MAONI:. Ndoa ,,, Waislam vs Wakristo

MAONI:. Ndoa ,,, Waislam vs Wakristo

Status
Not open for further replies.
FaizaFoxy:Nakubaliana na wewe kwa 100% kua kwa muislam hiyo si ndoa ni zinaa,Ila kwa mkristo hiyo ni ndoa halali na ina baraka na wataishi vizuri tu.Na pia mwanamke wa kikristo akibadili dini aolewe na muislam ni hivyo hivyo,wakristo watasema hiyo ni zinaa hakuna ndoa wakati huku kwenye Uislam ndoa hiyo ni halali na ina baraka tele na wataishi vizuri tu.Tumeshakua tofauti ni kawaida kusema kua ndoa ya upande mwingine ni ZINAA.Kinachotakiwa mtu binafsi uendeleze juhudi za kuelimisha watu kuhusu imani yako waijue na waifuate.
Hiyo ndoa ni "Najisii" hadi Qiyama....!!
 
Mi nakuelewa sana mkuu, nimeishi kwenye hizo nchi pia. Ukiusoma vizuri uislamu utaelewa kwa nini pamoja na hayo unayosema lakini M'mungu anawaamrisha kumtii kwa kadri ya uwezo wao. M'mungu mwenyewe amesema katika Qur'an kuwa binadamu ni viumbe dhaifu sana na wenye mapungufu, kwa hiyo kukosea ni kitu kinachotarajiwa ila kila unapokosea ni vyema kuomba msamaha na kutubia. Kifupi ni kwamba perfectionism kwenye uislamu ni suala la mtu kukubali ubinadamu, kumtambua M'mungu na kuomba msamaha kila anapokwenda tofauti, sio kuwa malaika.

Kitu kingine kuwa muislamu ni hiari mkuu, kama unaona yale yanayosemwa katika uislamu ni mambo ya kizamani na hayawezekani, unaweza kuacha tu huo uislamu. Kwanza sina hakika sana kama unaweza kuendelea kujiita muislamu maana ushapingana na aya ya M'mungu inayosema kuwa wanaume ni viongozi wa wanawake katika Qur'an (Bahati siikumbuki hiyo sura wala namba ya aya, ila kama ni muhimu nitaitafuta nikuwekee).

Kingine unaongelea kuhusu masuala ya elimu kama vile uislamu unakataza kumsomesha mtoto wa kike. FYI kutafuta elimu ni excuse pekee inayomruhusu mtoto wa kike kwenda kinyume na amri za mume au baba yake. Yaani kama baba/mume anasema hakuna kupata elimu, mtume amemruhusu mtoto wa kike kwenda kinyume katika hili na kuelekea katika njia ya kutafuta elimu. Sasa sijui unaongelea vitu gani hapa.

Nakukumbusha kaka angu katika imani. Hii hapa aya suratul Nisaa aya ya 34 "arijalu kawamuuna alaa nisai......" "Wanaume ni walinzi wa wanawake, kwa sababu M.mungu amewafadhilisha baadhi yao kuliko wengine, na kwa sababu ya mali zao wanazozitoa. Basi wanawake wema ni wale wenye kutii, wanaojihifadhi hata wasipokuwepo waume zao, kwa kuwa mungu amewaamrisha wajihifadhi......"
 
