usiopingika mazingira ni mwalimu mzuri katika maisha ya mwanadamu hasa kwenye umri 7 - 25 tunakosea tunapodhani mtu aliyekulia pwani au mjini anaweza kuwa DC au RC kwenye wilaya au mikoa ya wakulima na wafugaji, hawezi kuwa na mchango wowote kwa aliyemteua au watu anaowaongoza..mimi naamini kama DC au RC anapewa majukumu ya kufanya na malengo kufikia kwa muda fulani kutokana na eneo analopewa kuongoza, nchi yetu ingekuwa mbali sana kwenye uzalishaji unaotokana na kilimo, ufugaji na uvuvi...hivyo tatizo la kwanza la hali tuliyo nayo ni USIMAMIZI USIOFAA kutumia rasilimali tulizo nazo..niishie hapa kwanza.
 
Hawana akili hiyo ,huwa naamini kabisa nchi kubwa na yenye resources zote hizi mfano land and water ni rahisi kuitransform kuwa nchi tajiri kama ungekuwa na viongozi wenye akili na morals za uongozi na passion ya kuleta mabadiliko ya kweli .

Mfano : wote tunajua kilimo chenye Tija ni kilimo kinachohitaji mitaji na equipments za kisasa na pia wafanyakazi wenye utaalamu WA kuoperate mitambo ,kuhudumia mazao . Sasa serikali kila siku inakopa hizo trillions kuwekeza kwenye vitu vya kipumbav badala ya kwenye tangible things zenye multiplying effects kwenye uchumi WA mwananchi wa kawaida ,mfano Kwani nini hizo trillions zisitumike kuwavuta wazalishaji WA mitambo ya kilimo mfano marsey Ferguson na John deere Kwa kuwapa incentives kama vile punguzo kubwa la Kodi na kuwapa maeneo bure ya kuja kuanzisha viwanda vya kuzalisha mitambo ya kilimo hapa Tanzania ili watu wetu wengi wapate ajira in the mean time pia BEI ya hizo machineries mfano tractors kupungua Kwa sababu gharama za uzalishaji WA hiyo mitambo itakuwa Chini tokana na punguzo kubwa la Kodi pia wawekezaji kupewa ardhi bure na subsidies kiasi na serikali ili mkulima WA kawaida Tanzania aweze kuafford kuzinunua hizo machines na kufanya kilimo chenye tija . Pia hapo hapo tutainunua GDP Kwa kuuza hiyo mitambo nchi za jirani na Africa nzima Kwa kuanzia ,

Huku sekta ya kilimo inainuka na kuongeza pato la mkulima na nchi ,pia kuzalisha ajira Kwa upande WA uuzaji WA mazao nje ya nchi pia viwanda vya uchakataji WA hayo mazao Kwani production ikiwa kubwa itawashawishi wawekezaji WA viwanda vya uchakataji WA mazao na kuzalisha pembejeo kama mbolea na madawa ya kilimo kuongeza mitaji na kuwekeza Tanzania na hivyo ajira zinazalishwa na Kodi toka kwenye hivyo viwanda inaongeza pato la nchi .

Nchi kama Tanzania kuwa masikini ni aibu Sana ,hii nchi haikutakiwa kuwa hivi ilivyo ,ilitakiwa kuwa moja Kati ya nchi tajiri kabisa Africa na hata Duniani .

Hawa wapuuzi wanakopa pesa wanaenda kuwekeza kwenye ujinga
 
Umewaza vema mkuu tatizo taifa letu halijawahi pata kiongozi mwenye uthungu wamaendeleo yataifa kwaujumla wengi mawazo yao Nika v8 holder nkuxhakata pis kiubua
Mungu libaliki taifa letu

Sent from my TECNO B1f using JamiiForums mobile app
 
Umenena vema, ila kwenye lugha ya kufundishia iwe lugha yetu na kingereza tusome kama lugha ya kigeni
Sasa haya matabaka kwenye elimu yetu tutayaondoaje basi ni bora shule zote tuwe na elimu sawa yaani swahili medium lakini je viongozi wetu wataruhusu watoto wao kusoma mfumo wa swahili speaking kutokea primary?
 
