Maoni ya Mnyika dhidi ya hotuba ya rais ya mwezi Juni


Zomba (-a+e) = Zombe ni wale wale waliofunikwa kwa ghubighubi la kijani na njano. Ukipenda chongo huita kengeza. Mtabaki na chongo mkijua mna kengeza.
 
True wananchi watataka kusikia hoja lakini si mradi hoja tu. Hapa watu sana sana kwa sasa hawataki tena kusikia maneno ya kisiasa watu wanataka kusikia huu mgomo unaisha vipi hili wapate matibabu yao serikali iliyowahidi itayadhamini.

Huo mgomo wa madaktari na vitendea kazi aikuwa malalamiko ya wananchi wanaopokea hizo huduma in the first place ni matakwa ya madokta. Wananchi kwa ujumla hapa hatasidhani wanaelewa ni vitu gani hasa vinavyohitajika ukitoa vitanda ambavyo wao wanajua havipo. Mpaka mwananchi aone kweli madaktari wanakesi inabidi um-convince aelewe ni nini hasa. Sasa basi ukikutana na jamaa ambae kazi yake ni propanganda ujue anaweza kukuamishia mpira maana kuna na madai ya kimaslahi makubwa tena. Kumbuka wengi katika jamii hawapati wala hata hawadhani kama watakuja lipwa hayo madai ya mishahara ya madokta.

Unless unakuja na kauli za kusema tungeweza hili kwa kufanya abc ndio unaweza kuingilia kati lakini we inakupa kuingilia kati kwa kupiga porojo tu. Si mwingine anaweza tumia maneno yako kuwambia wananchi unachochea wao kutopata matibabu. Narudi


 


Kuhusu lugha humu ndani ya mtandao huu ni tatizo kubwa. Tunashangaa sana wanavyojiita great thinkers.

Aidha kuhusu Mnyika,Bwana mdogo huyu alaisha poteza mvuto wake pale Dodoma wakati anachangia pale bungeni.
Amekuwa ni mtu wa kuheshimika sana kabla katika upande wa upizani kutokana na maneno yake yaliyopimwa vizuri
yakapimika. Lakini kwa sasa yeye na tundu Lissu hawana tofauti ndani ya CHAMA CHA DEMOKRASIA YA MATUSI.
 
N .
Kweli wewe Zomba hasa. Hujasikia Mnyika alishaandika barua kwa spika kutaja hoja ya madaktari ijadiliwe bungeni? au wewe ndio wale weny kuangalia wasione, kusikia wasielewe na wanapapasa wasiitambue? pili hoja hapa ni kujadili hotuba ya rais sasa ulitaka ajadili ya kichwa chake tena? wewe vipi? au ndiyo uliyetumwa kumpiga Dk nini? Mmeishiwa nyie akili za kuku. Ndogo Mnyika yule mbele maili 300m mbele ya kilaza jk
 
Unajua mapenzi yakizidi yanaaharibu?

Zanta,

You got me wrong.

Hapa hatuzungumziii mapenzi ya chumbani baali tunazungumzia siasa na mstakabali wa nchi yetu Tanzania. Kama wewe una mapenzi kwa Rais wako Kiwete is up to you. Mimi nimesoma speech ya Kiwete na nimesoma maoni ya Mnyika na kuyapima who is talking what.

Nakumbuka story moja kule Kenya miaka ya 90s. Kwamba Rais Moi kwa wakti ule alifanya ziara nchini USA akifuatana na viongozi waandamizi akiwemo Foreign Minister Marehemu Robert Ouko. Katika ziara hiyo ujumbe wa Moi ulifanya Press conference na kukawa na maswali toka kwa wanahabari. Kila swali likulizwa Moi alikuwa anajibu kwa kubabaisha na hivyo Foreign Minister Robert Ouko akawa anamsaidia Rais wake kujibu maswali mengi.