Mjasiria, Salaam Aleikum, Ahsante kwa maoni yako. Nimekuelewa. Swali langu ni hili: Kwa nini wewe ni Mwislamu zaidi yangu kwa kuwa unafunga na mimi sifungi? Dini ni sharia si ndio? Sasa kama wewe hufuati masharti ya dini yako, kwa nini uwaambie wengine kwamba wamepotea na warudi kwenye mwanga wakati wewe mwenyewe huwezi kufuata masharti ya dini yako. Kama nilivyosema mwanzo, hamna binadamu anayeweza kufata masharti YOTE ya dini yake. kwa hivyo kama wewe unafunga na mimi sifungi , lakini wewe hufuati sharia law Tanzania na unampeleka mkeo apewe dawa ya kuzuia mimba au kufunga kizazi basi kwa nini wewe uwe Muislamu bora zaidi wakati umeshavunja sharia ya Uislamu ya kutoingilia mambo ya Mungu? Umenipata? Katika maisha ya leo, narudia, hasa maisha ya karni hii, ni vigumu kujiita Mdini wakati huwezi kufuata sharia za dini. Hata Saudi Arabia yenyewe, watoto wa kiume wengi wanabatiliwa kwa kuwa wasichana wanafungiwa na hawana ruhusa kukutana na wanaume ambao sio ndugu zao na hamna ruhusa kutembea na mwanamme na mwanamke kama sio ndugu yako au jamaa yako. Hi ni sharia ya Kiislamu, je wewe unaishi namna hivi? Je, unapokea riba katika benki? Unatoa sadaka kamili kama inavyosema dini kila mwaka? Humtongozi mwanamke kazini au kuongea nae? Je, unakubali kukatwa mkono ukikamatwa na wizi? Kabla ya kunitenga na kuniambia mimi sio mwislamu kamili kwa kuwa sifungi, wewe pia jiangalia nafsi yako na toa jibu kamili kama wewe pia unafuata sharia ZOTE za dini yako, sio kuchambua chambua tu. Narudia, dini na maisha ya kisasa hayalingani, kama yangelingana basi tusiongetumia vidonge vya kuzuia mimba au wote tungeishi katika sharia za dini zetu ya karne ya 15. Sijui wewe, lakini mimi sitaki kuishi chini ya sharia za dini kama kanuni ya nchi kwa sababu zimepitwa na wakati wake ndio maana kuna binadamu wachache mno wanaoweza kusimama na kusema wanafuata aamri yoye ya dini zao.
Asalaam 3aleykum W W... Ndugu Mpendwa, Kila mwanaAdamu ana kasoro zake na upungufu wake katika kutii Amri za moula wetu Karimu Moula wetu rahimu Mwenye Rehema na Misamaha mingi na mwenyeEzzi Mungu ndo alokamilika.!! mimi na wewe na viumbe vyake tumekuwa tukihalifu na kutenda dhambi nyingi.... Lakini MwenyEzzi Mungu ni ------ (mvumilivu) na hutupa Time na kupokea TOBA (repent) na milango yake huweka wazi kwa yule atakae rudi au muombaji msamaha.
Ofcoz. kukosea ni ubinadamu na sote huteleza katika maisha... Lakini tumepewa chance ya kuomba MAGHAfirrah na kujirekebisha (corrections). kila mjjaa ata hesabiwa kwa yake na siyo aliyoyatenda na hatoshirikishwa na Hesabu za wengine !! Hiyo tafadhali ijue "You & me will be accounted by our deeds" hakuna nafasi ya kuExplain watu waivyo kuwa wakifanya au nchi/Maisha zilivyokuwa zikiendeshwa. " Vitabu/Amri alivyoteremsha Allah ni vile vile NO change "tangu enzi na hadi End of the Day. Siye ndiye hupindishapindisha. Kwa Heshima na taadhima kwako Rehema,Baraka (mke,watoto,Mali,Maisha yote) za Moula wako ni zako na kwa sababu yako. THE DOORS are open and thers enough space for all. ALLAH bless you and Umma.AMIN
 
Katika uislam hakuna ndoa ya muislam na asiyekuwa wa dini hiyo. Kama ni lazima aolewe ni sharti akubali tena kwa hiari yake kuwa muislam ndipo ndoa ifungwe. Tusichanganye kati ya watu wenye majina ya kiislamu who knows nothing about the morals and values of the religion, and the true muslims. Kuzaa na mkristu haimaanishi kuwa ni mkeo, huyo ni mzinzi mwenzio na huyo mtoto katika dini hatambuliki.
HUU NDIO UKWELI

Na kinyume chake ni sahihi, hata sisi wakristo hasa Roma mzazi akimuozesha mwanae kwa Muislam (Kwa kuchukua mahari) anafungiwa
 
Aleikum Salaam Ndugu Life is Short. Nimependezewa na jibu lako sana. Sisi binadamu WOTE tuna kasoro na wote tuna dhambi. Lakini mimi naambiwa kuwa sio Mwislamu kamili kwa kuwa sifungi, hio ndio ilikuwa point yangu na wewe umeshanijibu kuwa hamna binadamu asiye an kasoro. pale ambapo atatokea binadamu asiye na kasoro ndio nitaweza kuitwa na Waislamu wenzangu kuwa nipo gizani au Mwislamu wa jina na kadhalika. Nyosha mkono kama unafuata sharia ZOTE za dini yako halafu una ruhusa ya kuniita chochote upendacho. Usifanye masihara na Sharia Law!
 
