Mapigano ya kugombea ardhi yaua Tegeta

Mapigano ya kugombea ardhi yaua Tegeta

Niko likizo mkoani nimeona taarifa ya Habari ITV saa 2 usiku, Nilichokiona kimenisikitisha hakuna tofauti na Kenya (Post election) Rwanda (Genocide) Vijana wa kitanzania wameshika mapanga wanawakata watanzania wenzao, Very Sad!!!

Serikali (Polisi) inasema waache wamalizane wa mwisho ndo aje! What a shame! Haya ndiyo matokeo ya serikali legelege kama hii ya Tanzania, Jana wabunge wameisema serikali kuwa ni legelege na leo(7/4/11) yanathibitika. Nguvu ya watu inapozidia nguvu ya mafisadi maisha ya watu wasio na ajira yanapotea kwa ujira wa Tsh 50,000/= tu.

siamini tena kuwa Tz ni nchi ya amani na utulivu hata kwa bunduki, nasema siamini ng'o!!
 
Inasikitisha Sijui serikali hii inatupeleka wapi? Nimesikia taarifa ya habari ITV kuwa polisi baada ya kuarifiwa kuwa kuna tafrani huko wao walijibu kuwa " wamalizane wenyewe halafu wa mwisho ndio aje kutoa taarifa" sasa kama kuna ukweli hapo nadhani IGP achukue hatua dhidi yao, lakini utaratibu wa hao Mwangata kutumia vijana wasio na ajira kama watu wa kusimamia sheria kama kuna hukumu ni makosa wapaswa kuwajibishwa kwa mauwaji hayo.
 
Siamini kuwa intelijensia ya POLISI haikuona leo kutakuwa na uvujifu wa amani na badala yake wakalala tu hawakuwazuia hao Mwangata kwenda kuvunja hizo nyumba. Sasa wangetumia hiyo intelijensia wangezuia mauwaji hayo, au intelijensia ilikwenda likizo baada ya vurugu zan Arusha zilizo sababishwa napolisi?
 
Mwanzo nilikuwa ninachukulia hii habari kama nyingine ila baada ya kuona hii clip nimeshawishika kuwa hii ni habari kubwa na nyeti sana kwenye ustawi wa public safety kwenye nchi yenye Govt for the people by the people hasa ukiangalia mlolongo wa matukio

  1. Mabaunsa 400 wameletwa na Kampuni ya udalali kuvunja nyuma bila kumtafuta mwenyekiti wa mtaa na kuomba ulinzi wa vyombo vya dola wakati wa utekelezaji, kama walikuwa na haki ya kufanya hivyo
  2. Mwenyekiti wa mtaa na viongozi wanawasiliana na vyombo vya dola kwa lengo la kuepusha maafa lakini, kwa jeuri na uzembe wa hali ya juu hasa kwa kujua hawakuitwa na kiongozi wa juu wa serikali kulinda masilahi ya CCM basi wanaona kuwa maisha ya binadamu wengine is useless
  3. Polisi wanatoa kauli za dharua wakati wa dharula kuwa acha wananchi wauane na wa mwisho atakuja kuripoti polisi, hii ni kauli inayoweza kufanya wizara nzima inayohusika na usalama wa raia kuvunjwa na kuundwa upya katika nchi za demokrasia ya kweli na zenye kulinda masilahi ya wananchi. Isipofanya hivyo uchaguzi ujao inakuwa ni issue kubwa ya kupoteza kura
  4. Watu watano wanapoteza maisha hapo ndipo tutakapoona Full force ya kamatakamata kwa lengo la kujikosha na ku-sucrifice polisi aliyejibu utumbo kwa kumuhamishia sehemu ingine.
My Take: Hili suala linatakiwa kuondoka na Askari wote waliopigiwa simu kuwa kuna ugomvi, yaani kuanzia Mwema, Kova na wengine wote wa upande wa mawasilino. Pia kwa upande wa wanasiasa waziri muhusika anatakiwa kuwajibika kwa makosa ya askari wake ili kuongeza public trust