Baada ya press conference media zikaweka hadharani kwamba kwa namna Ouko alivyokuwa akijibu maswali NDIYE ALIPASWA AWE RAIS WA KENYA. Habari hizo zilitibua hali ya hewa ndani ya msafara wa Rais na wakti wa kurudi Ouko ilibidi aachwe nyuma na apande ndege ya peke yake! Alipofika airport alipokelewa na kiongozi mmoja aliyekuwa close na Moi Bwana Nicholous Biwott na aliposhuka tu kwenye ndege Biwott alimsalimia Ouko kwa dhihaka,''Good morning Mr. President.''

Hapo ndipo lilianza sekeseke la uhasama kati ya Moi na Ouko na hatimaye kuuawa kwa Robert Ouko na mwili wake kuchomwa moto!

Ninachotaka kusema ni kwamba hapa MNYIKA AMEONGEA NA KUONYESHA UMAKINI WA HALI YA JUU KIASI CHA KUWEZA KUWASHAWISHI WATU KUWA HUYU JAMAA NDIYE ALITAKIWA KUWA RAIS WA TANZANIA NA SIYO KIWETE!
 
Ninachotaka kusema ni kwamba hapa MNYIKA AMEONGEA NA KUONYESHA UMAKINI WA HALI YA JUU KIASI CHA KUWEZA KUWASHAWISHI WATU KUWA HUYU JAMAA NDIYE ALITAKIWA KUWA RAIS WA TANZANIA NA SIYO KIWETE!
Kwa mawazo yako lakini usitake kulazimisha kua kaongea kwa umakini wakati sie wengine tuanona hakuna jipya hapo alilosema
 
Umesomeka Kamanda Mnyika!

Niliisha wahi andika thread humu ndani kuhusu udhaifu wa mnyika nawashangaa humu jf members kumshadadia huyu dogo, jimboni ameshindwa na humu jf muda si mrefu atashindwa, dogo Yuko kisifa na kutafuta umaarufu zaidi
 
Kwa mawazo yako lakini usitake kulazimisha kua kaongea kwa umakini wakati sie wengine tuanona hakuna jipya hapo alilosema

Kama mapenzi yako yote yako kwa Magambas huwezi kuona jipya hata siku moja! Ndiyo maana hata CCM wakiongea pumba mijibunge na mifuasi ya magamba inashangilia tu.

Siku upinzani ukichukua madaraka ndipo utaona jipya linakuwaje.
 
Kama mapenzi yako yote yako kwa Magambas huwezi kuona jipya hata siku moja! Ndiyo maana hata CCM wakiongea pumba mijibunge na mifuasi ya magamba inashangilia tu.

Siku upinzani ukichukua madaraka ndipo utaona jipya linakuwaje.
Shida yaka ndio hii mtu asipokubaliana na hoja mnaleta ushabiki wa siasa. kwa mtazamo huu hamtafika kwa kweli. We ushaniona hapa nashabikia chama?
 
Mnyika naona unapimana ubavu na prezidenti wako....una mengi ya kufanya zaidi ya hicho unachong'ang'ana nacho, busara Fanya kazi zako za kibunge zaidi kwani 2015 haipo mbali na jimboni kuna mambo kibao hujayafanya. Mwenzako Jk ANAONDOKA zake Hvyo hana kugombea tena.
 
 
Na Lingine kama kweli serikali haina hela kwanini isitangaze kupunguza mishara na malupulupu yote kwa asilimia hata ishirini tu kwa viongozi wote hasa wa kisiasa? kama yupo anayelipwa sh 18 miliion kwanini ishindikane kwa madaktari? Hata katika familia kama baba unalia hali kwamba hela hamna na ukashiriki kula kiporo asubuhi na kula dona kwa Maharage, watoto watakuelewa tu. Lakini kama unawambia watoto hela hamna na unarudi usiku umelewa baada ya kula sijui wapi huko watoto hawatakulewa. Au watoto wanadai daftari za kwendea shule unasema hela hamna lakini unazidi kushona suti tu hutaeleweka hata kidogo. Kwa hiyo kama serikali kweli inaamnini haina hela(siamini) ya kuwalipa madaktari na walimu haki zao itangaze wote wenye mishahara zaidi ya 3.5m wapunguzwe!
 