Mjasiria, Salaam Aleikum, Ahsante kwa maoni yako. Nimekuelewa. Swali langu ni hili: Kwa nini wewe ni Mwislamu zaidi yangu kwa kuwa unafunga na mimi sifungi? Dini ni sharia si ndio? Sasa kama wewe hufuati masharti ya dini yako, kwa nini uwaambie wengine kwamba wamepotea na warudi kwenye mwanga wakati wewe mwenyewe huwezi kufuata masharti ya dini yako. Kama nilivyosema mwanzo, hamna binadamu anayeweza kufata masharti YOTE ya dini yake. kwa hivyo kama wewe unafunga na mimi sifungi , lakini wewe hufuati sharia law Tanzania na unampeleka mkeo apewe dawa ya kuzuia mimba au kufunga kizazi basi kwa nini wewe uwe Muislamu bora zaidi wakati umeshavunja sharia ya Uislamu ya kutoingilia mambo ya Mungu? Umenipata? Katika maisha ya leo, narudia, hasa maisha ya karni hii, ni vigumu kujiita Mdini wakati huwezi kufuata sharia za dini. Hata Saudi Arabia yenyewe, watoto wa kiume wengi wanabatiliwa kwa kuwa wasichana wanafungiwa na hawana ruhusa kukutana na wanaume ambao sio ndugu zao na hamna ruhusa kutembea na mwanamme na mwanamke kama sio ndugu yako au jamaa yako. Hi ni sharia ya Kiislamu, je wewe unaishi namna hivi? Je, unapokea riba katika benki? Unatoa sadaka kamili kama inavyosema dini kila mwaka? Humtongozi mwanamke kazini au kuongea nae? Je, unakubali kukatwa mkono ukikamatwa na wizi? Kabla ya kunitenga na kuniambia mimi sio mwislamu kamili kwa kuwa sifungi, wewe pia jiangalia nafsi yako na toa jibu kamili kama wewe pia unafuata sharia ZOTE za dini yako, sio kuchambua chambua tu. Narudia, dini na maisha ya kisasa hayalingani, kama yangelingana basi tusiongetumia vidonge vya kuzuia mimba au wote tungeishi katika sharia za dini zetu ya karne ya 15. Sijui wewe, lakini mimi sitaki kuishi chini ya sharia za dini kama kanuni ya nchi kwa sababu zimepitwa na wakati wake ndio maana kuna binadamu wachache mno wanaoweza kusimama na kusema wanafuata aamri yoye ya dini zao.

Waalaykum msalaam. Kwanza mkuu mimi sijasema kuwa mimi ni muislamu kuliko wewe. Nilichosema mimi ni kuwa, kwa wewe kutangaza hadharani kuwa hujafunga kwa miaka 10 kwa kuwa tu umeamua hivyo (Kumbuka hukutoa sababu yeyote ya msingi). Zaidi ya hapo ukaongeza kuwa huna mpango wa kufunga kabisa, hapa kwa mujibu wa taratibu na sheria za kiislamu sidhani (makusudi kabisa nimetumia neno sidhani, hata ukirudi kwenye ile posti yangu ya kwanza ndilo neno nililotumia) kama unaweza kusimama mahali na kuusemea uislamu. Hii ni kwa sababu japokuwa uislamu una mambo mengi, lakini funga ni nguzo ya tatu ya uislamu na funga ni moja ya ibada ambayo imesisitizwa sana katika uislamu na ghadhabu anazopata M'mungu kwa mtu kuacha kufunga kwa makusudi ni kubwa mno. Hivyo basi mtu anayeacha kufunga bila sababu ana walakini sana na imani yake juu ya uislamu wake. Kumbuka kuwa si mimi nayehukumu hapa, nilichofanya mimi ni kukupa tu msimamo wa uislamu juu ya kuacha kufunga bila sababu. Unaweza ku-google hapo kwa maelezo zaidi juu ya kuacha funga. Kumbuka pia kwenye uislamu dhambi hazilingani, kwa mfano kuua si sawa na kumtukana mtu.

