Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Nipo hoi

Siku glazers watakapobwaga manyanga na ndio mikosi yote itaondoka pale traford
Hali tete sana Mkuu..

Na hawa jamaa nadhani bado wapo wapo..

Lakini walau kwa sasa mwanga utaonekana kama Jim ayasemayo atayasimamia haijalishi ugumu na changamoto atakazopitia..

Mpira ni Sayansi na Sanaa kwa wakati Mmoja..

Njia sahihi
Watu sahihi(kila idara)

Matokeo yanakuja yenyewe..

Muda utakuwa mfupi maamzi magumu yakifanyika
Muda utakuwa mrefu kiasi maamzi magumu yakichelewa..

Kocha ni wa kawaida(Bahati mbaya dunia haina tena mafundi wengi)..Ten Hag, Graham Potter, daraja moja tu hilo..

Ila kitu hatuna zaidi ni wachezaji..

Namtoa ;
Rasmus
Kobbie
Daraja A..

Onana
Alejandro
Lisandro
Dalot
Shaw
Bruno
Daraja B..

Waliobaki kwa kuongeza ukubwa wa timu, matumizi baadhi ya mechi mtego
Scott
Wan Bissaka..

Hawa kina
Antony
Harry
Casemiro
Varane
Victor
Mount
Rashford
Sancho and co

Wawapunguze tu..

Natumai tutatejea na tutabeba mataji tena kwa mwendelezo..
Lakini hadi hiyo siku ije kuna fagio lazima lipite..

Mshindi huwa hakubali kushindwa..
Hapa ndio ninapompa Pep(EXCELLENT)
 
Manchester United sio timu ya mchezaji kwenda kujitafuta kama kule kwingineko..

Machaguo ni ucheze kwa kiwango ama uondoke..

Miaka hii watu wanajitafuta anaua mkataba wa kwanza anapewa mwingine ajitafute tena..

Huu ni utovu wa nidhamu na maadili kwa viongozi na wachezaji...

Ni kweli kwamba kuna wakati mambo hukataa..
Coutinho-->Barcelona
Griezman -->Barcelona
Mane-->Bavaria
Kaka-->Madrid
na wengine wengii..

Sio kina Amrabat
Kina Mount
Kina Anthony..

Aliesign zile pesa za Anthony natumai ni Kipanga sana..
Mchezaji wa kawaida Uholanzi aje akimbize EPL??
Inawezekana ila kwa juhudi na mazingira bora sana..
 
Ngolo Kante anayecheza saudia arabia ni bora zaidi kuliko casemiro wa msimu huu.

Hili zee benzema hatuwezi kulichukua japo kwa miaka miwili?

Bado lipo fiti kuliko jackson
Hapana Man United wachezaji wanaflop kutokana na mfumo wa mwalimu.

Casemiro analazimika kulinda zaidi ya nusu ya uwanja peke yake.

Kila baada ya sekunde 45 wachezaji wa Man U wanalazimika kukimbia kutoka kwenye final third ya mpinzani kumuokoa Onana.
 
INEOS wasipofanya operesheni ya moyo hawatofika mbali.

  • Eriksen mwili wake hautaki tena kugombania mpira.
  • Tukubali makosa ya kusajiliwa wan bissaka, level yake ni crystal palace.
  • Varane bado ana kitu mguuni lakini mwili hautaki tena, majeruhi yasiokwisha huku akiramba mshahara mkubwa.
  • Kulipa millioni 60 paundi kwa casemiro mwenye miaka 30 kwenye dunia yenye ruben neves, palhinha ni kosa jengine la kutoipa umuhimu future.
  • Kwanini tulimsajili Onana ikiwa mfumo wetu wa uchezaji ni ule ule, tujiulize amekuja kuongeza nini, hapa kipara awajibike.
  • Tuache tabia ya kupapatikia wachezaji kwa hoja mfu, tuliwahi kukataa kumuuza lingard kwenda newcastle kwa hoja ya kumuimarisha adui, msimu huu klabu imekataa 30 millioni kwa scott mctominay, ni kichekesho.
  • Klabu ya mpira si hisani, luke shaw aonyeshwe mlango wa kutokea, amekosa mechi nyingi sana kwa hoja ya majeruhi na pia hana consistency.
  • Nguvu aliotumia kipara kumgombania amrabat hailingani na anachomfanyia, hapa tumelipa paundi millioni 10 kwa mkataba wa mwaka mmoja, kosa jengine la kipara.
  • Victor lindelof hawezi kuwa na miujiza na hatokuwa na miujiza.
Ni mchakato unaoweza kuchukua madirisha mawili makubwa ya usajili.
 
United itakuua
 
Unachosema hapa ni sawa sawa unamiliki duka la vipodozi, bidhaa nyingi zime-expire unaogopa kuziondoa zote kwenye mashelf kwa sababu duka litaonekana limefilisika.

Hivyo unaamua kuziacha. Baadhi unaziuza kwa kuwabambika wateja angalau urudishe mtaji wako, nyingine unazitupa kidogo kidogo.
 
Unachosema hapa ni sawa sawa unamiliki duka la vipodozi, bidhaa nyingi zime-expire unaogopa kuziondoa zote kwenye mashelf kwa sababu duka litaonekana nimefilisika.
Sisi ni tofauti na chelsea linapokuja swala la kuuza wachezaji (hatuna mvuto)
Tupo ovyo sana eneo hilo ndio maana nimeweka madirisha mawili ya usajili.

Vile vile hatuna nguvu ya kureplace wachezaji 10 kwa mkupuo kwa sababu sisi hatufanani na Yanga au Simba.
 
Ukiondoa Simba na Kaizer Chiefs Man United ndiyo timu inaendeshwa hovyo zaidi duniani kwa vilabu vikubwa.

Wachezaji walioko United hawawezi kuwa sehemu ya kikosi chochote cha vilabu vikubwa Uingereza,Spain au Bundesliga.

Tuna idadi kubwa ya wachezaji wanaopaswa kuhamia Serie A.
 
Open heart surgery ya Ralf ilikuwa na maana kubwa sana kama ingezingatiwa tungekuwa tulishaondoa.
Lindelof, Shaw, Fred, Bissaka, Antony, Brandon, Eriksen, Varane, na Martial. Kwa dirisha moja tu.
 
Leo hio tuko na Nottingham Forest halafu ukuta wa Berlin Harry Maguire atakosekana uwanjani huku Bruno na Varane hakuna uhakika kama watakuwepo.
Hofu yangu ni Forest kuondoka na Clean sheet maana timu inaingia uwanjani bila ya uwepo wa goal scorers muhimu Hojlund na Maguire.
Kama vile nawaona kina Awoniyi, Elanga, Hudson-Odoi na Morgan Gibbs White wanavyochekelea

Halafu jumapili tuko na Man City yaani mpaka tuseme Baba ubaya pale Carrington hua anafundisha Rugby au rede.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…