Mandela-Kifo cha furaha nyumbani siyo Ulaya

Sawa lakini huduma ya hospitali za Afrika Kusini alizijenga Mandela? Je Waafrika wote wa Afrika ya Kusini wanapata huduma hizo bora na hivyo hawaendi nje ya Afrika ya Kusini kupata tiba? Na wakiamua kwenda kupata tiba nje ina maana hawana uzalendo.

Mandela kazi yake kubwa na aliikamilisha ilikuwa ni kumaliza au kukomesha ubaguzi wa rangi ingawa hata Wasouth Africa weusi ni wabaguzi sasa hivi kuliko wazungu.

Bahati mzuri mimi nimefika South Africa Mandela akiwa bado Rais na nimeshuhudia wazalendo wasio na nyumba wakigaiwa nyumba bure kwenye location za Cape town hasa Khayerisha na Guguletu na wapo Watanzania pia walionufaika na mpango huu wa Mandela wa kujenga na kugawa nyumba bure kwa wale waliojaza fomu za kuomba na waliokuwa na South African ID.

Kwenye mfumo wa afya South Africa kila Community ina hospital yake yenye facility za kiwango cha kufanyiwa oparesheni.

Hakuna Msouth Africa anayefikiria kwenda kubeba box UK na USA sembuse kutibiwa?

Kwa kifupi South Africa kuna chama cha weusi kinatawala lakini njia kuu za uchumi na Think tankers ni wale wale weupe.
 
Mandela kazi yake kubwa na aliikamilisha ilikuwa ni kumaliza au kukomesha ubaguzi wa rangi ingawa hata Wasouth Africa weusi ni wabaguzi sasa hivi kuliko wazungu.

Aah ok; nimekuelewa, Afrika ya kusini facilities zote za mambo ya afya ni za ubora wa juu na weusi wote hawahitaji kwenda nje kutibiwa kwani wanaweza kutibiwa ndani. Good for them.
 
Sawa lakini huduma ya hospitali za Afrika Kusini alizijenga Mandela? Je Waafrika wote wa Afrika ya Kusini wanapata huduma hizo bora na hivyo hawaendi nje ya Afrika ya Kusini kupata tiba? Na wakiamua kwenda kupata tiba nje ina maana hawana uzalendo.

mkuu unamaanisha hata kama Mandela amefia nyumbani hana tofauti na viongozi wengine wanaofia Ulaya.?
sababu ni kwamba huduma alizohudumiwa nyumbani sio yeye alieziboresha.!
 
mkuu unamaanisha hata kama Mandela amefia nyumbani hana tofauti na viongozi wengine wanaofia Ulaya.?
sababu ni kwamba huduma alizohudumiwa nyumbani sio yeye alieziboresha.!

Maana yangu ni kuwa kwa mgonjwa kutafuta tiba mahali popote inapowezekana ili kunusuru maisha yake ni haki yake ya msingi na hawezi kuchekwa kwa hilo. Kuona kwamba ati mgonjwa (awe kiongozi au la) kwenda kutafuta tiba isiyopatikana kwake ni kutokuwa mzalendo ni hoja duni na dhaifu. Hoja hii inashindwa kuelewa tofauti ya magonjwa mbalimbali, utaalam n.k. WAnaoitoa wanasema nchi yetu ingekuwa imejitosheleza kwa kila aina ya tiba na mahospitali yangekuwa na kila kitu ili Rais wetu wa kwanza (Nyerere) asingeenda kutafuta tiba.

Inaonesha ndugu zetu hata historia yetu ya nchi hawaijui au wameisahau. Baada ya miaka zaidi ya 40 ya ukoloni wakati wa Uhuru Nyerere aliiachiwa madaktari wazalendo 2; na wahandisi wazalendo 12. Hospitali kubwa zote zilikuwa za misheni, sehemu nyingi hakukuwa na kliniki wala vituo vya maana vya afya. Hatujazungumzia manesi n.k. Hapa pia hatujazungumzia hali ya elimu ilivyokuwa; hatujazungumzia barabara, nishati, n.k

Sijui ndugu zetu walitaka Nyerere ajenge mahospitali ya kimataifa yenye huduma za juu at the expense of what? Kwa uchumi na utaalamu gani aliokuwa nao?

