Mapenzi yananiumiza naombeni uzoefu wenu tafadhali

Mapenzi yananiumiza naombeni uzoefu wenu tafadhali

LAKI

Senior Member
Joined
Jun 12, 2013
Posts
100
Reaction score
37
Salamu kwa wote,

Mi ni yuleyule mpenzi wangu hataki tukacheki afya,

Jamani mapenzi yananiumiza sina raha ndugu zangu, nampenda sana huyu mpenzi wangu lakini yeye simuelewi.

Nina miaka 27, nina kazi ya kudumu, tumekuwa tukigombana mara kwa mara nakuwa mdogo mambo yanaisha maisha yanaendelea.

Mara nyingi ananikwaza nikimuuliza ananitumia meseji za matusi, nikishauri kitu ansema hataki kushauriwa, tunaishi mkoa mmoja lakini hana time na mimi kabsa, cha ajabu mesg za kusema ananipenda hazikawii.

Napata wakati mgumu sana, hajawahi kuninunulia hata kazawadi ka shilling 500!hana muda wa kuspendi na mimi zaidi ya kuwasiliana kwenye simu na kila tukitofautiana iwe ni yeye chanzo au ni mimi ananitumia meseji za matusi, ninapohisi nimekosea namwomba msamaha but naambulia matusi, akinikosa yeye anarudisha kosa upande wangu na msg za matusi.

Anajifanya ni mbabe, na kama katili flani, ubahili ndo usiseme. Kanambia tuanze process za ndoa ila naogopa maana nawaza hivi tukioana atakuwa anatunza familia? maana anaoekana sio mtoaji hata kidogo japo anapata almost laki 3 kwa siku.

Pia atakuja kuacha matusi au atanitukana mbele za watu au watoto?

Naombeni ushauri wenu kichwa kinaniuma hapa nilipo nikifikiria na umri ndou unaenda.

asanteni.
 
Usiwe mjinga achana nae haraka sana
Utaumia kwa muda kidogo then utakaa sawa
 
Mbona ni kama unajipendekeza kwake wakati yeye hana time na wewe
 
Ukiolewa atakuwa anashinda nyumbani siku 6 za wiki ili kufidia muda huu ambao yuko busy lol.

Dada wenzio wakiwa wachumba mapenzi huwa motomoto wakioana yanabaki moto au kupungua kidogo wewe hujaolewa mapenzi yamedorora. unless kama wataka tu kuitwa mrs. ........ endelea na ndoa.
 
Kijana wakati ndio sasa , vunja huo uhusiano kungali mapema wala usifikirie kuingia na huyo dada kwenye ndoa, ipo siku tutakukuta juu ya paa unaota jua huku umejifunika blanketi..........kama hayo unayosema ni kweli, jikaze kisabuni muachane, utampata mwingine mutakayeendana na kukuheshimu.......kwanza pole sana.
 
hivi kitu kikikuumiza hujui kama unaumia, na ukiumia suluhisho hujui ni nini?
 
unasubiria filimbi ya kuambiwa achana nae... mapenzi ni kuheshimiana na wala si karaha kama upati raha upendo wako kwake usiwe mzigo kwako..... love is two way trafic okey..... think again is this love true? if no why u waste ure time their? and if yes why this thing happen?
 
kunywa dawa kwanza kichwa kipoe ndio uzungumze sasa....
 
Kijana wakati ndio sasa , vunja huo uhusiano kungali mapema wala usifikirie kuingia na huyo dada kwenye ndoa, ipo siku tutakukuta juu ya paa unaota jua huku umejifunika blanketi..........kama hayo unayosema ni kweli, jikaze kisabuni muachane, utampata mwingine mutakayeendana na kukuheshimu.......kwanza pole sana.

asante kwa ushauri, mimi ni mdada na sio me.
 
asante kwa ushauri, mimi ni mdada na sio me.

Oooh......samahani, dada ila ushauri ni huo huo mmoja, kama anakupenda kweli anapaswa akuheshimu na kukuthamini.
 
Back
Top Bottom