Halafu mkuu kuwa kwangu muislamu mbaya hakuwezi kuhalalisha wewe kuwa mbaya vilevile. Pili dini si sharia peke yake. sharia ni sehemu ya dini. Uislamu ni mfumo wa maisha wenye kila kitu. Kuhusu vijana wa Saudi, hapo kuna mkorogo wa mambo mengi na sidhani kama hapa ni mahali pake. Duniani leo kuna matatizo mengi sana ambayo kama tukianza kuyajadili hapa hatuwezi kumaliza. Nafikiri ni busara zaidi tuendelee kubaki kwenye mada husika japokuwa kwa kiasi fulani naona kama tunatoka.

Mkuu kwa nini unanisemea mambo ambayo huna uhakika nayo. Maana umeshasema nampeleka mke wangu akapewe dawa ya mimba, nakula riba wakati hata hunijui. Tufanye basi labda nafanya hayo mambo. Lakini kama umesoma vizuri pale juu nimekwambia kwamba Allah(sw) anatambua watu tunafanya makosa na ndiyo maana milango iko wazi kwa waumini kutubia na kuomba msamaha. Hicho ndicho kinachotufanya sisi binadamu. Ndiyo maana kuna hadi aya, Allah(sw) anasema, "Kama mngalikuwa ninyi binadamu hamfanyi makosa, basi ningeliwaondoa na kuwaleta wengine wanaokosea na kuomba msamaha" (Siyo tafsiri rasmi, bidodo kama unaweza tusaidie na hii tafadhali). Kwa hiyo basi naweza kuwa nafanya hayo lakini nina nafasi ya kutubu na kutaka maghfira.

Kuhusu suala la sheria za dini kupitwa na wakati, dini ni hiari na uislamu haujapitwa na wakati. Huwezi kudai wewe ni muislam halafu wakati huo huo unaukataa huo uislamu. Huu ni mkanganyiko wa aina yake, nimesema hapo kuwa unaweza kuacha uislamu kama huridhiki, ni hiari si lazima.

Mkuu binadamu hatujakamilika na tunabadilika, mimi siwezi kujiona bora kuliko yeyote. Hata kama mimi ni bora kuliko wewe sasa hivi kitu ambacho siwezi kujua wala kuwa na uhakika nacho, lakini nitajuaje kama wewe kesho utakuwa bora kuliko mimi. Allah(sw) anatuambia ni kwa rehma zake tu mtu anaweza kumtii na kufuata haki, si ujanja wetu. Na ukifikiria kwa makini, hii kitu ina maana sana, maana mtu hajichagulii anachoamini. Ni kama vile mtu anajikuta tu anaamini kitu fulani. yaani hatuna udhibiti kabisa wa imani zetu na ndio maana sisi waislamu tunatakiwa kumshukuru Allah(sw) kwa neema hii kubwa ya kuwa waislamu

Allah(sw) atuongoze sote katika nuru na njia ya haki....Amin.
 
Aleikum Salaam Ndugu Life is Short. Nimependezewa na jibu lako sana. Sisi binadamu WOTE tuna kasoro na wote tuna dhambi. Lakini mimi naambiwa kuwa sio Mwislamu kamili kwa kuwa sifungi, hio ndio ilikuwa point yangu na wewe umeshanijibu kuwa hamna binadamu asiye an kasoro. pale ambapo atatokea binadamu asiye na kasoro ndio nitaweza kuitwa na Waislamu wenzangu kuwa nipo gizani au Mwislamu wa jina na kadhalika. Nyosha mkono kama unafuata sharia ZOTE za dini yako halafu una ruhusa ya kuniita chochote upendacho. Usifanye masihara na Sharia Law!

Mkuu japokuwa uko sahihi lakini kuna vitu ambavyo vimeshakatiwa shauri katika dini. Huwezi kupinga aya ya M'mungu wazi wazi na kuita ni ujinga halafu uendelee kuwa muislamu. Na hii haina maana kuwa anayekwambia ukweli huo ni muislamu saaaaaaaaaana. Huenda hata yeye ameshakufuru ila hajui tu, lakini hilo haliondoi ukweli kuwa hata wewe umekufuru. Upo hapo mkuu??
 
