Maombolezo ya Kawawa na Rais Mpirani

Ninajaribu kuangalia maisha ndani ya familia ambapo baba wa kaya anaagiza kuwa nyama itakuwa inaliwa siku ya sikukuu tu kutokana na hali ngumu ya kipato, siku nyingine zote watakula kauzu. Halafu baba huyo huyo anakuwa ananunua nusu kilo ya nyama kila siku kwa ajili yake tu: watoto na mama wanakula kauzu, je hiyo ni sahihi? Ingawa jambo hilo inafanyika katika baadhi ya kaya zetu, siyo jambo jema na linajenga tabia mbaya kwa watoto kuwa wanafiki na waongo. Kikwete ni kiongozi wa kaya, na kwenye hili la maombolezo ya kitaifa alitakiwa aonyeshe mfano siyo kuagiza wengine waomboleze yeye asherehekee. Kuna mambo ambayo anaweza kuendelea nayo wakati wa maombolezo lakini siyo hili kwenda kushangilia timu ya taifa wakati anaomboleza; huko ni kulinafikia taifa kuwa anaomboleza huku kumbe hana taimu na maombolezo hayo; ni afadhali angesema kuwa Taifa litaomboleza kwa siku tatu tu ingeeleweka.


Nikirudi nyuma, nakumbuka kuwa rais huyu huyu aliwahi kukatisha mkutano na watanzania huko uingereza bila kujibu maswali kusudi eti akatazame mpira, halafu baadaye akapanga safari nyingine ya kurudi uingereza ili akajibu maswali aliyokwepa!!
 
Nilidhania taifa liko kwenye maombolezo ya aliyekuwa Waziri Mkuu na Makamu wa Rais na muasisi wa taifa hili kwa siku saba. Aliyetutangazia maombolezo hayo yuko mpirani kuhamasisha ushindi.. hivi alishindwa hata kujibanza Ikulu kuangalia kwenye big screen na kumtuma waziri mmoja hivi..kweli ilimpasa kwenda?

MM..
Maneno yako yatamfanya Muungwana asiende tena uwanjani tar 7 (Rwanda Vs Kina Drogber) Coz alikuwa na mpango huo...
muachen atanue jaman..hamjui huu waweza kuwa mwaka wake wa mwisho..
Ponda mali kufa kwaja
 
Lazima tukubali JK ni mtu wa watu, anajichanganya sana, tena nadhani urais ni kikwazo kwake otherwise angeendelea kuripoti Msondo pale Amana, kujiwe cha Saigon etc.
Hata hivyo, hili la kuwa mtu wa watu, sio excuse ya madhaifu yake judgment, kwenye issues ndogondogo tusizikuze, hakuna ubishi JK ni mtu wa avarage inteligence, hatuna sababu ya kumvua nguo hata kwenye issues zinazohitaji average common sense.

Tupunguze malalamiko, turudi kwenye kupanga strategies, tufanye actions, tusonge mbele!.

Mkuu Pasco,

Nafikiri hapo kwenye BOLD umemaliza yote.

Itakuwa ajabu kama tutaendelea kujadili kwenda au kutokwenda kwa Muungwana kwenye mechi ya Mpira.

Labda cha kufanya ni kuangalia nini kifanyike ili mtu wa aina hii asiwe kiongozi na hata kama akiwa basi watu wanaomzunguka (walau wabunge) wasiwe watu wa "Mfalme leo kapendeza kinomaa na hili vazi lake lisiloonekana." Kama wakubwa hatulioni basi vitoto vitasema "mfalme yuko uchi".
 
Sasa wapi mnako elekea asingekuwepo Uwanjani mngeanzisha thread tena, ameenda maneno tena binadamu kweli hamridhiki, nilicho ona mm bendera zilipepea nusu mlingoti na wachezaji walisimama dk 1 kumkumbuka. Mambo mengine jamani muwe mnaangalia sio kila kitu kukosoa tu.
 
