mtana76
JF-Expert Member
- May 31, 2015
- 517
- 438
Maneno yako yanaweza kuwa na mbolea kiasi, lakini kama wangekuwa wema hivyo tusingesikia watu /wafanyakazi wao wakawalalamikia. Mfano mdogo tu ni huu wa karibuni wa madreva na waajiri wao! Sikiliza wanavyohadithia kunyanyaswa kwao na matajiri wao. Tajiri anachojali yeye ni kutengeneza faida kubwa sana kwa kumyonya mtumishi wake ambaye ni maskini. Hapa ndiyo maana Mwl. Nyerere aliwaambia watanzania kuwa UBEPARI NI UNYAMA kama unakumbua!
Sometimes: Ndugu yangu ndio maanaa Sera za Chadema na Ukawa kipaumbele cha kwanza Elimu,Cha pili Elimu na cha Tatu Elimu.Hivi vitu kwa mwanadamu kulalamika avikuanza leo toke kuumbwa kwa ulimwengu mwanadamu si mtu wa kuridhika.hata umpatie nini mwanadamu aridhiki.hilo linaeleweka..turudi kwenye point.tunaposema Elimu sio tuu itolewe elimu ya Sayansi na kadhalika..ni elimu ya nyanja zote..mpaka elimu ya uelewa wa Haki zetu.usipojua haki zako za msingi hata uwe Prof..wewe utakuwa bure tuu.Sisi watanzania elimu ndio inatusumbua ..matokeo yake tunaanza kuwachukia watu wenye kipato tunawaona sio binadamu wanaoweza kutujali sisi maskini,,sio kweli maana mchango mkubwa wa kumuokoa maskini katika dunia hii unadhaminiwa na Matajiri.watu wenye pesa.,hilo lipo wazi,,unaposema unyanyasaji wa wafanyakazi .ndio Sawa hupo huo unyanyasaji .lakini tukirudi pale pale Elimu itamapokuwa nzuri watu wakajitambua wakatambua haki zao.huo unyanyaswaji utaisha,maana utawekwa mfumo mzuri kwa sisi kabla ya kupata kazi utapatiwa mkataba utausoma vizuri mkataba usiporidhika nao basi,ukiridhika utasaini kwa makubaliano na sheria na haki zako zote zitafuatwa kutokana na ajira hiyo.hilo litakapokuwepo Nchi utoona unyanyasaji Wa tajiri kwa maskini ,viwandani au kwenye sekta yoyote hile.Nafikiri ndugu yangu inaweza kuwa umewahi kutembea zaidi nchi zilizoendelea ,utakuta mtu anaweza kuwa na vitu vya thamani kuliko boss wake aliyemwajiri,,lkn kwa Tanzania aiwezekani utaambiwa tuu wewe ni mwizi boss wako anaendesha baiskeli wewe unaendesha gari..tuache fikra hizo..za matabaka .ukiwa mbinafsi ni mbinafsi tuu atojalisha wewe Maskini au Tajiri..Nyerere ni binadamu kama mimi na wewe..ana nyongo sio malaika.hivyo basi sio alichokifanya au kusema basi yupo sahihi..watu wanaamka sasa hivi..atuwezi kuinua hii Nchi kama tutamfikiria Nyerere,watu tunaenda mbele Future.hili tuweze kwenda na Dunia ya sasa nyinyi mnaturudisha miaka 50 ya ujamaa,,Mataifa yote ya sera za ujamaa sasa hivi Chali.Chagua Lowasa na Ukawa ujue haki zako na uwezi kuzihoji ukizikosa ,,Umeme unakatwa katwa hovyo,hospital hovyo unashindwa kuhoji maana haki zetu atuzijui kwa sababu elimu mbovu.Serikali ni wajibu wake kutoa huduma muhimu kwa raia wake.Maji,barabara,umeme,elimu,usalama wa raia na mali zao,huduma ya afya,na mengine.Hila pia serikali sio wajibu wake kumfanya mtu awe tajiri.,ukipata huduma hizo.hapo juu utokuwa na sababu ya kumuangalia tajiri kwa jicho baya..utajiri ni nguvu binafsi..Siku njema ndugu yangu.