Katika ukoo wetu hamna aliyeoa wala kuolewa na muislamu. Hivyo kusoma hii mada ni burudisho sana.
 
binti mkristo kuolewa namwislam ni dhambi yamauti,hujiamulia hilo wenyewe bila ridhaa ya kanisa au wazazi.uchunguzi tuloufanya-rc-unaonesha vijana wakiislam huoa wakristo kwa sababu tatu muhimu.1~binti mkristo kafundishwa kuwa ndoa niyamilele hakuna talaka hadi kifo,jambo ambalo mwislam halipati kwabinti mwislam kwakuwa kafundishwa kuwa mkishindana taraka ruksa,hivyo hukaa kimtego tu kwamume akijua wakati wowote taraka sababu hata ktk harusi inaagizwa siku ileile.2~huamini kuwa kuoa binti mkristo na kumfanyakuwa mwislamu hupata thawabu kwa molawao.3~baadhi ya mashirika yakidini toka Iran,yanatoa zawadi (pesa)kwa vijana wakiislam watakaowatia mimba,au kuoa binti zakikristo,kwakuwa mtoto atakaezaliwa atakuwa mwislam.
 
Mungu ndo huyo huyo mmoja ispokua nyie mmekufuru pale mliposema Jesus ni mwana wa Mungu na kumtukuza kiumbe wake kama Mungu. Mungu ni mmoja wala hakuna aliyefanana nae, Hakuzaa wala hakuzaliwa. Kiufupi nyie mna dini yenu na sie tuna dini yetu

uko sahihi mkuu ila usibishane na waliokufuru waeza jiingiza kwenye kufuru pasi nawewe kujua,,..cz wengi wao humu ni mashabiki tu na hawako tayari kujifunza so ni vema ukawa kimya usije haribu swaum yako bure!! rejea (surat baqarah aya ya 138)
 
Mungu ndo huyo huyo mmoja ispokua nyie mmekufuru pale mliposema Jesus ni mwana wa Mungu na kumtukuza kiumbe wake kama Mungu. Mungu ni mmoja wala hakuna aliyefanana nae, Hakuzaa wala hakuzaliwa. Kiufupi nyie mna dini yenu na sie tuna dini yetu

tumemtukuza kadirir ya uislamu au ukristo
 
Katika ukoo wetu hamna aliyeoa wala kuolewa na muislamu. Hivyo kusoma hii mada ni burudisho sana.
Oh my Dear BJ,
MaShaallah, naona unabweteka na unasikia raha.... Sawa sote tupo kwenye mgongo ardhi hii jitaarishe kesho kijana handsome religious young Muslim atafanya ziara kwenu licha ya kuoa tu, atafungua milango na madirisha mupate mwangaza atasilimisha wanyumbani wote na mutaburudika zaidi, in-ShaAllah.
kila la heri.
 
Waalaykum msalaam. Kwanza mkuu mimi sijasema kuwa mimi ni muislamu kuliko wewe. Nilichosema mimi ni kuwa, kwa wewe kutangaza hadharani kuwa hujafunga kwa miaka 10 kwa kuwa tu umeamua hivyo (Kumbuka hukutoa sababu yeyote ya msingi). Zaidi ya hapo ukaongeza kuwa huna mpango wa kufunga kabisa, hapa kwa mujibu wa taratibu na sheria za kiislamu sidhani (makusudi kabisa nimetumia neno sidhani, hata ukirudi kwenye ile posti yangu ya kwanza ndilo neno nililotumia) kama unaweza kusimama mahali na kuusemea uislamu. Hii ni kwa sababu japokuwa uislamu una mambo mengi, lakini funga ni nguzo ya tatu ya uislamu na funga ni moja ya ibada ambayo imesisitizwa sana katika uislamu na ghadhabu anazopata M'mungu kwa mtu kuacha kufunga kwa makusudi ni kubwa mno. Hivyo basi mtu anayeacha kufunga bila sababu ana walakini sana na imani yake juu ya uislamu wake. Kumbuka kuwa si mimi nayehukumu hapa, nilichofanya mimi ni kukupa tu msimamo wa uislamu juu ya kuacha kufunga bila sababu. Unaweza ku-google hapo kwa maelezo zaidi juu ya kuacha funga. Kumbuka pia kwenye uislamu dhambi hazilingani, kwa mfano kuua si sawa na kumtukana mtu.