Jamani kawawa ameshamaliza safari yake duniani, let wengine tuliobaki tu endelee na maisha yetu, wanaoomboleza waomboleze moyoni lakini mie sioni ubaya wa rais kwenda huko mpiranii, walau ingekuwa ni mke wa marehemu tungesema katoroka eda! na mkumbuke hiyo michezo ilikuwa imepangwa tangu awali, sasa msiba ndio ulioingilia ratiba ya michezo maana umekuja ghafla! let us live our life ooh! na tuwaache wafu wapumzike kwa amani amen
 
Nilidhania taifa liko kwenye maombolezo ya aliyekuwa Waziri Mkuu na Makamu wa Rais na muasisi wa taifa hili kwa siku saba. Aliyetutangazia maombolezo hayo yuko mpirani kuhamasisha ushindi.. hivi alishindwa hata kujibanza Ikulu kuangalia kwenye big screen na kumtuma waziri mmoja hivi..kweli ilimpasa kwenda?
Mzee mwanakijiji Sitarajii mwelewa kama wewe uwe na chuki zisizo na msingi[nachelea kutumia neno halisi kwa kuhishimu JF Lakini inaelekea una biff kubwa na bwana Mzee. Wenzangu nyie alivyoahirisha spichi yake ya mwaka ambayo ilitakiwa aitowe mlimponda sana na kusema ingawa kuna msiba lakini ile spich ni ;national issue na ni muhimu angeitowa siku ya mkesha. Maskini jamaa alifanya vile kwa sababu ambayo watu wa kawaida walielewa. Na alipotoa hiyo spich siku ya tarehe 1 mkaanza kuiponda sasa tarehe 4 amekwenda kwenye shughuli ya kitaifa mnasema mbona nyinyi wazee mlianza sherehe ya mwaka mpya kwa kunywa kustarehe hivi ule msiba nyie haukuwahusu????
 
Mzee mwanakijiji Sitarajii mwelewa kama wewe uwe na chuki zisizo na msingi[nachelea kutumia neno halisi kwa kuhishimu JF Lakini inaelekea una biff kubwa na bwana Mzee. Wenzangu nyie alivyoahirisha spichi yake ya mwaka ambayo ilitakiwa aitowe mlimponda sana na kusema ingawa kuna msiba lakini ile spich ni ;national issue na ni muhimu angeitowa siku ya mkesha. Maskini jamaa alifanya vile kwa sababu ambayo watu wa kawaida walielewa. Na alipotoa hiyo spich siku ya tarehe 1 mkaanza kuiponda sasa tarehe 4 amekwenda kwenye shughuli ya kitaifa mnasema mbona nyinyi wazee mlianza sherehe ya mwaka mpya kwa kunywa kustarehe hivi ule msiba nyie haukuwahusu????

duhhh.wewe kweli Abunuwasi
 
Nilidhania taifa liko kwenye maombolezo ya aliyekuwa Waziri Mkuu na Makamu wa Rais na muasisi wa taifa hili kwa siku saba. Aliyetutangazia maombolezo hayo yuko mpirani kuhamasisha ushindi.. hivi alishindwa hata kujibanza Ikulu kuangalia kwenye big screen na kumtuma waziri mmoja hivi..kweli ilimpasa kwenda?

kwa hili namtetea, ya kaisali mpe kaisali..... hapa lazima tujilaumu wote si rais tu hata hao TFF kuidhinisha mechi kubwa wakati wa maombolezo ya kawawa.
 
Yakhe Mzee wakati mwengine unabowa! Hivyo kufa kwa mtu mmoja ndani ya Taifa ndio kila kitu kisimame? Basi vilabu vya Pombe na hata hii burudani ya JF vyote vifunge! Mzee una kisu na muungwana na pengine ummoja wa wale waliowaona yeye mwenyewe!

