Bayern vs man u, game ilikua tofauti sana na watu walivyofikiria
Dakika 15-20 za mwanzo man u aliishika vizuri kabisa game.
Ata Bayern walipopata rhymes yao, still man u walikua bado wapo mchezoni
4-3
Ina maana Bayern alikua anafungika vizuri tu
Rashford anakosa sifa za kuitwa mchezaji mkubwa kwasababu ana mapepe Sana, na anachosahau kwa Sasa yeye ndio wakuibeba timu katika mechi Kama hizi
Kiungo ya man u, inakata Moto mapema sana, sababu ni umri
Mentality ya wachezaji ipo chini, hii inawafanya team kuwa underdog mchezoni
Pundits wangekuwa wanaenda mazoezini kutoa hamasa na sio kuishambulia timu kwenye media ingekua vizuri sana
Ten hag angemaliza tofauti zake na Sancho, asimame Kama baba, mtoto akinyea mkono hatuukati
Kuna uwezekano mkubwa Antony, amrabat, Sancho, mount, maino wangekuwepo Jana Mambo yangekua tofauti
Ndio maana shabiki wa man u aliesema Hawa wakija OT hawatoki, nilimuelewa Sana
Man u wamekosa nafasi nyingi, na wameshindwa kuzitumia nafasi nyingi kuliko hayo makosa ya Onana
Timu yenu inahitaji vitu viatau: utulivu, morali iwe juu, strong mentality
Kama unafatilia mpira vizuri, ni rahisi man u ku-bounce back kuliko chelsea
Bayern anakikosi kizuri wanakosa chemistry nzuri
Au wanakikosi Cha kawawaida lakini wanacheza kwa amsha-amsha tu
Au mentality ya kuwa timu kubwa bado wanaitumia vizuri
Ile Bayern akicheza na Brighton, anakufa vizuri tu