Halafu mkuu kuwa kwangu muislamu mbaya hakuwezi kuhalalisha wewe kuwa mbaya vilevile. Pili dini si sharia peke yake. sharia ni sehemu ya dini. Uislamu ni mfumo wa maisha wenye kila kitu. Kuhusu vijana wa Saudi, hapo kuna mkorogo wa mambo mengi na sidhani kama hapa ni mahali pake. Duniani leo kuna matatizo mengi sana ambayo kama tukianza kuyajadili hapa hatuwezi kumaliza. Nafikiri ni busara zaidi tuendelee kubaki kwenye mada husika japokuwa kwa kiasi fulani naona kama tunatoka.

Mkuu kwa nini unanisemea mambo ambayo huna uhakika nayo. Maana umeshasema nampeleka mke wangu akapewe dawa ya mimba, nakula riba wakati hata hunijiu. Tufanye basi labda nafanya hayo mambo. Lakini kama umesoma vizuri pale juu nimekwambia kwamba Allah(sw) anatambua watu tunafanya makosa na ndiyo maana milango iko wazi kwa waumini kutubia na kuomba msamaha. Hicho ndicho kinachotufanya sisi binadamu. Ndiyo maana kuna hadi aya, Allah(sw) anasema, "Kama mngalikuwa ninyi binadamu hamfanyi makosa, basi ningeliwaondoa na kuwaleta wengine wanaokosea na kuomba msamaha" (Siyo tafsiri rasmi, bidodo kama unaweza tusaidie na hii tafadhali). Kwa hiyo basi naweza kuwa nafanya hayo lakini nina nafasi ya kutubu na kutaka maghfira.

Kuhusu suala la sheria za dini kupitwa na wakati, dini ni hiari na uislamu haujapitwa na wakati. Huwezi kudai wewe ni muislam halafu wakati huo huo unaukataa huo uislamu. Huu ni mkanganyiko wa aina yake, nimesema hapo kuwa unaweza kuacha uislamu kama huridhiki, ni hiari si lazima.

Mkuu binadamu hatujakamilika na tunabadilika, mimi siwezi kujiona bora kuliko yeyote. Hata kama mimi ni bora kuliko wewe sasa hivi kitu ambacho siwezi kujua wala kuwa na uhakika wake, lakini nitajuaje kama wewe kesho utakuwa bora kuliko mimi. Allah(sw) anatuambia ni kwa rehma zake tu mtu anaweza kumtii na kufuata haki, si ujanja wetu. Na ukifikiria kwa makini, hii kitu ina maana sana, maana mtu hajichagulii anachoamini. Ni kama vile mtu anajikuta tu anaamini kitu fulani. yaani hatuna udhibiti kabisa wa imani zetu na ndio maana sisi waislamu tunatakiwa kumshukuru Allah(sw) kwa neema hii kubwa ya kuwa waislamu

