LOVI MEMBE
JF-Expert Member
- Mar 16, 2012
- 1,122
- 183
.
Ameeleza mafanikio yake kupitia kampuni yake ya Quality Plaza na dunia inavyomthamini. Ila amesema nchi yake haimthamini.. Sijajua nini maana ya Manji kusema nchi haimthamini, anakusudia nini Maana nchi ni watu na viumbe..
Anasemaje sisi watanzania hatumthamini wakati tumempa udiwani Mbagala na tumempa uenyekiti Yanga.
uyu igwite ibyata maanake ameshiba anabeua msamehe mwenye shibe hamjui mwenye njaa. mtu ukimkaribisha sebuleni anataka aingie chumbani kosa ukimkaribisha chumbani atataka hata stahiki yako iwe YAKE. MUACHENI AENDELEE KUBEUA WATANZANIA WANGAPI HAWANA FURSA KAMA YEYE AU YEYE ANA HAKI KULIKO WENGINE?
Naomba Manji atupe ufafanuzi ni nchi haimthamini au viongozi ndio hawamthamini?
Atueleze vizuri..
Ni kweli anaweza kuhama nchi ila tujue tu atahama na ajira za watu kibao ambao mpaka sasa serikali bado haijajipanga kuwapa ajira wala kuwawezesha kujiajiri.
Siungi mkono ufisadi ila nawakubusha tujadili haya mambo kwa kuangali pande zote ili watu waweze kujipanga.
Manji anataka athaminiwe kwa kwendakutafuna futari ikulu kama ilivyokuwa miaka kumi iliyopita halafu apewe na deal kama alivyokuwa anapewa na liprofeseri la msogaIle habari kuhusu majina ya mfukoni ilikuwa uongo?
Nchi yake ipi? Tanzania? Ngoja nikae kimya
Kuna watu huwa wanashindwa kujenga hoja na kukimbilia kutukana au kujaribu kuleta lugha za kihuni. Mimi na Manji hatujuani na wala sina maslahi naye kwa vyovyote vile. Hapa ninachotaka kujulishwa sifa za mtu kuwa mtanzania ni zipi? Mimi na Manji tuna tofauti kubwa sana.
1. Manji ni Muislam mimi ni Mkristo.
2. Manji CCM mimi CHADEMA
3. Manji anaishi Dar mimi naishi Iringa
4. Manji ni Yanga mimi ni Simba
5. Yeye Mhindi mimi Mnyamwezi
4. Yeye Mfanyabiashara Mkubwa mimi Machinga
Mjadala huu ni kutaka kujua sifa za mtu kuwa mtanzania na wala si mjadala wa ufisadi wa Manji au utajiri wake ameupataje. Ikifika kujadili ufisadi wake basi huko tutajadili ufisadi. Lakini katika hili hakuna mwenye hoja za kushiba kueleza ni kwa nini wengi wenu mnafikiri kwamba Manji si mtanzania. Kama tukizijua sifa za utanzania basi ndiyo tutaweza kujua kama Manji ni mtanzania au la.
Somji Juma alisema unaweza kuwa Raia wa Tanzania lakini usiwe Mtanzania. Nikataka kufafanuliwa inakuwaje uwe Raia wa Tanzania ingawa si Mtanzania. Mimi sikuelewa lakini Mzito Kabwela alimuelewa, na wengine pia labda wamemuelewa. Ninachotaka kueleweshwa ni hiki. Utanzania ni nini?
magufuli anamchukia sana Manji, sijui alimfanyia nini...manji amesaidia watu wengi sana mpaka club yetu ya Yanga
@Elli ndiyo Tanzania ni nchi yake kwani ana uraia wa nchi nyingine? Kuna tatizo la watu kuwaza kwamba wahindi siyo watanzania. Ni bahati mbaya sana!!
Ni kweli anaweza kuhama nchi ila tujue tu atahama na ajira za watu kibao ambao mpaka sasa serikali bado haijajipanga kuwapa ajira wala kuwawezesha kujiajiri.
Siungi mkono ufisadi ila nawakubusha tujadili haya mambo kwa kuangali pande zote ili watu waweze kujipanga.
Pimbi tutembee kwenda wapi? Tunaona ubaguzi America hadi kwenye Campain za Urais, tumeona South, tunauona kila siku kwenye shughuli zetu mjini.
Kwa Ufupi India naijua kuanzia Bihar mpka Mumbai. Wahindi ni wezi tu na wanatudharau, bora mchina kuliko Muhindi.
kwa nini hawako jeshini au kuna sheria inazuia wao ni biashara tu kama vp warud india
ndugu mtetezi wa wahindi... nitajie mtu mweusi yoyote aliyetoka nanjilinji kule lindi ambae ana uraia wa India na akawa na priviledges kama za wahindi hapa Tanzania, pia niambie kwanini watanzania wenye asili ya India hua wanapenda kujifungia kwenye nyumba zao walizokodisha nhc, bila kuchangamana na watanzania wenzao wa tandale, pia nipe mfano wa ndoa baina ya Masai wa arusha na mtanzania mwenye asili ya india.
Tumia akili japo kiduchu tu, unawajuwa Wahindi? Jamal aliaminiwa na nyerere na akampa uwaziri wa fedha hebu tueleze alipokufa alikwenda kuzikwa wapi? hivi ujinga ni kipaji kumbe?