Mandela anakuzwa kuliko anavyostahili?

Mandela anakuzwa kuliko anavyostahili?

Synthesizer

Platinum Member
Joined
Feb 15, 2010
Posts
15,157
Reaction score
28,766
Namheshimu sana Mandela, lakini nimekuwa nikijiuliza sana, hivi ni nini hasa kinachofanya Mandela akuzwe sana duniani? Mara nyingi naona Mandela amekuzwa kulikoanavyostahili. Hivi ni lipi hasa la ajabu sana alilowafanyia Wa-South Africa,kuwapa uraisi wa mtu mweusi? Kwanza hata hayo mazungumzo ya kupata raisi mweusiAfrika Kusini Mandela hakushiriki kiasi hicho, walishiriki wengine.

Hebu linganisha Nyerere na Mandela katika kuchangia ukombozi wa demokrasia Afrika Kusini. Maoni yangu ni kwamba Nyerere alikuwa na mchango mkubwa kwa ukombozi wa Afrika Kusini kuliko hataMandela. Kumbuka Nyerere ndie aliyewashawishi ANC na wengineo AfrikaKusini wafanye mazungumzo na Makaburu, mazungumzo yaliyozaa demokrasia Afrika Kusini.In fact baadhi ya ANC walimtukana Nyerere alipowaambia wakae na kuzungumza naMakaburu. Kumbuka pia Nyerere ndiye alieanzisha kampeni iliyoitwa "boycottSouth Africa" kwa kampuni za kimataifa kutofanya biashara na Afrika kusiniya Makaburu.

Nyerere huyo huyo ndie aliyesababisha Afrika Kusini iondolewe kwenyeCommonwealth, jambo ambalo Makaburu waliona ni pigo kubwa sana. Nyerere ndiealiyetoa ardhi kwa kambi za ukombozi wa kusini mwa Afrika ili eneo lote lakusini likombolewe, kutia ndani kambi za wapigania uhuru za ANC, PAC (SouthAfrica), FRELIMO (Msumbiji), SWAPO (Namibia), ZAPU, ZANU-PF (Zimbabwe) na MPLA(Angola). Nyerere alikuwa akitoa ndege kwenda kuwatorosha wapigania uhuru tokaSouth Afrika, ambapo kuna ndege moja ya East African Airways ililipuliwa ikiwakwenye hiyo mission. Nyerere ndiye alikuwa mstari wa mbele kuzuia mataifa ya nje kuwauzia Makaburu silaha akisema silaha hizo zilitumika dhidi ya watu weusi.

Halafu Mandela huyu, ziara zake za kwanza baada ya Afrika kusini kupata uhuruhaikuwa kuzitembelea nchi zilizoisaidia Afrika Kusini kupata demokrasia, balialienda Ulaya. Alipotaka kufanya ziara ya pili Ulaya kabla ya kuzitembelea nchizilizowasaidia alikataliwa na baadhi ya watu ndani ya ANC. Mandela alidai etianaenda Ulaya kuwaelimisha kwa nini ilikuwa muhimu yeye aachiwe kwa sababu nchikama Uingereza na Marekani waliwashauri Makaburu wasimwachie huru.

Suala la msamaha kwa yale Makaburu waliyowafanyia Wazalendo halikuwa laMandela, bali sehemu ya makubaliano katika mazungumzo kati ya Makaburu na ANC.

Basi hadi leo nashindwa kuelewa ni nini hasa kinachofanya Mandela akuzwe kiasihiki. Kwa sababu alifungwa? Mbona wapo wengi tu waliofungwa nae hatusikiiwakivuma kama Mandela?

Binafsi hata huwa inanisikitisha na kuniuma sana kwamba South Afrika huwa haionyeshi appreciation kamili kwa mchango alioufanya Nyerere kwa ukombozi wa nchi yao. Leo hii vijana wa South Afrika hawamjui Nyerere, wanajua uhuru wao uliletwa na Mandela tu. Nasikia kuna barabara pale Durban inaitwa Nyerere, kweli hiyo ndiyo shukurani ya Afrika Kusini kwa Nyerere? Tanzania tunaonekana kumuenzi Mandela mara nyingi zaidi ya South Afrika wanavyomuenzi Nyerere, tumetoa majina ya Mandela kwa barabara muhimu, viwanja nk, kama vile wao ndio waliotusaidia sisi. Kwa nini? Nasikitika sana. Kweli tenda wema uende zako.

 
Namheshimu sana Mandela, lakini nimekuwa nikijiuliza sana, hivi ni nini hasa kinachofanya Mandela akuzwe sana duniani? Mara nyingi naona Mandela amekuzwa kulikoanavyostahili. Hivi ni lipi hasa la ajabu sana alilowafanyia Wa-South Africa,kuwapa uraisi wa mtu mweusi? Kwanza hata hayo mazungumzo ya kupata raisi mweusiAfrika Kusini Mandela hakushiriki kiasi hicho, walishiriki wengine.