Allah(sw) atuongoze sote katika nuru na njia ya haki....Amin.
Mjasiria, Salaam Aleikum, Shukran kwa majibu yako. Nimekuelewa. Naomba samahani kama unafikiri nimetoa mfano mbaya kama nilitumia mfano wa mke kutumia dawa ya kuzuia mimba. Nia yangu sio ya kuvunja heshima yako wala ya mkeo (maka umeoa) ila kuonyesha kuwa sisi binadamu tuna kasoro. Mimi kama wewe, nimepita madrassa na naifahamu dini yangu na najua sharia muhimu za dini yetu. Nadhani ni muhimu kuachana hapa kwa heshima kwa kuwa hatutaonana macho kwa macho na pointi tunazozichambua. Japokuwa nina dhambi zangu naamini kuwa mimi naishi kwa kusaidia wasiojiweza, naangalia familia yangu na kuheshimu wazee wangu na marafiki zangu, natoa zakat naswali vile vile, lakini napinga kabisa kuwa kuna binadamu hapa duniani anaweza kuniambia kuwa mimi si Mwislamu bora kwa kuwa sifuati baadhi ya sharia za dini. Hapa ndio kuna utata. Kama hamna mtu anayeweza kuishi na kufuata sharia zote za dini, basi hamna mtu ana haki ya kuniambia mimi sio mwislamu kamili na kadhalika. Naomba radhi kama nimesukasirisha au kutokupa heshima unayostahili, lakini point yangu iko pale pale. Mimi naweza kuwa Muislamu kama wewe na Mola peke yake ndio anajua, hapa duniani hakuna mahakama itayonihukumu na dhambi zangu. Na wale Waislamu wanaopenda kuwasaidia wenzao kuona njia na uwanga, basi wawe tayari kunyosha mkono na kusema mbele ya Mungu wao kuwa , ndio, wao wamefata SHARIA zote za dini. Nasema baadhi ya sharia ni za kale sio kwa kutoheshimu sharia za dini ila katika maisha haya ya karne ya 21, asilimia ngapi unafikiri ya Waislamu wasiotumia madawa ya kinga ya mimba, hawapokei riba, hawanywi pombe na wanasali sala tano na kufunga? Sasa atakapovunja sharia hizo, kwa nini wao ni Waislamu zaidi kuliko mimi? Tusichambue sharia, aidha tunazifuata au hatuzifuati. Hata nchi zenye wananchi wengi wa Kiislamu wanashindwa kufuata Sharia law kama ilivyooandikwa katika Quran Tukufu, kwa sababu gani unafikiri?
 
Oh my Dear BJ,
MaShaallah, naona unabweteka na unasikia raha.... Sawa sote tupo kwenye mgongo ardhi hii jitaarishe kesho kijana handsome religious young Muslim atafanya ziara kwenu licha ya kuoa tu, atafungua milango na madirisha mupate mwangaza atasilimisha wanyumbani wote na mutaburudika zaidi, in-ShaAllah.
kila la heri.

Hii dua kiboko!
 
uko sahihi mkuu ila usibishane na waliokufuru waeza jiingiza kwenye kufuru pasi nawewe kujua,,..cz wengi wao humu ni mashabiki tu na hawako tayari kujifunza so ni vema ukawa kimya usije haribu swaum yako bure!!

ukweli nikuwa MUNGU tunayemwabudu sie wakristo tangu mwaka 33bk ilipoanza RC,siyule anaeabudiwa na waislamu tangu mwaka 570bk ulipoanza uislam,nadaima mwislam ndo hutangaza kwamba Mungu ni yuleyule ili kuficha mengi yaajabu ndani ya uislamu,mfano wawazi mwislamu anaamini kuwa peponi munguwake atampa zawadi ya mke bikra,tena maraika,wakati BIBLIA itakataa hayo na kusema mambo yakuoa na kuolewa ni yahapa duniani tu.
 
bidodo@@,,...nimesoma comments zako zote,,..hongera sana Allah azidi kukuzidishia elmu(Rabbana zidna ilma) umejitaidi kuelimisha kwa qadri Allah alivyokujalia but stil watu nafsi zetu ngumu na tumekua wagumu kukuelewa na kuanza kukufuru,,.. Ivo usiumize dole gumba lako au kuzichosha keypards zako kwa nafsi nzito zenye makongwa shingoni mwetu tumeekewa vizuizi mbele yetu..nyuma yetu n.k.(surat ya sin aya ya 10) inasema,,...:Ni Sawa Kwao Ukiwaonya Au Usiwaonye,Hawataamini::,,..ivyo tumuachie Allah afanye kazi yake,,..na kamwe usilumbane na asiekua na elmu ya Allah SW)),,...Jazaka llah kheiry,,.... @"BIDODO"@
 
Last edited by a moderator:
..na kamwe usilumbane na asiekua na elmu ya Allah SW)),,...Jazaka llah kheiry

bora umemuonya mapema asijeuona mwanga,akamjua MUNGU waukweli akafika mbinguni,bora umzuie muangamie wote jehanum.
 
Hebu nipe source ya haya maelezo yako

Kama unajua kiarabu soma kwanza biography ya mtume muhamed.
Ukitoka hapo soma quran.

Ukisha maliza soma Torah, ambacho kitabu cha mungu cha myaudi.

Ukisha toka hapo soma bibilia, ya kisasa.

Hapo utakua haudanganywi na mtu tena.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom