Econometrician
JF-Expert Member
- Oct 25, 2013
- 15,795
- 28,454
Mambo pekee niliyoyabaini katika uchaguzi huu wa kura za maoni ni kama yafuatayo:-
Ni mara 100 urudi utaratibu wa zamani wa kila mwanachama wa CCM arudi kupiga kura za maoni. Huu mchakato wa sasa hivi ndio una rushwa zaidi.
Angalia wajumbe ukumbini wanakaa katika kata zao, wanakwenda kupiga kura katika kata yaani hawaachani kama pete na kidole. Hii maana yake ni kwamba ukikamata wajumbe wote katika kata 6 kwenye Jimbo la kata 20 tayari unakuwa na zaidi ya kura 180 na kwa mtu mwenye hela na ambaye ana jina kubwa ni kitu rahisi sana tofauti na zamani ambapo huwezi toa rushwa katika watu wote.
Jambo la muhimu nililojifunza ni kuwa Jamii yetu ya kitanzania bado sana katika swala la elimu hamna mwananchi anayesikililiza hoja wala sera ya mtu ndani ya ukumbi, wala hamna anayeangalia kwamba huwa unasaidia jamii yako wanachoangalia ni nani alimuona kwa shilingi ngapi, wanaingia na majina mfukoni
Ili kusaidia Vijana ndani ya chama kisiasa inahitajika kuwepo na model mpya kabisa haya mambo ya kura ya maoni ni ya hovyo, la sivyo ijulikane moja tu kwamba ukitaka kuingia katika siasa tafuta hela kwanza kisha ingia katika Siasa
Ni mara 100 urudi utaratibu wa zamani wa kila mwanachama wa CCM arudi kupiga kura za maoni. Huu mchakato wa sasa hivi ndio una rushwa zaidi.
Angalia wajumbe ukumbini wanakaa katika kata zao, wanakwenda kupiga kura katika kata yaani hawaachani kama pete na kidole. Hii maana yake ni kwamba ukikamata wajumbe wote katika kata 6 kwenye Jimbo la kata 20 tayari unakuwa na zaidi ya kura 180 na kwa mtu mwenye hela na ambaye ana jina kubwa ni kitu rahisi sana tofauti na zamani ambapo huwezi toa rushwa katika watu wote.
Jambo la muhimu nililojifunza ni kuwa Jamii yetu ya kitanzania bado sana katika swala la elimu hamna mwananchi anayesikililiza hoja wala sera ya mtu ndani ya ukumbi, wala hamna anayeangalia kwamba huwa unasaidia jamii yako wanachoangalia ni nani alimuona kwa shilingi ngapi, wanaingia na majina mfukoni
Ili kusaidia Vijana ndani ya chama kisiasa inahitajika kuwepo na model mpya kabisa haya mambo ya kura ya maoni ni ya hovyo, la sivyo ijulikane moja tu kwamba ukitaka kuingia katika siasa tafuta hela kwanza kisha ingia katika Siasa