Waliouwawa ni mabaunsa ambao kwa jinsi inavyooneka wengi wao ni jobless ndiyo maana wakawa tayari kurisk maisha yao kwa ujira wa Tshs 50,000. Kundi hili ni lazima litakuwa linajumuisha wavuta bangi na vibaka. wasiwasi wangu ni kuwa kwa wale waliopona na kukimbia wanweza kuwa na moyo wa kulipiza kisasi kwa kupoteza wenzao watano na kuamua kuvamia mivumoni usiku wa manane kutoa kibano cha haja kwa mkazi mmojammoja hasa wale waliowa identify kuwa ni frontliners. Hapa busara itumike hasa kuwapoza mabaunsa waliosalia kwani nina hakika kuwa aliyewaleta anawafahamu. Upande mwingine ni kuwa aliyewaleta nae anaweza kugeukwa na mabaunsa hawa baada ya kuwapeleka machinjioni na kuwakimbia.

Nina hakika kabisa kuwa kama KOVA angepigiwa simu kuwa CHADEMA wanaandamana bila kibali basi isingechukua dakika kumi na tano kwa magari FFU waliosheheni silaha zote nzito kufika eneo la tukio kuwavurumusha ili apate credit kwa viongozi wa CCM
 
nimebahatika kuangalia taarifa ya habari ya itv ya saa 2 leo. ingawa nlikua najua kwamba nchi yetu haina hiyo amani hawa jamaa wetu wa ccm wanahubiri kila siku,lakini sikujua watanzania tumekata tamaa vile. nimeona ukatili ambao sikuamini watanzania tunaweza katana mapanga na mashoka kiasi kile. kama tutaendelea hivi natabiri hivi karibuni nchi yetu itashuhudia mauaji ya kimbari.
 
Sio ili apate credit, ili aweze ku retain kazi yake.

Sasa tuache domokaya lazima tuanze mkakati wa kushinikiza wakina mwema kujiuzulu na huyo JK wao. Lakini ndugu zangu watanzania tuanze kwa kupongezana, yule aliyesema ya misri hayawezekani hapa bado anashangaa? Mimi nimefurahi sana kwamba sasa watanzania wanajua njia.

Na sitashangaa kama huyo mwenye kampuni ya udalali na huyo mwekezaji feki hawatachukuliwa hatua kwa sababu walifadhili CCM kwenye uchaguzi uliopita.

Hebu fikiri unapotuma jeshi la vibaka 400 kwa mwanamke mwenye watoto wa kike na kiume, hawa wangeishia kuwabaka hao wenye nyumba maana wameshajengewa dhana kwamba wanamakosa na wala si chochote mbele yao hawana haki kwa kuwa tu mali yao imetamaniwa na bwana wao. Hawa wangeweza kuwalawiti na kuwabaka watu wote kwenye nyumba hiyo tena in public, tunaomba wanasheria wajitolee kufungua kesi hiyo against jamhuri haraka iwezekanavyo.

Na sisi wananchi tuendelee kusaidiana katika kulindana, nawapongeza sana sana sana viongozi wa huko tegeta na wakazi wote hasa vijana waliotimiza ushujaa huu, hongereni sana, serikali ya JK na CCM ijiuzulu sasa 2015 mbali sana. Ni kweli wamezoea kula damu labda ndio hayo majini tuliyoambiwa na shehe yahaya kwamba yanatoa ulinzi, tusiwachekee watatumaliza Mwema, Kova, Rugimbana (aliyepewe uongozi kwa kukimbiza mwengi na kuwa karibu na mama mkapa, yale yale ya Lazaro Nyalandu, hivyo ndivyo vigezo vya uongozi wa juu kwa serikali yetu ya chama cha mapinduzi.

Mstahiki meya Mwenda, hebu ongoza haya mapambano maana umeanza vizuri,
 
Sikuamini zile picha za ITV kwamba naona watanzania wakiwacharanga watanzania wenzao vile. Hata kama wananchi tumechoshwa na dhuluma na uonevu wa watawala na mafisadi,lkn ile haikua njia sahihi kuwaua kikatili watanzania wenzetu. Waliopoteza maisha ni wananchi masikini wenzetu. Wameponzwa na elfu 50!! Poleni sana wafiwa.
 
Mbona kila kitu kinakuwa politicized?....kama mnadhani chadema kilianzishwa ili kuwapa ardhi walalahoi hapo mmekosea, CDM ni chama kinachotetea privatisation na nina ushahidi.Na haya ndio mambo ya privatisation.