Thailand mchango wako ni mzuri..ni jambo la kusikitisha kwa nchi yenye miaka 60 baada ya uhuru, ukame wa mwaka mmoja maisha yamekuwa magumu na hasa upatikanaji wa chakula, tafsiri ya hali hii ni kwamba bado hatujaweza kufanya kile kinachotakiwa kufanyika kwenye kilimo, wakati mwingine unawaza pengine ni kutokana na uongozi kutojua nini cha kufanya kwa ajili ya wilaya, mkoa na taifa..nchi yetu unaweza igawa katika makundi mawili, kuna wale wamezaliwa pwani au mjini na wale wamekulia kijijini au bara, ni ukweli usiopingika mazingira ni mwalimu mzuri katika maisha ya mwanadamu hasa kwenye umri 7 - 25 tunakosea tunapodhani mtu aliyekulia pwani au mjini anaweza kuwa DC au RC kwenye wilaya au mikoa ya wakulima na wafugaji, hawezi kuwa na mchango wowote kwa aliyemteua au watu anaowaongoza..mimi naamini kama DC au RC anapewa majukumu ya kufanya na malengo kufikia kwa muda fulani kutokana na eneo analopewa kuongoza, nchi yetu ingekuwa mbali sana kwenye uzalishaji unaotokana na kilimo, ufugaji na uvuvi...hivyo tatizo la kwanza la hali tuliyo nayo ni USIMAMIZI USIOFAA kutumia rasilimali tulizo nazo..niishie hapa kwanza.
Nakubaliana na wewe tatizo lingine nchi ni kwamba makada wa chama ndo wanapewa mamlaka ya kuongoza taasisi nyeti kama uwaziri, ukuu wa mikoa na wilaya. Lazima kupata viongozi kutokana na taaluma na ujuzi wa hali ya juu kwenye sekta husika.
 
Hawana akili hiyo ,huwa naamini kabisa nchi kubwa na yenye resources zote hizi mfano land and water ni rahisi kuitransform kuwa nchi tajiri kama ungekuwa na viongozi wenye akili na morals za uongozi na passion ya kuleta mabadiliko ya kweli .
Mfano : wote tunajua kilimo chenye Tija ni kilimo kinachohitaji mitaji na equipments za kisasa na pia wafanyakazi wenye utaalamu WA kuoperate mitambo ,kuhudumia mazao . Sasa serikali kila siku inakopa hizo trillions kuwekeza kwenye vitu vya kipumbav badala ya kwenye tangible things zenye multiplying effects kwenye uchumi WA mwananchi wa kawaida ,mfano Kwani nini hizo trillions zisitumike kuwavuta wazalishaji WA mitambo ya kilimo mfano marsey Ferguson na John deere Kwa kuwapa incentives kama vile punguzo kubwa la Kodi na kuwapa maeneo bure ya kuja kuanzisha viwanda vya kuzalisha mitambo ya kilimo hapa Tanzania ili watu wetu wengi wapate ajira in the mean time pia BEI ya hizo machineries mfano tractors kupungua Kwa sababu gharama za uzalishaji WA hiyo mitambo itakuwa Chini tokana na punguzo kubwa la Kodi pia wawekezaji kupewa ardhi bure na subsidies kiasi na serikali ili mkulima WA kawaida Tanzania aweze kuafford kuzinunua hizo machines na kufanya kilimo chenye tija . Pia hapo hapo tutainunua GDP Kwa kuuza hiyo mitambo nchi za jirani na Africa nzima Kwa kuanzia ,
Huku sekta ya kilimo inainuka na kuongeza pato la mkulima na nchi ,pia kuzalisha ajira Kwa upande WA uuzaji WA mazao nje ya nchi pia viwanda vya uchakataji WA hayo mazao Kwani production ikiwa kubwa itawashawishi wawekezaji WA viwanda vya uchakataji WA mazao na kuzalisha pembejeo kama mbolea na madawa ya kilimo kuongeza mitaji na kuwekeza Tanzania na hivyo ajira zinazalishwa na Kodi toka kwenye hivyo viwanda inaongeza pato la nchi .
Nchi kama Tanzania kuwa masikini ni aibu Sana ,hii nchi haikutakiwa kuwa hivi ilivyo ,ilitakiwa kuwa moja Kati ya nchi tajiri kabisa Africa na hata Duniani .

Hawa wapuuzi wanakopa pesa wanaenda kuwekeza kwenye ujinga
mlishaambiwa na Gwajima kuwa nchi haina maono kila kiongozi anayeingia madarakani ni copy and paste.
 
Back
Top Bottom