Mangula: Lowassa bora uondoke kuliko kuivuruga CCM

Mangula: Lowassa bora uondoke kuliko kuivuruga CCM

tatizo la vijana wa lumumba hawajui hata kanuni za chama chao,kumbe kosa la chadema ni kusimamia kanuni tnen kutekeleza mnao watetea wakina ZITTO mko wapi?mbona leo mmekimbia maana nape na CCM yake amesema wanaofanya hivyo ni kinyume cha kanuni za chama,ila kwa chadema iwe si kinyume nawataka leo hapa wakina tuntemeke na ttema mate na sixgates
 
EL ni wa Kaskazini, Tena anaurafiki mkubwa na viongozi wa CDM, na habari zinazoenea mtaa wa ufipa ni kuwa akipigwa chini huko aliko basi atapewa mikoba ya kupeperusha bendera ya CDM come 2015.
Kwa hiyo Mangula kwa vile ni wa Nyanza za juu kusini/Kusini anataka kushindana na ukaskazini sivyo? haya mawazo ni sumu inayotutafuna Watanzania, angalieni sifa stahiki za mtu na siyo dini, kabila ama ukanda. Kumbukeni huyo hapigiwi kura na wazaramo ama waluguru pekee bali Watanzania.
 
Hongera Mangula kama kweli yametoka kinywani mwako, lakini nauliza mbona CCM mnamhamasisha ZZK adai haki yake CDM? Vivyo hivyo hata Lowasa nae anadai haki yake ya kugombe 2015. Patamu hapo haya ni mawazo yangu binafsi sina mrengo wa mtu au chama.
Haki haiji bila wajibu!

EL ni msumari wa moto kwa mafisadi ndani ya ccm wanajua akiingia yule ule ulaji wa bila kunawa utakuwa haupo tena na ulelege wa viongozi pamoja na kutoletewa maendeleo wananchi utakufa. EL ni mlaji wa kisayansi huku kazi zikionekana waziwazi tena kama ni hiyo Richmond alishaeleza ni ya nani EL ni kiama cha wahindi na mabwana zao kwa jina la uwekezaji
 
tatizo la vijana wa lumumba hawajui hata kanuni za chama chao,kumbe kosa la chadema ni kusimamia kanuni tnen kutekeleza mnao watetea wakina ZITTO mko wapi?mbona leo mmekimbia maana nape na CCM yake amesema wanaofanya hivyo ni kinyume cha kanuni za chama,ila kwa chadema iwe si kinyume nawataka leo hapa wakina tuntemeke na ttema mate na sixgates
Wao ndio wahusika wa kwanza katika kusimamia na kuhakikisha hilo shauri linakuwa wanavyotaka, kumbe leo lazima wapo busy kupitia mwenendo wa kesi na kupanga plan B.
 
CCM inabidi wawe waangalifu sana na Mtandao huu wa Nchimbi, Mwigulu. ZZK, Hamad Rashid, Kafulila. Jan Makamba, Sophia Simba na sasa wamemwingiza na Fenella kukamata media. waangalie sana na wasimpuuze nape. hii ya CDM ni sehemu ya huo mchezo uliopangwa
Nadhani katiba ya CCM bado inatambua mfumo wa chama kimoja, vinginevyo wangejitahidi kulea mfumo wa vyama vingi na kuukubali. Huwezi kupambana na mfumo wa vyama vingi kwa kuua upinzani kwa nguvu nje ya sera na matendo ya kutekeleza sera. Ukiona chama kinapambana na wapinzani kwa nguvu nje ya sera, basi mfumo wa vyama vingi haujaeleweka na haujakubalika. Anayejua katiba ya CCM anisaidie nijue inavyosema juu ya mfumo wa vyama vingi nchini Tanzania.
 
Ama kwel mkuki kwa nguruwe kwa binadam mchungu. . yamewakuta tena CCM km yalivyotokea CHADEMA!!babu alikuja juu mno na harambee jaman na kiukweli wananchi wanaofikir vizur walishajua nia ya Babu yetu .kwakweli mimi ni mwana CCM lkn akisimama Lowassa kugombea Urais...kimya kimya!!!ntawaambia ngoja tusubir tuombe uzma
 
Sasa hapa unataka tujadili nini?Hivi uliishia darasa la ngapi vile?Isijekuwa tunajadiliana na standard seven graduate hapa
ukirusha jiwe gizani ukisikia uwiiiiii ujue limempata sasa kama ujaona cha kujadili pole,elimu si ya darasani mkuu elimu ni jinsi gani unaisaidia jamii yako na wewe unaitumiaje kupambana na mazingira unayoishi mimi leo nawataka vijana wa lumumba mje mmseme Mangula kuwa amekosea
 
EL ni msumari wa moto kwa mafisadi ndani ya ccm wanajua akiingia yule ule ulaji wa bila kunawa utakuwa haupo tena na ulelege wa viongozi pamoja na kutoletewa maendeleo wananchi utakufa. EL ni mlaji wa kisayansi huku kazi zikionekana waziwazi tena kama ni hiyo Richmond alishaeleza ni ya nani EL ni kiama cha wahindi na mabwana zao kwa jina la uwekezaji

Mimi sijaandika kumtetea Lowasa, hafu we ni mwongo unataka kunifanya mi nimwamini EL? kwa lipi kijana kwanza hao wahindi ndo marafiki zake mfano Rostam, pili hizo pesa ambazo anaenda kuchangia katika harambee zinatoka kwa nani si ni bora aikopeshe serikali iboreshe huduma kwa wananchi, naupinga sana Urais wa kupita nyumba za ibada, unadhani wasio na dini hizo za kikristu na kiislam wakiamu kumchagua Rais wao itakuwaje?
 
Unalinganisha na waraka wa ushindi 2013 by Samson mwigamba?lakini hawa wenzetu hawatawafukuza wala kuwavua vyeo vyao akina fisadi EL na wala hawatawaita wahaini
soma waraka wa mangula kamwambia muasi msaliti na ni uhaini aondoke aache chama hivi wewe zinakutosha kweli au unadhani JF ni jukwaa la kwako ambapo unaweza kuongopa unavyotaka
 
Mimi napata shida kidogo kuamini kama Mangula na Nnape wanamzuia Lowassa kwa nia njema au na wao wana agenda zao binafsi au chuki binafsi tu kwa jamaa.
Jamaa ukimsikiliza akiongea ni kweli ni kampeni ya kiaina ya kujipigia chapuu kupata nafasi ya kuwania urais mwaka 2015, lakini binafsi jamaa namkubali sana na naona kama atatufikisha sehemu kimaendeleo kutoka tulipo sasa.
Mnaonaje wadau?
 
EL ni wa Kaskazini, Tena anaurafiki mkubwa na viongozi wa CDM, na habari zinazoenea mtaa wa ufipa ni kuwa akipigwa chini huko aliko basi atapewa mikoba ya kupeperusha bendera ya CDM come 2015.
Acha kujilembua lembua kimaandishi wewe unajichanganya kama wanawake wa kwenye madanguro huyo wa kaskazini si ndio alimwezesha Kikwete kuingia IKULU kwa pesa zake na marafiki zake na mtandao wake,bila Lowassa KIkwete asingeingia IKULU MKapa alishakataa mbinu alizofanya KIkwetekuingia IKULU kupitishwa na CC ya CCM ndicho atakacho fanya LOwassa, CCM hawana nguvu wala uwezo wa kumtosa Lowassa ndio nguzo yao bila Lowassa hakuna CCM
UNapenda kusema wakaskazini hawatakuja kushika uraisi ndivyo itakuja kuwa kwa pwani kanda ya kati nyanda za juu kusini magharibi na kaskazini watasema hatuwapitishi kanda ya ziwa na Pwani
 
Mimi sijaandika kumtetea Lowasa, hafu we ni mwongo unataka kunifanya mi nimwamini EL? kwa lipi kijana kwanza hao wahindi ndo marafiki zake mfano Rostam, pili hizo pesa ambazo anaenda kuchangia katika harambee zinatoka kwa nani si ni bora aikopeshe serikali iboreshe huduma kwa wananchi, naupinga sana Urais wa kupita nyumba za ibada, unadhani wasio na dini hizo za kikristu na kiislam wakiamu kumchagua Rais wao itakuwaje?

Tatizo umezaliwa juzijuzi; unakijua kilichomfanya EL asigombee urais mwaka 1995? walichukua fomu siku moja na Kikwete siku ya pili yake akaitwa nyumbani kwa Nyerere akaulizwa utajiri wote huu ulionao kijana mdogo kama wewe umeutoa wapi? akaambiwa arudishe fomu na akairudisha; na je unajua pesa iliyomuingiza Kikwete Ikulu ilikuwa ya EL na Rostam toka mifukoni mwao? najua utasema ni za EPA lakini epa iliandaliwa kwa ajili ya Sumaye chaguo la Mkapa kabla ya Sumaye kubwagwa pale dodoma EPA haikuwa ikimgharamia kikwete hadi kufikia hatua ile bali zilikuwa ni njuluku za EL kwa binafsi yake. Sasa unapotaka kuonyesha kwamba EL kaanza kushika mpunga juzijuzi katika kipindi cha awamu hii ya magumashi ya ufisadi ni kutoelewa somo; pia Rostam sio mhindi kwa taarifa yako na hoja yako ya nyumba za ibada ni upofu wa kutoona kinachoendelea sasa ndani ya nchi na namna hata uongozi wa ngazi za juu unavyoteuwa watendaji wa serikali kwa mlengo wa udini na kampeni za wazi kupigwa katika nyumba za ibada na watu hawafanywi lolote.
 
Acha kujilembua lembua kimaandishi wewe unajichanganya kama wanawake wa kwenye madanguro huyo wa kaskazini si ndio alimwezesha Kikwete kuingia IKULU kwa pesa zake na marafiki zake na mtandao wake,bila Lowassa KIkwete asingeingia IKULU MKapa alishakataa mbinu alizofanya KIkwetekuingia IKULU kupitishwa na CC ya CCM ndicho atakacho fanya LOwassa, CCM hawana nguvu wala uwezo wa kumtosa Lowassa ndio nguzo yao bila Lowassa hakuna CCM
UNapenda kusema wakaskazini hawatakuja kushika uraisi ndivyo itakuja kuwa kwa pwani kanda ya kati nyanda za juu kusini magharibi na kaskazini watasema hatuwapitishi kanda ya ziwa na Pwani

Kamwe Rais hata toka Kaskazini - Mwalimu
 
MiCCM kwa porojo hawajambo, fukuzeni Lowasa kama CDM walivyofanya kwa Zitto.
 
Sasa EL atarudishaje pesa aliyoonga miskitini na makanisani?.Chonde chonde miskiti na makanisa mliyopewa pesa na EL,tafadhari rudisheni chenji mlizobakisha kwa Lowassa.
 
Kijana unadhani hayo yote siyajui, kisa cha yeye kuukwaa ukwasi wote huo wakati ni mtumishi wa Umma? au kuwa mkurugenzi AICC kipindi hicho ndo kiwe kisingizio? au kisa ni mfugaji? hata roho haikuumi? Sasa unataka tukuamini kuwa pesa ya kampeni mwaka 2005 ilitoka mfukoni mwake? aliuza mifugo? maana yeye siyo mfanya biashara, kwahiyo CCM hawakuwa na pesa? na kama alikuwa anautaka urais mwaka 2005 kwanini hakugombea? Pole sana nadhani mnacheza na akili za watanzania nakushauri uje upime upepo huku ktk mikoa ya magharibi, Ziwa Victoria na Nyanda za juu usikie wapiga kura wanamuongeleaje!

Tatizo umezaliwa juzijuzi; unakijua kilichomfanya EL asigombee urais mwaka 1995? walichukua fomu siku moja na Kikwete siku ya pili yake akaitwa nyumbani kwa Nyerere akaulizwa utajiri wote huu ulionao kijana mdogo kama wewe umeutoa wapi? akaambiwa arudishe fomu na akairudisha; na je unajua pesa iliyomuingiza Kikwete Ikulu ilikuwa ya EL na Rostam toka mifukoni mwao? najua utasema ni za EPA lakini epa iliandaliwa kwa ajili ya Sumaye chaguo la Mkapa kabla ya Sumaye kubwagwa pale dodoma EPA haikuwa ikimgharamia kikwete hadi kufikia hatua ile bali zilikuwa ni njuluku za EL kwa binafsi yake. Sasa unapotaka kuonyesha kwamba EL kaanza kushika mpunga juzijuzi katika kipindi cha awamu hii ya magumashi ya ufisadi ni kutoelewa somo; pia Rostam sio mhindi kwa taarifa yako na hoja yako ya nyumba za ibada ni upofu wa kutoona kinachoendelea sasa ndani ya nchi na namna hata uongozi wa ngazi za juu unavyoteuwa watendaji wa serikali kwa mlengo wa udini na kampeni za wazi kupigwa katika nyumba za ibada na watu hawafanywi lolote.
 
Ngoma ya segere ndani ya chama kubwa immeansa

Kama nakumbuka vizuri maneo ya Mhe. Lowasa yalikuwa yakushukuru wanachama na wale wenye mapeni mema kwa kumuunga mkono katika safari yake yenye matumaini. Hakusema kwamba safari hiyo ni ya kugombea Uraisi. Pengine ameamua kuwa Mchungaji na kama ni hivyo kwa nini Uongozi wa CCM unaanza kumshutumu hata kabla hajaweka bayana nia yake? Hakika hii siyo demokrasia ni ubabe na chuki binafs.i
 
Kijana unadhani hayo yote siyajui, kisa cha yeye kuukwaa ukwasi wote huo wakati ni mtumishi wa Umma? au kuwa mkurugenzi AICC kipindi hicho ndo kiwe kisingizio? au kisa ni mfugaji? hata roho haikuumi? Sasa unataka tukuamini kuwa pesa ya kampeni mwaka 2005 ilitoka mfukoni mwake? aliuza mifugo? maana yeye siyo mfanya biashara, kwahiyo CCM hawakuwa na pesa? na kama alikuwa anautaka urais mwaka 2005 kwanini hakugombea? Pole sana nadhani mnacheza na akili za watanzania nakushauri uje upime upepo huku ktk mikoa ya magharibi, Ziwa Victoria na Nyanda za juu usikie wapiga kura wanamuongeleaje!
Kibopa mwanzilishi wa migodi ya Arusha kabla serikali haijafungua macho unamjua? hivi watalii wanakuja Arusha kuangalia ng'ombe wa wamasai na AICC? Kwa kifupi Nyerere hakuamini watanzania maskini wangeweza kuongozwa na Rais tajiri kama Lowassa hasa baada ya misingi ya Azimio la Arusha kupigwa chini hao ndio aliokuwa anawaita nguruwe wa kufilisi shamba na akasema hawezi kuachia nchi yake ichukuliwe na ng'uruwe; kwa hiyo Nyerere alihofia kile ambacho kingetokea mbele na wala sio kile kilichokwisha kutokea. Sasa poa basi tuambie basi huyo ambaye sio fisadi nchi hii unayefikiria anaweza kuwa raisi manake ccm wote mafisadi, cdm ndio haohao waganga njaa hakuna atakayefanya kazi nje ya kulenga tumbo lake na familia yake si bora huyo anayejulikana atafanya kitu?
 
Mimi napata shida kidogo kuamini kama Mangula na Nnape wanamzuia Lowassa kwa nia njema au na wao wana agenda zao binafsi au chuki binafsi tu kwa jamaa.
Jamaa ukimsikiliza akiongea ni kweli ni kampeni ya kiaina ya kujipigia chapuu kupata nafasi ya kuwania urais mwaka 2015, lakini binafsi jamaa namkubali sana na naona kama atatufikisha sehemu kimaendeleo kutoka tulipo sasa.
Mnaonaje wadau?

Unachafua hewa na huyo fisadi wako bwana!!! wengine tuko mezani tunakula!!!
 
Unataka kuniaminisha kuwa yeye ndo aliyegundua Tanzanite? Na wakati huo Tanzanite inagunduliwa yeye alikuwa mtumishi wa umma na hakuwa naruhusiwa kumiliki biashara ilikuwaje akamiliki? huoni huo ni ufisadi? We unadhani Nyerere angeamua kubinafsisha au kujilimbikizia mali leo tungekuwa tunaweza kuongelea rasilimali za nchi hii? maana leo tungekuwa kama nchi nyingi tu za Afrika vurugu na vita.
Mimi siwezi kukutajia nani anafaa lakini ndni ya CCM kuna watu 2 ambao wannchi wanapenda sana utendaji kazi wao na ndiyo nguzo ya CCM kwasas kwani hata wakitaka kuongea mafanikio ya serikali ya JK lazima Wizara zao utazigusa, CDM yupo wananchi wanimani naye vilevile.

Kibopa mwanzilishi wa migodi ya Arusha kabla serikali haijafungua macho unamjua? hivi watalii wanakuja Arusha kuangalia ng'ombe wa wamasai na AICC? Kwa kifupi Nyerere hakuamini watanzania maskini wangeweza kuongozwa na Rais tajiri kama Lowassa hasa baada ya misingi ya Azimio la Arusha kupigwa chini hao ndio aliokuwa anawaita nguruwe wa kufilisi shamba na akasema hawezi kuachia nchi yake ichukuliwe na ng'uruwe; kwa hiyo Nyerere alihofia kile ambacho kingetokea mbele na wala sio kile kilichokwisha kutokea. Sasa poa basi tuambie basi huyo ambaye sio fisadi nchi hii unayefikiria anaweza kuwa raisi manake ccm wote mafisadi, cdm ndio haohao waganga njaa hakuna atakayefanya kazi nje ya kulenga tumbo lake na familia yake si bora huyo anayejulikana atafanya kitu?
 
Back
Top Bottom