Chukua tano Mkuu, naona MM anambana sana JK, naona nitaanza kuziangalia Thread zake zingine naona duh zinazidi....
 
Kimya cha Dakika moja kilifanyika. Maombolezo ya siku 7 na bendera kupepea nusu mlingoti, the rest ni issues za judgement, a man with a mission to sell Tanzania, as a sales man, baada ya kutoa pole, unapanga na bidhaa zako bazarani kwa wafiwa ili wale wanaokuja kutoa pole wazione nao japo wanunue. Msiba umemkuta kipindi cha mauzo, as a good salesman of his nation, maadam tumeshiriki hatua zote mpaka maziko, then life goes on, biashara kama kawa.

RIP Simba wa Vita.
Pasco, you have clearly put it. Hata msibani tunacheka kama la kuchekesha lipo. Kushusha bendera nusu mlingoti ni ishara tosha ya maombolezo.
RIP Rashid Mfaume Kawawa.
 
Yakhe Mzee wakati mwengine unabowa! Hivyo kufa kwa mtu mmoja ndani ya Taifa ndio kila kitu kisimame? Basi vilabu vya Pombe na hata hii burudani ya JF vyote vifunge! Mzee una kisu na muungwana na pengine ummoja wa wale waliowaona yeye mwenyewe!

From the bottom of your heart and brain are you really convinced that it was necessary for the PRESIDENT to go to that football match? Hivi hana vitu vingine vya maana vya kufanya au hata kujipumzisha yeye mwenyewe kutokana na ushauri aliopewa na madaktari?! Sishangai kusikia watu wanasema kwamba aligombea urais na kuupata just for FUN!
 
Sasa wapi mnako elekea asingekuwepo Uwanjani mngeanzisha thread tena, ameenda maneno tena binadamu kweli hamridhiki, nilicho ona mm bendera zilipepea nusu mlingoti na wachezaji walisimama dk 1 kumkumbuka. Mambo mengine jamani muwe mnaangalia sio kila kitu kukosoa tu.

mimi si mmoja wao; kwani nabeza sana jinsi tunavyotukuza vitu ambavyo tunajua hatujagharimia kuviboresha. Kila Taifa Stars ikicheza tunafikiri utatokea muujiza kuwa itakuwa timu nzuri! Asingeenda mimi wala nisingefikiria mechi hiyo ya Ivory Coast.. ni waota ndoto ndio wanafikiri kuwa mechi hii itabadilisha soka la Tanzania!

Niliandika miaka miwili iliyopita kujiandaa na Olimpiki ya 2012.. hizo bilioni 7 zingeanza kutumika leo kuandaaa timu hiyo mnajua ingekuwaje..? well.. we don't think that far ahead anyway..
 
Pasco, you have clearly put it. Hata msibani tunacheka kama la kuchekesha lipo. Kushusha bendera nusu mlingoti ni ishara tosha ya maombolezo.
RIP Rashid Mfaume Kawawa.

sasa si wangeshusha hayo mabendera tu tungejua amekufa mtu fulani muhimu.. mambo ya kutukalisha chini na kutuhutubia kama taifa ilikuwa na haja gani?

I'm tired.. I already made my point.
 
kwa hili jamani mi sidhani kama rais amefanya kosa. Kumbuka yeye ni rais wa nchi na anayo majukumu mengine kama rais ya kufanya ikiwemo kuhamasiha michezo nchini mbona mle mpirani walimkumbuka marehemu kwa dakika moja kwani hiyo haitoshi?
 
Duuh!Kuna chuki zingine too much,maana huyo mwanakijiji amemchukia Kikwete kiasi kwamba kila anachokifanya Kikiwete ni baya na la kijinga!
 
