As if TZ kuna machaguo ya kazi.
Wangekuwa wajinga kama wangeacha kazi na kuwa jobless. Weka input ndogo upate output kidogo; so wanadeliver kutokana na serikali yenu inachowapa, la watakuwa mafala kuibiwa nguvu zao.
Private schools mwalimu wa primary (ndugu yangu) ana degree ya ualimu na anaondoka na 1.5m per month na anadeliver kazi yenye same thamani. So mwl anayelipwa .3m tegemea na kazi yake itakuwa pungufu mara 5 ya anaye lipwa 1.5m
Kaunga sikubaliani na wewe.
Namna hii hatuwezi kujenga hii nchi, kama ni swala la mishahara midogo nchi hii kila sekta ina mishahara midogo, namna hii ni kuwafanya ng'ombe kuwa na akili kuliko binaadamu, ng'ombe akikataa kunywa maji hanyw'i ng'o, kwa nini walimu wanashindwa kukataa kufundisha kama wanaona hawapati wananchokitaka.
naona watu wote tumeamua kuangalia upande mmoja tu kiasi cha kusababisha ionekane walimu hawawajibiki kwa namna yoyote ile na hili tatizo.
Mimi binafsi nimesoma katika shule za namna hii hii, walimu wanapata pesa nyingi tu kwenye tuition hasa mjini, wajijini wanaweza kujikimu vizuri tu kwa kilimo, na wengi wanafanyisha wanafunzi kazi kwenye mashamba na bustani zao, in fact kila sehemu wanayohishi walimu wanapata favor nyingi sana, achilia mbali heshima wanayopewa, leo wanabehave kiajabu ajabu watu mnajitokeza kutetea.
sisemi kwamba hawastahili kupatiwa malipo mazuri, lakini nchi hii nani analipwa vizuri, watu wanataja wanasiasa na wakuu wenginine serikalini, wakati hawa tayari kuna agenda iyosambaa nchi nzima kwamba ni mafisadi, au ndio tumefikia hatua ya kutamani ufisadi wao?