Manumba alazwa ICU Aga Khan

Manumba alazwa ICU Aga Khan

adui yako muumbee apone ili unapofanikiwa ajionee kwa macho
 
malaria? Kwani JK hakumugawia chanarua alichobadirishana na dhahabu zetu! Kama aligawiwa Manumba anadharau tangazo la Bi Kidude kuhusu matumizi ya vyandarua tulivyo gawiwa na sirikali.
 
Mashehe,watabiri na wachawi wapiga ramri wanasemaje kwa hili ,atakufa ama hafi?
 
"..Mpeni pole lakini ijulikane kuwa hata ukiwa mwamba kiasi gani, jua Maisha ni imara zaidi yetu.."
 
Mlivyosoma hii tarifa nikajua ni yule jamaa niliesoma nae Dar tech mwanzoni mwa miaka ya 2000. Get well soon kiongozi
 
Breaking News: Manumba alazwa ICU Aga Khan

HALI ya Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai, DCI Robert Manumba ni mbaya na amelazwa katika Hospitali ya Aga Khan, kwenye wodi ya wgonjwa Mahututi (ICU) jijini Dar es Salaam akisumbuliwa na ugonjwa wa malaria.

Kwa mujibu wa taarifa zilizonaswa na Habarimpya.com hivi punde ni kwamba Manumba amelazwa katika Hospitali hiyo tangu juzi.
Hata hivyo vyanzo vya kuaminika ndani ya Jeshi la Polisi nchini zinadai kwamba hali ya Mkurugenzi huyo wa makosa ya jinai nchini ni mbaya.......

MY TAKE:
Eah Mwenyezi Mungu Msaidie Kiumbe wako huyu apone haraka aje atutumikie watanzania kama alivyotutumikia Jana na juzi na kesho afanye hivyo,
Umzidishie maisha marefu aishi ili aine kesho na kesho kutwa.
Amin!


Hakuna Mkurugenzi wa mashtaka Tanzania anayeitwa Manumba...
 
si wengine huwa wanawapeleka India, huyu ndo kusema serikali haina hela? Aishi ili aone mengi
 
To hell na bado, wote wanaokwamisha mabadiliko Mungu atawaondoa, Mwigulu, Nape, Tiss and others
 
Kisasi ni cha MUNGU,msimhukumu ilanafsi yake inamsuta kama alishiri si tu kumtesa ULIMBOKA bali hata kufumbia macho watu waliomtesa,tumombee apone ila tuendelee kumuachia MUNGU wale wote waliomwaga damu za watz wengi,baadhi ni Mwangosi,wafanyabihashara wa madini,waandamanaji (zanzbar,arusha,morogoro nk)

siwezi kumwombea mtu mwenye 'ushetani' ndani yake
 
Hawa ndio wanatesa na kuua madaktari; lakini wakiugua wanataka huruma ya madaktari. Huyo angepigwa sindano ya sumu tu!!!
 
MY TAKE:
Eah Mwenyezi Mungu Msaidie Kiumbe wako huyu apone haraka aje atutumikie watanzania kama alivyotutumikia Jana na juzi na kesho afanye hivyo,
Umzidishie maisha marefu aishi ili aine kesho na kesho kutwa.
Amin!

Kama kuishika kwenyewe ni kwa stahili hiyohiyo ya kulinda UFISADI ambao unakunufaisha wewe huko UGHAIBUNI ndio maaan povu linakutoka hapa.
Potelea mbali yeyeyote aje lakini my wish ndio hiyo, sawasawa DADA.

Naona "YOUR TAKE" inabadilika kila sekunde.
Ungeiacha ile ile ya mwanzo ambayo inaonesha rangi zako halisi. By the way mie ni MWANAUME, sio DADA.
 
Back
Top Bottom