Hapa Tanzania ni mikoa ya Moshi, Arusha na Mara ndio kihistoria hawana communal land tangu enzi za ujamaa watu wa mikoa hii wamekuwa wakiuana kwa ajili ya ardhi, they don't have a communal culture kwa kuwa ni wachungaji. Na chadema inawapata sana watu wa mikoa hii kwa kuwa walikuwa against socialism from the getsgo!

Sasa hivi wanawadanganya mayanki with that peoples power crap! waki dilute their policy from right wing capitalists to centrist (what the hell is centrist anyway?).

Sehemu kama za Tegeta yalikuwa ni mapori tu like 20yrs ago,watu wa pwani ni nadra sana kupigania ardhi kubwa kwa kuwa naturally wao ni peasants na fishermen who don't really need big plantations. Huu ubinafsishaji wa ardhi za watu maskini ni sera zilizopiganiwa sana na kina Mtei enzi za Nyerere,sasa tunaona matokeo yake.

Haya mambo yapo Angola, Mozambique, Ethiopia n.k ambapo walala hoi walipewa ardhi during villagization and now Serikali zao zinasema arhdi yao haikuwa planned na hazina hati.

Na sasa mnataka nchi iwe ya kibepari,matokeo yake ni kama haya!
 
Masikini taifa hili halina mwenyewe, kila mtu amekuwa mlafi kama nguruwe pori, wenye husda na wasio na utu, tukianza na rais mwenyewe na wasanii wote wanaomzunguka. The emergence of anarchy society.
 
This is not fair. Hata kama serikali inashindwa kuwahakikishia raia wake ulinzi na usalama wa uhakika, bado tuna haki ya msingi ya kupata habari kwa wakati muafaka
 
Hayo ma auction mart nayo hovyo! Yamekuwa vikaragosi vya wenye nazo.
 
This is not fair. Hata kama serikali inashindwa kuwahakikishia raia wake ulinzi na usalama wa uhakika, bado tuna haki ya msingi ya kupata habari kwa wakati muafaka

Uliangalia taarifa ya habari saa mbili usiku?mbona walitangaza na kusema watu 2 wamekufa!
 
Habari nilizozipata ni kuwa "MMILIKI" wa hilo eneo ni D. Yona Jr. Huyu ndiye aliyekimbizwa kwa mawe na wananchi akiwa kwenye Toyota Hilux!

Big UP kwa wananchi wa Mivumoni - Mlichofanya ni vizuri kikaigwa na wale wote wanaodhulumiwa nchi nzima..

Kwa waliokufa na waliowatuma wote ni sawa sawa tu - Kama unapewa 50,000/- na unakubali kwenda kubomoa nyumba ya 10mil plus, then wewe pia unastahili kupigwa panga na kufa!
 
TBC wametangaza hii habari ila tu wamepunguza idadi ya waliokufa!
 
u
This is not fair. Hata kama serikali inashindwa kuwahakikishia raia wake ulinzi na usalama wa uhakika, bado tuna haki ya msingi ya kupata habari kwa wakati muafaka
Nazjaz, this is not fair, hukuangalia news za TBC halafu unaibuka na lawama!. TBC walitangaza tena kwa kitumia authority. Kunapotokea ajali au vurugu, taarifa ya maafa inatakiwa kutolewa na authority police, serikali na kuwa cross checked na hospitali. Wengine wote wamesema vifo watu 5, TBC wao wamesema vifo ni viwili. They are right idadi huweza kuongezeka wakati wowote usishangae ukisikia sasa ni watu 10!.
 
Mkuu binafsi sijakuelewa, hiyo miloni 96 kwa nyumba 26 umeiona ni kubwa au ni ndogo? naomba uniweke wazi ili tuelimishane kitu

Ina maana wastani wa sh milion 3.7 kujenga kila nyumba. Ni kazi kwako kuamua kama hiyo ni ndogo mno au kubwa mno
 
Kwani aliesababisha matatizo ya ardhi na utaratibu wa kifisadi kugawa ardhi ni nani kama sio ccm na kikwete? Wamekaa madarakani kazi zao kusafiri nchi za nje na kukaa majumba ya serikali bila hata aibu. Hivi vita vya kupigania resources vitaendelea mpaka wananchi tupate "Katiba" na "Sheria" za maana kwa manufaa kwa wananchi.