Hebu linganisha Nyerere na Mandela katika kuchangia ukombozi wa demokrasia Afrika Kusini. Maoni yangu ni kwamba Nyerere alikuwa na mchango mkubwa kwa ukombozi wa Afrika Kusini kuliko hataMandela. Kumbuka Nyerere ndie aliyewashawishi ANC na wengineo AfrikaKusini wafanye mazungumzo na Makaburu, mazungumzo yaliyozaa demokrasia Afrika Kusini.In fact baadhi ya ANC walimtukana Nyerere alipowaambia wakae na kuzungumza naMakaburu. Kumbuka pia Nyerere ndiye alieanzisha kampeni iliyoitwa "boycottSouth Africa" kwa kampuni za kimataifa kutofanya biashara na Afrika kusiniya Makaburu.

Nyerere huyo huyo ndie aliyesababisha Afrika Kusini iondolewe kwenyeCommonwealth, jambo ambalo Makaburu waliona ni pigo kubwa sana. Nyerere ndiealiyetoa ardhi kwa kambi za ukombozi wa kusini mwa Afrika ili eneo lote lakusini likombolewe, kutia ndani kambi za wapigania uhuru za ANC, PAC (SouthAfrica), FRELIMO (Msumbiji), SWAPO (Namibia), ZAPU, ZANU-PF (Zimbabwe) na MPLA(Angola). Nyerere alikuwa akitoa ndege kwenda kuwatorosha wapigania uhuru tokaSouth Afrika, ambapo kuna ndege moja ya East African Airways ililipuliwa ikiwakwenye hiyo mission. Nyerere ndiye alikuwa mstari wa mbele kuzuia mataifa ya nje kuwauzia Makaburu silaha akisema silaha hizo zilitumika dhidi ya watu weusi.

Halafu Mandela huyu, ziara zake za kwanza baada ya Afrika kusini kupata uhuruhaikuwa kuzitembelea nchi zilizoisaidia Afrika Kusini kupata demokrasia, balialienda Ulaya. Alipotaka kufanya ziara ya pili Ulaya kabla ya kuzitembelea nchizilizowasaidia alikataliwa na baadhi ya watu ndani ya ANC. Mandela alidai etianaenda Ulaya kuwaelimisha kwa nini ilikuwa muhimu yeye aachiwe kwa sababu nchikama Uingereza na Marekani waliwashauri Makaburu wasimwachie huru.

Suala la msamaha kwa yale Makaburu waliyowafanyia Wazalendo halikuwa laMandela, bali sehemu ya makubaliano katika mazungumzo kati ya Makaburu na ANC.

Basi hadi leo nashindwa kuelewa ni nini hasa kinachofanya Mandela akuzwe kiasihiki. Kwa sababu alifungwa? Mbona wapo wengi tu waliofungwa nae hatusikiiwakivuma kama Mandela?

Binafsi hata huwa inanisikitisha na kuniuma sana kwamba South Afrika huwa haionyeshi appreciation kamili kwa mchango alioufanya Nyerere kwa ukombozi wa nchi yao. Leo hii vijana wa South Afrika hawamjui Nyerere, wanajua uhuru wao uliletwa na Mandela tu. Nasikia kuna barabara pale Durban inaitwa Nyerere, kweli hiyo ndiyo shukurani ya Afrika Kusini kwa Nyerere? Tanzania tunaonekana kumuenzi Mandela mara nyingi zaidi ya South Afrika wanavyomuenzi Nyerere, tumetoa majina ya Mandela kwa barabara muhimu, viwanja nk, kama vile wao ndio waliotusaidia sisi. Kwa nini? Nasikitika sana. Kweli tenda wema uende zako.

PITIA FILAMU HII
[h=3]MOVIE REVIEW: ‘Mandela: Long Walk to Freedom'[/h]
 
Sifa kubwa ya mzee madiba ni kutokua na KINYONGO WALA UBAGUZI KTK SIASA
 
Namheshimu sana Mandela, lakini nimekuwa nikijiuliza sana, hivi ni nini hasa kinachofanya Mandela akuzwe sana duniani? Mara nyingi naona Mandela amekuzwa kulikoanavyostahili. Hivi ni lipi hasa la ajabu sana alilowafanyia Wa-South Africa,kuwapa uraisi wa mtu mweusi? Kwanza hata hayo mazungumzo ya kupata raisi mweusiAfrika Kusini Mandela hakushiriki kiasi hicho, walishiriki wengine.

Hebu linganisha Nyerere na Mandela katika kuchangia ukombozi wa demokrasia Afrika Kusini. Maoni yangu ni kwamba Nyerere alikuwa na mchango mkubwa kwa ukombozi wa Afrika Kusini kuliko hataMandela. Kumbuka Nyerere ndie aliyewashawishi ANC na wengineo AfrikaKusini wafanye mazungumzo na Makaburu, mazungumzo yaliyozaa demokrasia Afrika Kusini.In fact baadhi ya ANC walimtukana Nyerere alipowaambia wakae na kuzungumza naMakaburu. Kumbuka pia Nyerere ndiye alieanzisha kampeni iliyoitwa "boycottSouth Africa" kwa kampuni za kimataifa kutofanya biashara na Afrika kusiniya Makaburu.

Nyerere huyo huyo ndie aliyesababisha Afrika Kusini iondolewe kwenyeCommonwealth, jambo ambalo Makaburu waliona ni pigo kubwa sana. Nyerere ndiealiyetoa ardhi kwa kambi za ukombozi wa kusini mwa Afrika ili eneo lote lakusini likombolewe, kutia ndani kambi za wapigania uhuru za ANC, PAC (SouthAfrica), FRELIMO (Msumbiji), SWAPO (Namibia), ZAPU, ZANU-PF (Zimbabwe) na MPLA(Angola). Nyerere alikuwa akitoa ndege kwenda kuwatorosha wapigania uhuru tokaSouth Afrika, ambapo kuna ndege moja ya East African Airways ililipuliwa ikiwakwenye hiyo mission. Nyerere ndiye alikuwa mstari wa mbele kuzuia mataifa ya nje kuwauzia Makaburu silaha akisema silaha hizo zilitumika dhidi ya watu weusi.

Halafu Mandela huyu, ziara zake za kwanza baada ya Afrika kusini kupata uhuruhaikuwa kuzitembelea nchi zilizoisaidia Afrika Kusini kupata demokrasia, balialienda Ulaya. Alipotaka kufanya ziara ya pili Ulaya kabla ya kuzitembelea nchizilizowasaidia alikataliwa na baadhi ya watu ndani ya ANC. Mandela alidai etianaenda Ulaya kuwaelimisha kwa nini ilikuwa muhimu yeye aachiwe kwa sababu nchikama Uingereza na Marekani waliwashauri Makaburu wasimwachie huru.

Suala la msamaha kwa yale Makaburu waliyowafanyia Wazalendo halikuwa laMandela, bali sehemu ya makubaliano katika mazungumzo kati ya Makaburu na ANC.

Basi hadi leo nashindwa kuelewa ni nini hasa kinachofanya Mandela akuzwe kiasihiki. Kwa sababu alifungwa? Mbona wapo wengi tu waliofungwa nae hatusikiiwakivuma kama Mandela?

Binafsi hata huwa inanisikitisha na kuniuma sana kwamba South Afrika huwa haionyeshi appreciation kamili kwa mchango alioufanya Nyerere kwa ukombozi wa nchi yao. Leo hii vijana wa South Afrika hawamjui Nyerere, wanajua uhuru wao uliletwa na Mandela tu. Nasikia kuna barabara pale Durban inaitwa Nyerere, kweli hiyo ndiyo shukurani ya Afrika Kusini kwa Nyerere? Tanzania tunaonekana kumuenzi Mandela mara nyingi zaidi ya South Afrika wanavyomuenzi Nyerere, tumetoa majina ya Mandela kwa barabara muhimu, viwanja nk, kama vile wao ndio waliotusaidia sisi. Kwa nini? Nasikitika sana. Kweli tenda wema uende zako.

Habari hii aisome kiwatengu.
 
Last edited by a moderator:
mandela alijenga nyumba million 3 kwa raia wake kipind yuko madarakan wako kajenga ngap?

mandela pamoja na kukaa jela kwa miaka 27 kutokana na harakat zake za uhuru lakin ata alivyotoka akawasamehe makaburu na wengine ni mawaziri. je rais wako angesamehe?

mandela hakuwa fisadi na alikuwa mzalendo.je rais wako siyo fisadi?
 
Unaumia sehemu? aliyekuzidi kakuzidi tu mwache apumzike amekula chumvi sana....
 
mandela alijenga nyumba million 3 kwa raia wake kipind yuko madarakan wako kajenga ngap?

mandela pamoja na kukaa jela kwa miaka 27 kutokana na harakat zake za uhuru lakin ata alivyotoka akawasamehe makaburu na wengine ni mawaziri. je rais wako angesamehe?

mandela hakuwa fisadi na alikuwa mzalendo.je rais wako siyo fisadi?

So, what you mean Mwl alikuwa fisadi pia, huh!!??
 
Mleta maada, Madiba angetaka angetoka jela mwanzoni tu mwa miaka ya 70. Kumbuka kuwa binamu yake ndie aliekuwa "kiongozi" wa Transkei na Botha alishamshawishi sana Mandela autambue "utawala" wa Transkei ili amuachie huru. Lakini mzee Mandela aligoma katakata.

Huwezi kutenganisha mwisho wa ubaguzi wa rangi South Africa na Mzee Mandela.
 
acheni wivu wa kiliberal. mwachen mandela amefanya mengi kwa Taifa lake na Africa kuliko kiongoz yoyote Africa.

we sio mzima mandela amefanya nn kwa afrika??? mandela hamfikii hata robo ya mchango wa nyerere kwa ukomboz wa bara hili!!!
 
In my opinion, soma kitabu cha "long walk to freedom" by Nelson Mandela!
Hapo utaona mchango wa mandela katika ukomboz wa S.A and kwa nn anaheshimika!...
On the other side, naamini kuwa nyerere alikua na mchango mkubwa sana katika ukomboz wa AFRICA, n kama unafuatilia mambo na kusoma articles mbalimbali huwez kataa hili!...
N sio kwamba MANDELA anaheshmika zaid ya nyerere BUT kwa sababu he is alive ni rahis kumzungumzia yeye kuliko NYERERE, NKURUMAH na wengne wenggi katka historia ambao wametangulia mbele ya haki!

Sent from my BlackBerry 9780 using JamiiForums
 
mandela alijenga nyumba million 3 kwa raia wake kipind yuko madarakan wako kajenga ngap?

mandela pamoja na kukaa jela kwa miaka 27 kutokana na harakat zake za uhuru lakin ata alivyotoka akawasamehe makaburu na wengine ni mawaziri. je rais wako angesamehe?

mandela hakuwa fisadi na alikuwa mzalendo.je rais wako siyo fisadi?

Ujenzi wa nyumba kwa wananchi masikini ni programu iliyoamuliwa na ANC kama chama, sio Mandela (ANC Reconstruction Program, RDP; to tackle*violence * Iack of housing * Iack of jobs * inadequate education and health care * Iack of democracy * a failing economy). Na si kweli kwamba Mandela aliwasamehe wahalifu Makaburu kama nilivyosema kwenye thread, hayo yalikuwa ni makubaliano wakati wa mazungumzo ya uhuru. Kumbuka Makaburu walidai kuwa hata askari wa ANC waliua raia kutia ndani watoto na wanawake wasio na hatia katika kile walichoita mapambano ya uhuru, wakivamia wakulima na kuchinja familia yote. Je huo ndio upigania uhuru?

Makubaliano ilikuwa kwamba kwamba Truth Renconciliation Commission (TRC) chini ya Desmond Tutu ndio ingeamua nani asamehewe na nani afungwe. Sio Mandela. Wale ambao hawakujitokeza kukiri makosa yao kwa TRC walitakiwa washitakiwe. Sasa suala la Mandela kusamehe Makaburu linaingiaje hapa?
 
Ukipenda kupunguza msongo we mleta mada usipende kulinganisha watu, kila mtu na strength na weakeness. So kama unataka kudiscuss ukuu wa Mandela usilinganishe na Nyerere, kila mtu ana umuhimu wake kwa watu wake. Ukipata baba wa hiari akakusaidia sana kwasababu baba yako wakati huo amehitaji msaada, utamheshimu zaidi kuliko baba yako?kama unafanya comperative analysis labda!
 
Unafananisha Nyerere na Mandela.
 
Sasa ndo ili iwe nini? Haya Nyerere anaheshimika zaidi ya Mandela, So what? Wazee walifanya kazi yao nasi tujikite kufanya yetu tuendeleze Afrika yetu. KWISHA.
 
we sio mzima mandela amefanya nn kwa afrika??? mandela hamfikii hata robo ya mchango wa nyerere kwa ukomboz wa bara hili!!!
Leo kweli ni siku yangu ya kushangaa!si ndio nyie kila siku mnamponda Julius K N,leo imekuaje mnatamani na kutaka awe mkubwa kuliko madiba?
 
Kujitoa kwaajili ya watu wake tu kunatosha kumpa sifa azipatazo achilia mbali mengi aliyoyafanya, infact Nyerere na Mandela kila mmoja ana mchango wake mkubwa kwa Africa na hata ndani ya nchi zote mbili kwa ujumla.
27 years ndani for the country and the people is more than enough.
Kulinganisha sifa kati ya Nyerere na Mandela is nothing, what matters now, ni kuunganisha matendo yao mema kufanya.
I LOVE YOU VERY MUCH MANDELA.
 
Back
Top Bottom