Mapenzi yamenitesa nasema sasa basi

Mapenzi yamenitesa nasema sasa basi

Tangu nilipoamua kuyaweka kando mapenzi na masuala ya kuhusiana kwenye medula oblangata yangu......na nafasi yake ikachukuliwa na...mazoezi ya mwili, kula vizuri, kuvaa vizuri.....kuelekaeza nguvu zangu kwenye kujenga uchumi wangu......kuwa karibu na wapendwa wangu......nimeyaona mabadiliko chanya kwenye maisha kwa ujumla wake.......

Nilichojifunza ni kuwa mapenzi hayapiganiwi bali mapenzi huja natural....pindi unapoona unaanza kutumia nguvu na moyo wako kujaa shaka juu ya mapenzi basi jua umeshakuwa mfungwa kwenye gereza la mapenzi na ndio utakuwa mwanzo wa mahangaiko maishani mwako!!

THINK BIG , TAKE CONTROL OF YOUR DESTINY.......

FB_IMG_1754192284701.jpg
 
Poleni Sana mnaoteswa na hawa viumbe


Jana kuna jamaa naye ananipa stori amekaa na mwanamke Miaka mitatu kumbe aliolewaga Jana..mama mkwe ndo kamchana jamaa kwamba huyo NI mke wa mtu unapoteza naye muda .halafu wamejenga wote nyumban..
Hawa viumbe kuishi nao inahitaji akili ya kijanja yaani mfanye kama ndugu au rafiki zaidi..kingine ambao hamjaoa tafuteni wanawake wa nyumbani kijijini kwenu ikibidi hata ukoo wako na ukoo wako wanajuana vzr
Noma
 
Suala la mapenzi na siasa ni utapeli ambao siwezi kuwekeza ,siamini mtu hata siku moja.
 
Habari za usiku upande wangu nmekuwa na wakati mgumu wiki hii inayo Isha nilipogundua mpenzi wangu niliyempangia nyumba ameondoka bila taarifa ameenda kwa mwanaume mwingine huku ndugu zake wakiogopa kuniambia ukweli na Kila nilimuuliza ananiambia Yuko kwao lakini vitu vyake vyote ameacha ndani.

Hadi badae ya siku kazaa mama yake aliponitafuta na kuniambia ukweli alisema tulikuwa tunaogopa kukuambia maana huyu mwenzako amebadilika hakika nmeteseka hadi utendaji kazi wangu ukpungua nayalaani mapenzi mimi
Wako wengi hao tafuta pesa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom