Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,478
- 39,997
Ukimnyoshea mtu mkono kumpiga unaweza ukaurudisha angani au kuukwepesha usimpige au usimpate. Hata hivyo ukilitoa neno ambalo hukulimaanisha na likampata mwenzio huwezi na hauna jinsi ya kulirudisha. Neno likishatoka limetoka hata ukijaribu kulifuta halifutiki bali huacha alama. Lakini wapo watu ambao husema maneno makali wakiwa na hasira maneno ambayo japo wanaweza kujaribu kuyapoza kwa mabusu, miguso na samahani nyingi. NImeyasikia mengi sana kwa mfano mtu katika hasira anaanza kumuita mwenzie:
"Mpumbavu wewe"
"mwanamme gani wewe"
"malaya Mkubwa"
"Kwani miye mtumishi wako"
"Acha mambo ya kijinga"
Je kuna maneno ambayo umewahi kusikia watu wakiyasema na ukajua si mazuri kuambiana hasa watu ambao mnadai kupendana? Je wajua madhara ya maneno yalivyo katika hisia na mioyo ya watu? Inakuwaje mtu mtukanane halafu mwende chumbani pamoja? Je unajua wakati mwingine mtu anaenda pembeni ya pendo lake ili akapate maneno ya utulivu na ya kutulizwa?
THINK ABOUT IT: IF YOU DON'T MEAN IT DON'T SAY IT!
n.k n.k
"Mpumbavu wewe"
"mwanamme gani wewe"
"malaya Mkubwa"
"Kwani miye mtumishi wako"
"Acha mambo ya kijinga"
Je kuna maneno ambayo umewahi kusikia watu wakiyasema na ukajua si mazuri kuambiana hasa watu ambao mnadai kupendana? Je wajua madhara ya maneno yalivyo katika hisia na mioyo ya watu? Inakuwaje mtu mtukanane halafu mwende chumbani pamoja? Je unajua wakati mwingine mtu anaenda pembeni ya pendo lake ili akapate maneno ya utulivu na ya kutulizwa?
THINK ABOUT IT: IF YOU DON'T MEAN IT DON'T SAY IT!
n.k n.k