Legacy ya kikwete inaendelea, ignorants wanadai wanaonewa!
 
Mwanzo nilikuwa ninachukulia hii habari kama nyingine ila baada ya kuona hii clip nimeshawishika kuwa hii ni habari kubwa na nyeti sana kwenye ustawi wa public safety kwenye nchi yenye Govt for the people by the people hasa ukiangalia mlolongo wa matukio

  1. Mabaunsa 400 wameletwa na Kampuni ya udalali kuvunja nyuma bila kumtafuta mwenyekiti wa mtaa na kuomba ulinzi wa vyombo vya dola wakati wa utekelezaji, kama walikuwa na haki ya kufanya hivyo
  2. Mwenyekiti wa mtaa na viongozi wanawasiliana na vyombo vya dola kwa lengo la kuepusha maafa lakini, kwa jeuri na uzembe wa hali ya juu hasa kwa kujua hawakuitwa na kiongozi wa juu wa serikali kulinda masilahi ya CCM basi wanaona kuwa maisha ya binadamu wengine is useless
  3. Polisi wanatoa kauli za dharua wakati wa dharula kuwa acha wananchi wauane na wa mwisho atakuja kuripoti polisi, hii ni kauli inayoweza kufanya wizara nzima inayohusika na usalama wa raia kuvunjwa na kuundwa upya katika nchi za demokrasia ya kweli na zenye kulinda masilahi ya wananchi. Isipofanya hivyo uchaguzi ujao inakuwa ni issue kubwa ya kupoteza kura
  4. Watu watano wanapoteza maisha hapo ndipo tutakapoona Full force ya kamatakamata kwa lengo la kujikosha na ku-sucrifice polisi aliyejibu utumbo kwa kumuhamishia sehemu ingine.
My Take: Hili suala linatakiwa kuondoka na Askari wote waliopigiwa simu kuwa kuna ugomvi, yaani kuanzia Mwema, Kova na wengine wote wa upande wa mawasilino. Pia kwa upande wa wanasiasa waziri muhusika anatakiwa kuwajibika kwa makosa ya askari wake ili kuongeza public trust

Waliouwawa ni mabaunsa ambao kwa jinsi inavyooneka wengi wao ni jobless ndiyo maana wakawa tayari kurisk maisha yao kwa ujira wa Tshs 50,000. Kundi hili ni lazima litakuwa linajumuisha wavuta bangi na vibaka. wasiwasi wangu ni kuwa kwa wale waliopona na kukimbia wanweza kuwa na moyo wa kulipiza kisasi kwa kupoteza wenzao watano na kuamua kuvamia mivumoni usiku wa manane kutoa kibano cha haja kwa mkazi mmojammoja hasa wale waliowa identify kuwa ni frontliners. Hapa busara itumike hasa kuwapoza mabaunsa waliosalia kwani nina hakika kuwa aliyewaleta anawafahamu. Upande mwingine ni kuwa aliyewaleta nae anaweza kugeukwa na mabaunsa hawa baada ya kuwapeleka machinjioni na kuwakimbia.

Nina hakika kabisa kuwa kama KOVA angepigiwa simu kuwa CHADEMA wanaandamana bila kibali basi isingechukua dakika kumi na tano kwa magari FFU waliosheheni silaha zote nzito kufika eneo la tukio kuwavurumusha ili apate credit kwa viongozi wa CCM

This is a failure of the Government!
Serikali ya Mkoa ilikuwa wapi?
The see-all-hear-all security system ilikuwa wapi?
Polisi walikuwa wapi?
Mlolongo wa matukio yanayoonyesha kushindwa kwa Government machinnery kuzuia mauaji haya ndiyo kitu kinachonitisha.
Kama yametokea hapa hapa DSM kwenye kitovu cha Serikali basi tumekalia kuti kavu.
 
Hivi ndivyo Katiba Ipeganiwe na haki ya kila mtanzania. Hakuna ku-back down anymore. This good warning to Kikwete na serikali yake!
 
Back
Top Bottom