KUjaribu kulinganisha juhudi za kipekee za Baba wa Taifa kuinua huduma ya afya halafu kuzipuuza ni kutomtendea haki katika ukweli. Angejenga mahospitali ya kisasa ambao viongozi ndio wangekuwa wanahudumiwa zaidi huku wananchi wengi wakipata huduma duni watu wangesema vingine. Lakini angeweza vipi kujenga mahospitali ya kisasa ya kuhudumia magonjwa ya aina zote duniani kwenye nchi iliyoachwa maskini na wakoloni? It just doesn't make sense.

Hiyo hospitali ya Medi-Clinic ya Pretoria ambapo Mandela alipelekwa siyo ya serikali; ni ya binafsi. Sasa sijui kwa namna gani Mandela anasifiwa kwa kuboresha huduma zake hadi kuchagua kwenda hapo? Kwanini asingepelekwa kwenye hospitali ya serikali kuonesha uzalendo wake? Na ndugu zetu hawa wanashindwa kujua au kutambua pia kuwa hospitali hiyo ni sehemu ya mtandao wa kimataifa wa hospitali za Medi-Clinic ambazo zina hospitali nchi mbalimbali duniani na kutengeneza mfumo wa hospitali ambazo ni wa 6 kwa ukubwa duniani.

Ndio maana I call this one of the most irrational and profoundly absurd argument ever attempted. It is an emotional argument more than anything.
 
Ni furaha kuona kwamba baba wa taifa anafia nyumbani kwake. Nchi zetu hizi viongozi wetu wanafia ulaya, India, S. Africa.

Kwa Mandela hiyo ni ishara ya nchi iliyo timamu. Iliyojengwa Kuwa nchi badala ya kujiandaa kuomba omba. Tusubiri msafara wa mazishi.

Nelson Mandela ana kila sababu za kutofia India au Uingereza kwa sababu nchi aliyoijenga haina tofauti kabisa na nchi yoyote ya dunia yakwanza, south Afrika ni kama ulaya tu.

Maskini kama Tz ndio hatutibiwi kwetu tunakimbilia nnje kwa kuwa tunajua kuwa Muhimbili ni hospitali kanjanja,
.
Mungu bariki Mandela
 
Nelson Mandela ana kila sababu za kutofia India au Uingereza kwa sababu nchi aliyoijenga haina tofauti kabisa na nchi yoyote ya dunia yakwanza, south Afrika ni kama ulaya tu.

Maskini kama Tz ndio hatutibiwi kwetu tunakimbilia nnje kwa kuwa tunajua kuwa Muhimbili ni hospitali kanjanja,
.
Mungu bariki Mandela

NA unaamini kabisa kuwa Mandela Ndio kaijenga Africa ya kusini kwa miaka mitano ya utawala wake?
 
Umemwambia vizuri mwisho unaanza kumrembaremba.
Nilichotaka ni kumwambia ukweli ambao ndio nilioelekeza mpaka mstari wa mwisho, sikuwa na nia ya kumkandia bali kumpa changamoto.
 
Ndio maana nasema tumejenga taifa la watu wasiojua kufikiri vizuri; wanafikiri wanajenga hoja kumbe wanatengeneza absurdities zisizo za lazima kabisa. Unamsifia Mandela kwa kufia nyumbani kwake - well kwa juu juu watu wanaweza kuona umesema kitu lakini kwa kweli ni an irrational argument. Kwani huduma za afya za Afrika ya Kusini zilijengwa na Mandela?

Hoja ya kusema kuweka posho na marupurupu kwenda nje hiyo nakubaliana na wewe kabisa. Lakini si watu hawa hawa wamechaguliwa na sisi na tunajua kuwa tunapowachagua tumewapa na hilo vile vile? Kama suala ni taifa kulipia viongozi kwenda kutibiwa nje hiyo ni hoja nyingine kabisa; lakini kama kiongozi ana fedha zake na kwa uwezo wake kwanini asiende kutibiwa nje? Kama mauti yakamkuta huko nje kwanini anaonekane si mzalendo? Kwani anayekufa ulaya na anayekufa Maneromango yupi anakuwa amekufa sana?

It is silly argument. Ukitaka kuzungumzia suala la kugharimia matibabu ya viongozi nje lete hiyo hoja.

Hivi kuna kufikiri vizuri na kufikiri vibaya ktk dunia hii? Wote tunafikiri basi!
Unaweza kufikiri mazuri au mabaya. Tatizo la mwanakijiji imekuwa ni kuteka nyara mawazo. Kwa nini unalazimisha tuzungumzie matibabu ya nje au ndani ya nchi. Hayo yanaeleweka na tulishajadili miaka mingi hapa JF. Kwa nini uite hoja isiyokuwepo? ukitaka ita wewe mwenyewe. Haya tunayoyazungumzia hapa ni matokeo yake, kwamba tangu miaka miwili au mitatu iliyopita Mandela amelelewa kwa huduma za nyumbani. Namaanisha Afrika kusini na siyo ndani ya nyumba.

Mandela hakuzijenga hizo Hospitali lakini pia hakuziharibu. Kwani Zimbabwe bado zipo? Sasa wewe ita silly, stupid, absurdities, n.k. ukweli unabaki pale pale kwamba kama wewe pia unawaza kwamba siku rais wetu akizidiwa basi maisha yake yaokolewe Apollo kwa hela zake unazosema, binafsi nitaendelea kuita ni ushenzi. huhitaji kunishawishi.

Kwa kumsifia Mandela Kufia nyumbani hatuna maana ya ile ya kitanzania kwamba amekufa kishujaa, binafsi naiona sifa ya mtu kutohitaji kubebwa hadi nchi nyingine ili kuokoa afya yako! kama umuhimu huo huuoni hilo siyo tatizo langu maana unaanza kuonyesha eti kiongozi akiwa na hela zake. Zipi na lini uliona nchi yetu kiongozi akitumia hela zake!
 
..............................................

Inaonesha ndugu zetu hata historia yetu ya nchi hawaijui au wameisahau. Baada ya miaka zaidi ya 40 ya ukoloni wakati wa Uhuru Nyerere aliiachiwa madaktari wazalendo 2; na wahandisi wazalendo 12. Hospitali kubwa zote zilikuwa za misheni, sehemu nyingi hakukuwa na kliniki wala vituo vya maana vya afya. Hatujazungumzia manesi n.k. Hapa pia hatujazungumzia hali ya elimu ilivyokuwa; hatujazungumzia barabara, nishati, n.k .

Binafsi ninaishi leo. Sihitaji kufundishwa historia ili imutetee mtu wa leo. Ukiniruhusu nitafute ubaya wa Yesu au Mtume Mohamad s.a.w. nitajaza ukurasa. Nikitafuta mazuri pia ni mengi sana. Wewe umeamua kuwinda uzuri wa Nyerere, sawa!

Niambie tangu Uhuru tumejenga hospitali ipi hapa TZ? Nasema Hospitali, ni ipi hiyo? Ninachokiona leo hii ni ushuhuda wa Ofisi kubwa za Chama zilizojengwa baada ya uhuru. Kila mkoa uliokuwepo ulijengewa gorofa kwa sifa.

Kusimulia historia iwe kinga ya uzembe uliokwishafanyika, ni ubabaishaji wa aina nyingine. Sipendi mtu anayeturudisha nyuma tusikojua kila wakati ili tuone umbali aliotembea. twambie umefika wapi? Mbona kuna nchi zimefika mbali bila kujali historia mbaya kama hiyo.
 
Back
Top Bottom