Mwanakijiji
Nadhani unalako binafsi na JK, huu ukosoaji sasa umezidi na unakera.kama umekosa hoja bora utulie na usubiri pumba za CCM uziandikie.

kwa taarifa yako kuna watu muhim wanakufa hata huko ulaya sports inatumika kama njia moja wapo ya kujifariji, michezo si siasa, michezo ni njia moja wapo ya kujifariji.kama wewe unaona JK alikosea sijui ni wawapi wewe...naona tangu uweke picha ya JK yupo hospitali anaazindua machine pale muhimbili umekua hauna hoja.
Semenya naona unabwabwaja hutoi hoja kusuport your argument. MM anatoa hoja hata kama wengi wanampinga. Hoja yangu katika hili ni kwamba both parties in this thread wako right depending on which angle one is trying to look at.
1. Kikwete anakuwa wrong pale ambapo kama rais wa nchi anashindwa kujua kwamba kuna wakati anahitaji kutumia busara ili asiingie kwenye unnecessary controversies kama hizi. Kwa mfano angeweza kutoa salamu za kuwatakia ushindi Taifa Stars na akaapologize in public kwamba hataweza kuattend hiyo match kwa sababu ya tukio la msiba ambalo linamhusu sana yeye. Nadhani asingekuwepo wa kumlaumu kwa yeye kutokwenda uwanjani. So he could just stay at home and watch in the telly.
2. Kikwete pia anaweza kusema kuwa though ni mechi ya kirafiki lakini it is an historic event kwa Tz kucheza na Ivory Coast. Kikwete can attend the match in a mourning mood kwa sababu pia kabla ya mpira kuna dakika chache za recognition ya marehemu. Nafikiri tuache allowance kidogo kwa great thinkers kuwa rational rather than kutaka wote tukubaliane na jambo moja. Mara nyingi mawazo yanatokana na strong or rational beliefs kuhusu msiba among JF members. Kuna baadhi ya beliefs mfano Born Again Christians wao ni jambo la furaha mtu anapokufa akiwa believer and they can as well thank God and be happy for that cos the person has joined with Him in heaven. Lastly naomba tusiwe na very strong views kwenye hilo. Lets give him the benefit of the doubt, tumkomalie pale anapocheka na mafisadi badala ya kuwashughulikia.

 
Ndugu zangu lets be realistic tuko krne ya 21, tusifanye mambo kama wajinga wajinga, kwenda mpirani siyo big issue, tumuache na yeye akajionee wote tunajuwa anapenda mpira na michezo kwa ujumla kwa hiyo ni vizuri sana kaenda kupumzika na kuipa support timu yetu ya taifa.
Usipoenda mpirani ndiyo atafufuka?? hata hivyo unajuwaje kama watoto wake mwenyewe hawakwenda mpirani, after all life must go on man!!! Hivi mnajuwa nchi zilizoendelea maiti huwa zinakaa kwenye mafridge, watu waneandelea na kazi mpaka siku ya kuzika, wanazika then kesho yake au siku ile ile watu wanarudi kwenye shughuli zao, lazima tubadilike bwana. Kwenda mpirani siyo issue. Na pia haimaanishi kuwa kitu chochote kibaya, hata hivyo tumshukuru sana mwenyezi Mungu huyu baba ameishi zaidi ya miaka 70 iliyoandikwa kwenye vitabu vya dini, kwa hiyo tumshukuru sana Mungu na tuendelee na maisha yetu.
Raisi kututangazia maombolezo ya siku saba is ok, bendera zitakuwa nusu mlingoti, na life will go on as usual.
 
Shukran Chesty kwa kukamilisha hoja kwa namna bora kabisa! Kwa Mkuu MMKJJ unayo point kuhusu kipi bora Mh. Rais angefanya wakati huu kuonyesha umakini wake, lakini thread hii haikuwa ya lazima sana na inawezekana ikachangia kupunguza uzito wa kero ya uongozi hafifu tuliyonayo juu ya utawala wake. Hebu tumchambue kwa yale yenye uzito zaidi kwa mustakabali wa Taifa letu.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom