Mapambano makali yanaendelea Kusini Magharibi mwa Rwanda

Mapambano makali yanaendelea Kusini Magharibi mwa Rwanda

Sio ta kudharau maana tycoon...tajiri sana mwenye ushawishi mkubwa sana Rwanda na jamii ya kimataifa Russesabagina amesema na yeye anawafund jamaa.

Hii ishu ni kubwa maana ni vita ya Watusi kwa Watusi na sio wahutu na Watusi tena...wote wana mkwanja na wote wana hasira.

I'm enjoying the show as usual...Let the rumble Begin.
Hahah aisee na unaamini kabisa kuna kitachotokea boss?Russasegina ndio unasema ana ushawishi Rwanda?

Just wait n see boss lkn
 
Kundi jipya la waasi la MRDC latangaza vita dhidi ya utawala wa Kagame Rwanda
Na RFIImechapishwa 18-07-2018 Imehaririwa 18-07-2018 Saa 16:40
2017-06-22t181625z_2084822424_rc1caa756c70_rtrmadp_3_rwanda-election_0.jpg
Rais wa Rwanda Paul Kagame.REUTERS/Jean Bizimana


Siku mbili baada ya kundi jipya la waasi la MRDC kutangaza vita dhidi ya utawala wa rais wa Rwanda Paul, Kagame, serikali ya nchi hiyo imesema kuwa madai ya mtu anayedai kuwa msemaji huyo Callixte Sankara Nsabimana ni ya uongo.

Hivi karibuni Callixte meja Callixte Sankara Nsabimana anayedai kuwa msemaji wa kundi hilo, alisem akuwa lengo la vita hivyo ni kuung'oa utawala wa Kagame na kubaini kwamba ni mwezi mzima sasa tangu majeshi ya kundi lake yakipigana na majeshi ya Rwanda katika msitu wa Nyungwe kusini mwa nchi hiyo.

Ameongeza kwamba majeshi yao yaliendesha mashambulizi ymnamo mwezi Juni katika kijiji cha Nyabimata karibu na msitu wa Nyungwe.

Kwa upande wake inspekta mkuu wa polisi Emmanuel Gasana amefutilia mbali madai ya kuepo kwa kundi la waasi katika msitu wa Nyungwe, huku akihakikisha kwamba kuna majambazi wachache ambao wamekua wakivuka na kuingia Rwanda na kuwapora watu katika kijiji cha Nyaruguru. Lakini polisi ilishughulikia vilivyo hali hiyo na majambazi hao waliweza kukimbilia eneo walitoka.

Meja Callixte Sankara Nsabimana, anatoka kabila la Tutsi na ni mjombake kiongozi wa upinzani aliye kizuizini nchini Rwanda Diane Rwigara. Meja Callixte Sankara amesema ni mwanajeshi aliyekuwa mshirika wa karibu wa rais Paul kagame kwenye kundi la lwaasi Rwanda Patriotic Front (RPF), madarakani leo nchini Rwanda, katika harakati za kupigania ukombozi.

Hivi karibuni Rwanda ilishuhudia mdororo wa usalama katika wilaya mbalimbali hasa wilaya ya Rusizi.
 
hahah Nikiona hizi habari za Rwanda nakumbuka kipindi kile cha uchaguzi 2015 jinsi Yericko Nyerere alivyokua anatulisha upepo khs Ukawa(Lowassa) akawa anasema wananchi jiandaeni kushona suti kwa ajili ya mzee kuapishwa hahah mpk sasa mzee ameshashinda kwa mbaaali saana,watu huku kitaa tukawa tunapiga shangwe na byere tu hahah sitasahau aise.

Sisi ni wepesi sana wa kupelekwa kwa hisia(emotional) zaidi kuliko pengine ukweli wenyewe.
 
Ungeandika kuwa ni tetesi.
mkuu upo... tetesi zina pelekea kuwa kweli... cheki wanavyo kanyagana viongozi wa nchi na ni vita ya takribani mwezi mmoja... lakini wameficha na kudai majambazi sasa sijui
 
Ungeandika kuwa ni tetesi.
Kundi la waasi la MRDC latuhumu kupambana na jeshi la Rwanda
  • Saa 7 zilizopita
  • BBC
_102575723_183a1b24-d1a4-4d54-86bf-20c1e864f602.jpg

Image captionMajor Callixte Sankara
Mamlaka nchini Rwanda zimetupilia mbali uvumi kuhusu kuwepo ukosefu wa usalama maeneo yanayozunguka msitu wa Nyungwe, ambapo kundi jipya la waasi wa MRCD linalodai kuwa linataka kuangusha uongozi wa Rais Paul Kageme linasemekana kuwa na ngome yake.

Akiongea na wenyeji wa wilaya wa Nyaruguru, inspekta mkuu wa polisi Emmanuel Gasana alisema kuwa licha ya majambazi wachache kuvuka na kuingia Rwanda na kuwapora watu eneo moja la Nyaruguru hali hiyo ilikuwa imeshughulikiwa vilivyo na vikosi vya usalama na majambazi hao kukimbilia eneo walitoka.

Kundi la MRCD (Rwanda Democratic Movement for Change) limetangaza rasmi uasi dhidi ya serikali ya Rwanda. Msemaji wa kundi hilo meja Callixte Sankara ameiambia BBC kwamba ni mwezi mzima sasa tangu majeshi ya kundi lake yakipigana na majeshi ya Rwanda katika msitu wa Nyungwe kusini mwa nchi hiyo ,na kwamba majeshi yao yamehusika katika mashambulizi ya mwezi uliopita katika kijiji cha Nyabimata karibu na msitu huo.

Je, huyu kiongozi wa kundi jipya la waasi Meja Callixte Sankara ni nani?
Ni machache yanayojulikana kuhusu Callixte Sankara, mtu aliyejitangaza kama naibu kamanda na msemaji wa kundi jipya la waasi la Rwanda Movement for Democratic Change.

Meja Callixte Sankara, kama avyojitambulisha kwa vyombo vya habari, ni mwanajeshi aliyekuwa mshirika wa karibu wa rais Paul kagame kwenye kundi la Rwanda Patriotic Front (RPF) katika harakati za kupigania ukombozi.

Alikuwa askari mwenye cheo cha chini baada ya RPF kushinda vita vya msituni na kuchukuwa hatamu za uongozi kufuatia baada ya kifo cha rais Juvenal Hybiamamana kwenye shambulzi la ndege.

Haijulikani kwanini Meja Sankara alikosana na utawala wa kagame, lakini alifungwa jela na mahakama ya kijeshi kwa kipindi kisichojulikana kutokana na kile kilichotajwa kama utovu wa nidhamu.

_102575724_5ea83c16-a315-444b-a6a1-43fd473ed4e8.jpg

Image captionMRCD linadaiwa kuwa ngome yake kwenye msitu wa Nyungwe
Baadaye alitoroka nchi na kukilmbilia taifa jirani la Tanzania alikotiwa mbaroni.

Juhudi za utawala wa Kigali wa kutumia waranti bandia za kutaka Dar es salam kumrudisha Meja Sankara Rwanda, ziligonga mwamba na hatimaye serikali ya Tanzania ilimwachilia mhuru na kumwezesha kusafiri uhamishoni Ufaransa.

Callixte Sankara badaye alijiunga na chama cha Rwanda National Congress (RNC) kilichioanzishwa mwaka wa 2010 na waliokuwa washirika wanne wa karibu wa rais Kagame, miongoni mwao mkuu wa zamani wa jeshi Jenerali Kayumba Nyamwasa.

Baada ya miaka kadha, ubishi ulizuka ndani ya chama cha RNC na kusababisha Meja Sankara na Jenerali Kayumba Nyamwasa kutafautiana.

Meja Callixte Sanaka alisomea uanasheria katika chuo kikuu cha Rwanda.Anatoka kabila la Tutsi na ni mjombake kiongozi wa upinzani aliyekizuizini nchini Rwanda Diane Rwigara.

Wakati huo huo kumekuwa na taarifa kuhusu ukosefu wa usalama katika baadhi ya maeneo ndani kwenyewe nchini Rwanda.