JK anasema amepandisha posho mpaka 25,000 kwa madaktari bingwa na 15,000 kwa madaktari wanaojifunza kwa vitendo mbona hajasema huko serikalini wanalipana posho kiasi gani kwa maafisa wao wakati wa kuandaa bajeti, safari, vikao, semina na makongamano?? anaejua wanavyolipana posho atuwekee hapa tulinganishe tafadhali.
 




Kwa ujula maoni ya mh. Mnyika kuhusiana na hotuba ya Raisi yana mambo mazuri yanayopaswa kuzingatiwa. Mwishoni mwa maoni yake anawasihi madaktari kurudi kazini na kutoa changamoto kwa serikali kutafuta suluhu ya kudumu ya matatizo yao ili kuepusha vifo vya wananchi. Katika sehemu nyingine ya maoni yake anatoa changamoto kwa chama cha madaktari kuweka wazi kwa wananchi wako tayari kupokei kipi kidogo kuliko walichoomba ili kama kanuni za usuluhishi patanishi zitafuatwa aliyepata apate nusu na kukosa nusu na kinyume chake. Amefafanua zaidi kwamba kama madaktari hawatakuwa tayari kupata nusu na kupoteza nusu watakuwa wanaweka maslahi yao kama ndio sharti la suluhu.

Kwamba Serikali haikupaswa kupeleka suala mahakamani kabla kamati ya Bunge haijatoa taarifa au ushauri wake kuhusiana na mgogoro yangeweza kuwa maoni muafaka kama madaktari wangekuwa tayari kukaa kimya kusubiri maoni au ushauri wa kamati ya Bunge. Bahati mbaya madaktari wetu wamekuwa na haraka sana kuhakikisha madai yao yanatekelezwa mara moja. Ndio maana walilazimisha kuwepo mgomo wenye athari kubwa katika maisha ya watu bila kujali kuwepo amri ya Mahakama Kuu ya kusitisha mgomo. Kwa utaratibu wa sheria zetu, panapokuwepo na mgogoro wa kisheria kati ya pande mbili mwenye dhamana na mamlaka kisheria ya kusuluhisha mgogoro huo ni Mahakama. Bunge halijapewa madaraka ya kutatua migogoro ya kisheria kati ya pande mbili. Lina mamlaka tu kama ulivyosema kwa usahihi mheshimiwa ya kuisimamia Serikali yenyewe lakini sio watumishi wa Serikali, kama madaktari. Chombo pekee chenye mamlaka juu ya Serikali na Bunge pamoja na watumishi wa umma kuhusiana na utatuzi wa migogoro niMahakama.


Kwamba mgogoro ulipaswa kupelekwa katika chombo cha usuluhishi ndivyo ilivyokuwa maana mgogoro ulikuwa mikononi mwa Kamati ya Usuluhishi na Uamuzi na iliposhindikana ilipelekwa Mahakama Kuu.
Suala la kuundwa kwa Tume huru kuchunguza mateso aliyofanyiwa daktari Ulimboka badala ya polisi ambao ni watuhumiwa linaweza kuwa na msingi kama polisi nao ni watuhumiwa.
 
Dingiswayo alifanya kazi nzuri sana jana. Jk anahutubia, huku mi nasoma kwenye mtandao Jf.
Sijui nani anamtengenezea hotuba feki namna ile, inawezekana ndiye anayempeleka Jk na ccm yake kwenye friji then kwenye coffin.
 
Last edited by a moderator:

Mfano tu Wabunge! Mbunge kama Maji Marefu elimu yake darasa la nne anapokea posho 200,000 kwa siku!
 
Upinzani ktk siasa si kupinga kila kitakachotolewa na wengine,sina hakika kama mambo yote yanaweza kuwa mabaya siku zote...hivi ni wazi kuwa kila litakalotamkwa na serikali au chama tawala kina walakini??na hivi ni sahihi kuamini kuwa kila kitakachosemmwa na mtu wa upinzani hasa wa CDM ndiyo sahihi??nani kasema kuwa CDM ndio framework sahihi ndani ya nchi hii??
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…