"Mapenzi yanasumbua wajinga"

"Mapenzi yanasumbua wajinga"

Mm ndo maana cku hiz nikiwa na demu, akinpenda poa, asiponipenda pia ni poa, nipo 50%- 50%
 
Sawa inawezekana sijawahi kuwa nae..but I always make sure that my happiness is secured..
 
hujawahi kua na mwanamke mzuri wewe mtoa mada........
Sawa ni mwanamke mzuri, ila akikuchoka akakutema hakuna kitu cha maana zaidi ya kutafuta pengine penye marisho bora tofauti na hapo utaishia kuumia tu, nikupe siri tu, mwanamke anapenda sana kubabaikiwa so utakuacha umfate fate weee, badilikeni ohoo!
 
Mi huyu nilie nae najua hanipendi anapenda hela tu.....
Na mie simpendi pia ila wacha namlia timing siku isiyo na jina atajikuta analia bila kulizwa
 
Rahisi kuongea wandugu! Hakuna anaependa kuumia na kuwa mtumwa na hata kuondokana na utumwa unahitaji nguvu ya ziada, siyo kwa maneno tuu hayo japo ingekuwa rahisi hivyo wengi wasingekuwa wanahangaika. shukuru Mungu tuu pale unapokuwa umefikia hatua ya maamuzi hayo afu ukawa na furaha, kuudanganya moyo wenye mazoea ni kazi sana na huhitaji mda smtz!

Ni hayo tuu!!!
 
  • Thanks
Reactions: DLS
Back
Top Bottom