Mashambulizi ya kutumia guruneti yameshuhudiwa katika kipindi cha miaka mitano iliyopita. Maeneo ya makumbusho ya mauaji ya halaiki, masoko, vituo vya mabasi na mateksi vimekuwa vikilengwa mjini Kigali na eneo la Ruhengeri. Shambulizi la hivi majuzi la gurunedi lilitokea Juni 2017 kwenye wilaya ya Rusizi ambapo mtu mmoja aliuawa.
 
Wazungu wanakutumia na lazima ufuate masharti yao kama ya mganga na siku ukiyakiuka tu wanaunda waasi na kukupiga chini
Rejea Gaddafi na Sadam na wengine kibao wa Africa na Europe
Hahah kweli yajayo yanafurahisha,huko Rwanda hakuna hata jiwe moja limerushwa achilia mbali mlio wa risasi.

Jamaa Wako bize kujiandaa na ujio wa Rais wa Mozambique hapo kesho mjini Kigali
Hata zimbabwe ilikuwa hivi hivi mpaka tukasikia tamko la.umoja wa vijana wa chama cha zanu-pf kuwa yaonekanayo mtandaoni ni propaganda.


Nadhani unajua kipi kimetokea.
 
Hata zimbabwe ilikuwa hivi hivi mpaka tukasikia tamko la.umoja wa vijana wa chama cha zanu-pf kuwa yaonekanayo mtandaoni ni propaganda.


Nadhani unajua kipi kimetokea.
Fanya kitu kirahisi tu boss,unadhani mpk baada ya muda gani mapinduzi huko Rwanda yatakua yamekamilika?

Ili niku tag hapa hio deadline ya mapinduzi ikifika mkuu.
 
Wabongo mnapenda sana story za udaku. Sisi tupo Rwanda hapa Kigali muda huu na wala huo ujinga hatuusikii.
 
Wacha ninoe CV yangu najua punde UNHCR watatangaza ajira.
Ajira za huko ni tatizo... ila kila la kheri mkuu... hizi za kujuana na uzoefu wa kufanya kazi katk emergency kama huna ka master kakuongezee angalau sifa zaidi na waone aibu kidogo japo hawato ona kabisa... na wanawake wana nafasi kubwa ili ma HR na mabosi waweze fanya yao kwa kale ka ugonjwa ka rushuwa
 
Kundi la waasi la MRDC latuhumu kupambana na jeshi la Rwanda
  • Saa 7 zilizopita
  • BBC
_102575723_183a1b24-d1a4-4d54-86bf-20c1e864f602.jpg

Image captionMajor Callixte Sankara
Mamlaka nchini Rwanda zimetupilia mbali uvumi kuhusu kuwepo ukosefu wa usalama maeneo yanayozunguka msitu wa Nyungwe, ambapo kundi jipya la waasi wa MRCD linalodai kuwa linataka kuangusha uongozi wa Rais Paul Kageme linasemekana kuwa na ngome yake.

Akiongea na wenyeji wa wilaya wa Nyaruguru, inspekta mkuu wa polisi Emmanuel Gasana alisema kuwa licha ya majambazi wachache kuvuka na kuingia Rwanda na kuwapora watu eneo moja la Nyaruguru hali hiyo ilikuwa imeshughulikiwa vilivyo na vikosi vya usalama na majambazi hao kukimbilia eneo walitoka.

Kundi la MRCD (Rwanda Democratic Movement for Change) limetangaza rasmi uasi dhidi ya serikali ya Rwanda. Msemaji wa kundi hilo meja Callixte Sankara ameiambia BBC kwamba ni mwezi mzima sasa tangu majeshi ya kundi lake yakipigana na majeshi ya Rwanda katika msitu wa Nyungwe kusini mwa nchi hiyo ,na kwamba majeshi yao yamehusika katika mashambulizi ya mwezi uliopita katika kijiji cha Nyabimata karibu na msitu huo.

