Maneno haya Mochwari yanauma sana!

Maneno haya Mochwari yanauma sana!

Hivi punde

JF-Expert Member
Joined
Apr 1, 2017
Posts
2,554
Reaction score
8,627
Wakuu. Kuna mochwari nilienda kumcheck ndugu yangu mmoja, akanitembeza mle ndani kwenye majokofu ya maiti kujionea miili ya watu iliyokata roho pamoja na mazingira yale.

Kuna maiti zilitokana na ajali, ugonjwa, uchawi n.k. Nikiwa humo ndani mochwari nikaona haya maneno kwenye ubao.

TULIKUWA KAMA WEWE, UTAKUWA KAMA SISI. USIJISAHAU!

Aina hii ya statement ya hawa marehemu inauma mpaka kesho.
 
Kufa siogopi ila huwa sipendi kuona maiti.

Kuna muda nawatamania waliofariki maana wanakuwa wamepata pumziko la milele.

Ikitokea umezaliwa sehemu nyingine unapata nafasi ya kurekebisha uliyoharibu mwanzo ulipokuwa duniani
 
Kama ulivyozaliwa ukiwa huna ufahamu wa jambo lolote vivyo hivyo ukifa ndio mwisho hautajua lolote na hakuna utakapoenda.

Yani ni mwisho mtimilifu. Dini hizi tu zimevuruga akili za watu.

Ukweli ndio huo.

Nikiwaza kufa naona bora nisingezaliwa, naogopa sana sana hasa kufukiwa kaburini natamani hata kungewezekana mwili wangu ungechomwa moto naogopa mnooo
 
Wakuu. Kuna mochwari nilienda kumcheck ndugu yangu mmoja, akanitembeza mle ndani kwenye majokofu ya maiti kujionea miili ya watu iliyokata roho pamoja na mazingira yale.

Kuna maiti zilitokana na ajali, ugonjwa, uchawi n.k. Nikiwa humo ndani mochwari nikaona haya maneno kwenye ubao.

TULIKUWA KAMA WEWE, UTAKUWA KAMA SISI. USIJISAHAU!

Aina hii statement ya hawa marehemu inauma mpaka kesho.
TULIKUWA KAMA WEWE, UTAKUWA KAMA SISI. USIJISAHAU!
 
Kufa siogopi ila huwa sipendi kuona maiti.

Kuna muda nawatamania waliofariki maana wanakuwa wamepata pumziko la milele.

Ikitokea umezaliwa sehemu nyingine unapata nafasi ya kurekebisha uliyoharibu mwanzo ulipokuwa duniani
Usiseme ivyo mkuu sio fresh kwani uhai ni zawadi.
 
Nikiwaza kufa naona bora nisingezaliwa, naogopa sana sana hasa kufukiwa kaburini natamani hata kungewezekana mwili wangu ungechomwa moto naogopa mnooo
Pole. Lakini unatakiwa kujua kuwa ni njia ya kila mmoja wetu. As long as unaishi (ulizaliwa) ujue tu kuna siku utakufa.

Unajua kwanini unahofia kifo? Soma huu uzi.

 
Nikiwaza kufa naona bora nisingezaliwa, naogopa sana sana hasa kufukiwa kaburini natamani hata kungewezekana mwili wangu ungechomwa moto naogopa mnooo

Na kuchomwa moto kwa madhambi ya hapa Duniani?
Well, binafsi siogopi kufa maana husikii wala kuhisi chochote. (There's no master nor slave in Grave) ila tukio la kuwaona ndugu zangu wakizikwa halafu sitawaona tena ndio linaniuma zaidi.
Binafsi sioni lengo la mimi kuumbwa na kuzaliwa kama after some time nitakufa, ndugu zangu watakufa hafu sitawaona tena kuna maana gani sasa yakuzaliwa??

Kuzaliwa ni upuuzi.
Screenshot_20220824-125308~2.png

 
Waliokufa Wana bahati kubwa sana,duniani hakuna la maana Mbona🙄tozo ndo usiseme🤦
Umenikumbusha biblia kitabu cha muhubiri

Muhubiri anasema kila kitu hapa duniani ni ubatili mtupu..Hamna Jambo la maana hapa duniani

Tunakula,tunashiba kisha tunasikia tena njaa,tunapata usingizi tunalala,tunaamka alafu tunalala tena..Unasikia genye, unagegeda unaridhika kisha baada ya Massa kadhaa unasikia tena hamu!!

Tunazaliwa,tunaishi,tunateseka na tozo alafu tunakufa..maisha yana maana gani sasa
 
Back
Top Bottom