Maoni ya Fundi Samico kuhusu ukamataji wa makahaba kiufundi; Tujifunze pamoja

Samico Tanzania

JF-Expert Member
Feb 6, 2022
276
792
Heshima kwenu ndugu zangu!

Nashawishika kuandika maoni haya Leo nikitambulika kama fundi Samico, Fundi bora kabisa wa umeme na ujenzi kwa bei nafuu kwa watu wote na taasisi!

Wateja wangu ni wengi wakiwemo hata makahaba wenyewe! Napatikana kwa simu 0711756341 au Instagram tafuta @Samico_Tanzania
Maoni yangu kuhusu ukamataji makahaba

Kuna msemo unaosemwa kwamba "Ukifeli kutambua aina vita, hata ukipigana utashindwa tu!
Vita ya ukahaba siyo ya kimwili, pamoja na kwamba ukahaba unafanyika katika mwili lakini chanzo chake ni rohoni.

Kuna mtu anauliza fundi unasema kitugani!!!
Nasema hivi, Ukahaba hauzuiliki kwa bunduki, Ukahaba hauzuiliki kwa fimbo, ukahaba hauzuiliki kwa kifungo na vitisho!

Mtu au taasisi yoyote inayoanzisha vita kwa mbinu za kijeshi huwa tayali imefeli kabla ya vita kuanza!
Mafunzo ya kijeshi hayana kipengele hata kimoja cha kumkamata kahaba!

Kahaba walikuwapo tangu enzi za mitume, hakuna hata sehemu moja inayonesha kwamba majeshi ya wafalme waliwahi kufanikisha vita kwa kutumia migambo au polisi!

Zaidi tunajifunza hadi Leo wapelelezi walifanikiwa kujificha kwenye kivuli cha kahaba kuweza kupeleleza!

Kwa maana nyingine kahaba anaweza Fanya au kusaidia kazi ya kijeshi na ikafanikiwa!

Namna bora ya kutokomeza ukahaba ni kama hivi

Mbinu pekee ya kuondoa ukahaba mjini zipo mbili tu

1. Mbinu ya kwanza ni kukamata wateja (Kuondoa wateja)
Mbinu hii haiwezi kufanikiwa kwasababu hatujui mteja ni nani hivyo HAIFAI KUTUMIKA

2. Mbinu ya pili ya kuondoa ukahaba ni ELIMU TAMBUZI, yaani kwanza kabisa ni kuwatambua kwamba wapo;
Baada ya kuwatambua pia nikutambua wanachokifanya ndicho wanachoamini kinawalisha!

Hivyo ukishatambua hilo ndipo unatakiwa kuwasajili ikibidi ili iwe rahisi kuwapata!

Mfano mimi Fundi Samico ningekuwa kiongozi, Ningaliwasajili makahaba wote bure, namna ya kuwapata ni kuwafuata walipo nikiwa katika muonekano wa kufanana nao! (Hakuna kamera wala magwanda ya kutisha)

Baada ya kusajili madada poa wote, ningechagua wawe na uongozi wao wakuleta malalamiko!
Baada ya hapo Waziri wa Ustawi wa jamii angeunda kikosi kazi cha wataalam wakiwemo wanasaikolojia na wachungaji wa kike!

Yaani tunatafta wachungaji sampuli kama ya Zumaridi wanajipodoa kama makahaba, wapaka wanja hadi kisogoni, wanavaa vimini matata then wanatinga na waziri wetu akiwa kavaa kimini na kitop!

Wanawafuata huko na kuongea nao!
Kila kahaba anazo sababu za kuwa kahaba, wengine wametelekezwa, wengine wametengwa na ukoo, wengine wanaamini ndiyo fasheni, wengine walipokelewa mjini wakaambiwa kazi ni hiyo,...yaani mtasikia sababu nyingi sana!

Sasa mtawachambua kulingana na matatizo yao, wale wenye pepo LA ngono wachungaji watawabadilisha kwa toba, wale wenye matatizo ya Afya akili mtawakomboa kwa wataalam mtakakuwa nao!

Na mtakapowasajili mtajua wanakufa wangapi na mshiriki mazishi yao mpate kuwapata Elimu hukohuko msibani!

Mkikosa yote hayo kama serikali basi watozeni kodi ili kuwapunguza ingawa lengo nikuwapunguza!

Ile mbinu ya kutumia mabunduki haiwezi kufanikiwa kwasababu ukahaba ni roho wa ngoni na bunduki ina roho wa uharibifu!

Hivyo ukikutanisha bunduki na ukahaba usishangae kabisa mauaji kutokea!

Kwa kazi kiufundi na ushauri wa kiufundi tafadhali usisite kuwasiliana nami fundi Samico kwa simu 0711756341 insta @ Samico_Tanzania
Nina mafundi wasaidizi wangu wawili, ambao walikuwa makahaba wakaacha kabisa! Sasa ni kazi kazi hata uje na prado wanakukataa wanataka kazi ukitaka kuwaona leta kazi tufanye!

"Ambaye hajawahi kufanya dhambi awe wa kwanza kumpiga jiwe kahaba"

Kahaba anatumia alichonacho kuharibu wengine kama fisadi anavyotumia madaraka kuangamiza taifa!
 
Kwanini mtu akomae na makahaba wakati shule haina madarasa kilimanjaro huko...
Shule za kata madogo wanavuta bangi tu, hawajui kuandika kimalkia lakn mtu bado anachagua makahaba.
Nauli zinapanda, umeme mgao, matibabu bei juu...makahaba wa nn?
 
Hapa Sinza polisi juzi wameingia bar kusaka makahaba na mitutu ya bunduki , wameua mlinzi (bodigadi) kwa kumpiga risasi katika harakati za kusaka makahaba kama majambazi!

Nimesoma hoja yako fundi umeeleweka, nahisi hukupaswa kuwa fundi tu una kitu utafika mbali!
 
Hapa Sinza polisi juzi wameingia bar kusaka makahaba na mitutu ya bunduki , wameua mlinzi (bodigadi) kwa kumpiga risasi katika harakati za kusaka makahaba kama majambazi!

Nimesoma hoja yako fundi umeeleweka, nahisi hukupaswa kuwa fundi tu una kitu utafika mbali!

Duh hii ishu ni serious hivyo!?

Kweli mjini kuna mengi. Ambao hawatoki usiku ni ngumu kujua haya yanayotokea huko barabarani.
 
Misplaced priorities. Kuna vitu kwenye jamii haviwezi kutokomezwa njia bora ya ku kuvishughulikia ni kuviwekea utaratibu maalumu (regulate). Binafsi napendekeza dadapoa wangewekewa utaratibu maalumu wa kufanya biashara zao ikiwezekana hata kuwepo na maeneo maalumu (Red light streets).
Utawaondoa kwenye ma bar leo ila mitandaoni wamejaa hapo unakua ume fanikiwa kwenye nini??, uongozi wote wa mkoa umekaa chini ukaona tatizo kuu la dar ni dada poa??? What a waste of time??, hapo ukiita hao viongozi wapumbavu watasema huna nidhamu. Aibu tupu.

Wengi wa hao wanaojifanya kutaka kutokomeza biashara hii ni wateja wazuri tu wa dadapoa/slayqueens tunakutana nao mara kadhaa kwenye machimbo.
 
1. Mbinu ya kwanza ni kukamata wateja (Kuondoa wateja)
Mbinu hii haiwezi kufanikiwa kwasababu hatujui mteja ni nani hivyo HAIFAI KUTUMIKA

2. Mbinu ya pili ya kuondoa ukahaba ni ELIMU TAMBUZI, yaani kwanza kabisa ni kuwatambua kwamba wapo;
Baada ya kuwatambua pia nikutambua wanachokifanya ndicho wanachoamini kinawalisha!
Ushafeli mpaka hapa, hivi unajua nini kinachowapelekea kufanya ukahaba? Chanzo na kiini unakijua?
 
Heshima kwenu ndugu zangu!

Nashawishika kuandika maoni haya Leo nikitambulika kama fundi Samico, Fundi bora kabisa wa umeme na ujenzi kwa bei nafuu kwa watu wote na taasisi!

Wateja wangu ni wengi wakiwemo hata makahaba wenyewe! Napatikana kwa simu 0711756341 au Instagram tafuta @Samico_Tanzania
Maoni yangu kuhusu ukamataji makahaba

Kuna msemo unaosemwa kwamba "Ukifeli kutambua aina vita, hata ukipigana utashindwa tu!
Vita ya ukahaba siyo ya kimwili, pamoja na kwamba ukahaba unafanyika katika mwili lakini chanzo chake ni rohoni.

Kuna mtu anauliza fundi unasema kitugani!!!
Nasema hivi, Ukahaba hauzuiliki kwa bunduki, Ukahaba hauzuiliki kwa fimbo, ukahaba hauzuiliki kwa kifungo na vitisho!

Mtu au taasisi yoyote inayoanzisha vita kwa mbinu za kijeshi huwa tayali imefeli kabla ya vita kuanza!
Mafunzo ya kijeshi hayana kipengele hata kimoja cha kumkamata kahaba!

Kahaba walikuwapo tangu enzi za mitume, hakuna hata sehemu moja inayonesha kwamba majeshi ya wafalme waliwahi kufanikisha vita kwa kutumia migambo au polisi!

Zaidi tunajifunza hadi Leo wapelelezi walifanikiwa kujificha kwenye kivuli cha kahaba kuweza kupeleleza!

Kwa maana nyingine kahaba anaweza Fanya au kusaidia kazi ya kijeshi na ikafanikiwa!

Namna bora ya kutokomeza ukahaba ni kama hivi

Mbinu pekee ya kuondoa ukahaba mjini zipo mbili tu

1. Mbinu ya kwanza ni kukamata wateja (Kuondoa wateja)
Mbinu hii haiwezi kufanikiwa kwasababu hatujui mteja ni nani hivyo HAIFAI KUTUMIKA

2. Mbinu ya pili ya kuondoa ukahaba ni ELIMU TAMBUZI, yaani kwanza kabisa ni kuwatambua kwamba wapo;
Baada ya kuwatambua pia nikutambua wanachokifanya ndicho wanachoamini kinawalisha!

Hivyo ukishatambua hilo ndipo unatakiwa kuwasajili ikibidi ili iwe rahisi kuwapata!

Mfano mimi Fundi Samico ningekuwa kiongozi, Ningaliwasajili makahaba wote bure, namna ya kuwapata ni kuwafuata walipo nikiwa katika muonekano wa kufanana nao! (Hakuna kamera wala magwanda ya kutisha)

Baada ya kusajili madada poa wote, ningechagua wawe na uongozi wao wakuleta malalamiko!
Baada ya hapo Waziri wa Ustawi wa jamii angeunda kikosi kazi cha wataalam wakiwemo wanasaikolojia na wachungaji wa kike!

Yaani tunatafta wachungaji sampuli kama ya Zumaridi wanajipodoa kama makahaba, wapaka wanja hadi kisogoni, wanavaa vimini matata then wanatinga na waziri wetu akiwa kavaa kimini na kitop!

Wanawafuata huko na kuongea nao!
Kila kahaba anazo sababu za kuwa kahaba, wengine wametelekezwa, wengine wametengwa na ukoo, wengine wanaamini ndiyo fasheni, wengine walipokelewa mjini wakaambiwa kazi ni hiyo,...yaani mtasikia sababu nyingi sana!

Sasa mtawachambua kulingana na matatizo yao, wale wenye pepo LA ngono wachungaji watawabadilisha kwa toba, wale wenye matatizo ya Afya akili mtawakomboa kwa wataalam mtakakuwa nao!

Na mtakapowasajili mtajua wanakufa wangapi na mshiriki mazishi yao mpate kuwapata Elimu hukohuko msibani!

Mkikosa yote hayo kama serikali basi watozeni kodi ili kuwapunguza ingawa lengo nikuwapunguza!

Ile mbinu ya kutumia mabunduki haiwezi kufanikiwa kwasababu ukahaba ni roho wa ngoni na bunduki ina roho wa uharibifu!

Hivyo ukikutanisha bunduki na ukahaba usishangae kabisa mauaji kutokea!

Kwa kazi kiufundi na ushauri wa kiufundi tafadhali usisite kuwasiliana nami fundi Samico kwa simu 0711756341 insta @ Samico_Tanzania
Nina mafundi wasaidizi wangu wawili, ambao walikuwa makahaba wakaacha kabisa! Sasa ni kazi kazi hata uje na prado wanakukataa wanataka kazi ukitaka kuwaona leta kazi tufanye!

"Ambaye hajawahi kufanya dhambi awe wa kwanza kumpiga jiwe kahaba"

Kahaba anatumia alichonacho kuharibu wengine kama fisadi anavyotumia madaraka kuangamiza taifa!
wana ukimwi hao, washaua masela wengi
 
Back
Top Bottom