Je, huyu kiongozi wa kundi jipya la waasi Meja Callixte Sankara ni nani?
Ni machache yanayojulikana kuhusu Callixte Sankara, mtu aliyejitangaza kama naibu kamanda na msemaji wa kundi jipya la waasi la Rwanda Movement for Democratic Change.

Meja Callixte Sankara, kama avyojitambulisha kwa vyombo vya habari, ni mwanajeshi aliyekuwa mshirika wa karibu wa rais Paul kagame kwenye kundi la Rwanda Patriotic Front (RPF) katika harakati za kupigania ukombozi.

Alikuwa askari mwenye cheo cha chini baada ya RPF kushinda vita vya msituni na kuchukuwa hatamu za uongozi kufuatia baada ya kifo cha rais Juvenal Hybiamamana kwenye shambulzi la ndege.

Haijulikani kwanini Meja Sankara alikosana na utawala wa kagame, lakini alifungwa jela na mahakama ya kijeshi kwa kipindi kisichojulikana kutokana na kile kilichotajwa kama utovu wa nidhamu.

_102575724_5ea83c16-a315-444b-a6a1-43fd473ed4e8.jpg

Image captionMRCD linadaiwa kuwa ngome yake kwenye msitu wa Nyungwe
Baadaye alitoroka nchi na kukilmbilia taifa jirani la Tanzania alikotiwa mbaroni.

Juhudi za utawala wa Kigali wa kutumia waranti bandia za kutaka Dar es salam kumrudisha Meja Sankara Rwanda, ziligonga mwamba na hatimaye serikali ya Tanzania ilimwachilia mhuru na kumwezesha kusafiri uhamishoni Ufaransa.

Callixte Sankara badaye alijiunga na chama cha Rwanda National Congress (RNC) kilichioanzishwa mwaka wa 2010 na waliokuwa washirika wanne wa karibu wa rais Kagame, miongoni mwao mkuu wa zamani wa jeshi Jenerali Kayumba Nyamwasa.

Baada ya miaka kadha, ubishi ulizuka ndani ya chama cha RNC na kusababisha Meja Sankara na Jenerali Kayumba Nyamwasa kutafautiana.

Meja Callixte Sanaka alisomea uanasheria katika chuo kikuu cha Rwanda.Anatoka kabila la Tutsi na ni mjombake kiongozi wa upinzani aliyekizuizini nchini Rwanda Diane Rwigara.

Wakati huo huo kumekuwa na taarifa kuhusu ukosefu wa usalama katika baadhi ya maeneo ndani kwenyewe nchini Rwanda.

Mashambulizi ya kutumia guruneti yameshuhudiwa katika kipindi cha miaka mitano iliyopita. Maeneo ya makumbusho ya mauaji ya halaiki, masoko, vituo vya mabasi na mateksi vimekuwa vikilengwa mjini Kigali na eneo la Ruhengeri. Shambulizi la hivi majuzi la gurunedi lilitokea Juni 2017 kwenye wilaya ya Rusizi ambapo mtu mmoja aliuawa.
Habari hio inasema shambulio la mwisho la gruneti lilifanyika Juni 2017 huko Rwanda(soma mstari wa mwisho wa hii habari) sa iweje sasa wawe wanapambana sasa hivi na wasiseme shambulio la mwisho lilikua jana/leo,hahah it's weird.

By the way kama huyo wa kwny picha ndio muasi na hayo ma miwani yake kama ya kina Wema Sepetu hahah kazi anayo aisee.
 
Naomba sana kwa God hii habari iwe kweli na Nkuruzinza na hao wafaransa wawasapoti hao waasi kumpiga huyu kagame kipigo cha mbwa koko wamtoe madarakani ili iwe fundisho kwa best ake Jiwe na marais dhalimu wote wa Africa wanaowanyanyasa wananchi wao kisa wana madaraka I hate Dictatorship

We mburula ungenyanyaswa ungekuwa hapa unabwabwaja. Unadhani vita vitamu. Mmekuwa wajinga mpka hampini mnachongea. Wewe hapo nini umenyanyaswa. Ninj umekatazwa kufanya cha manufaa yako. Kuuza unga. Pumbavu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom