Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Ile mikimbio ya Mauntiiiii...
 

sasa unadhani hao key player wakati wanauzwa kocha alikuwa hawahitaji?

nadhani nafasi ya kocha katika kuleta na kuondoa wachezaji ni ndogo sana kwa sababu pamoja na kutoa mapendekezo yake,bado itategemeana na uwezo wa kiuchumi wa timu.

na pia hata ukisema awaondoe wachezaji bado ni ngumu kwa sababu inapaswa kuwalipa kuvunja mikataba yao kitu ambacho kipo nje ya uwezo wake.

na kama ulivyosema mafanikio ya ajax yalisaidiwa sana na yule sporting director aliyejiuzuru, basi mwenye nafasi hiyo pale man utd ndo anapwaya.

sioni sababu ya kumlaum kocha hapa japo ndio anabebeshwa lawama.
 
Haya unayosema Mimi nimeyasema miezi karibu minne iliyopita

Ten hag last season alibebwa na form ya Rashford na juhudi za Degea

Kama Rashford hatarejea kiwango chake Cha mwaka Jana Basi mtaiona sura halisi ya Ten hag
 
United pia inahitaji watu wawili eneo la ushambuliaji wanaolijua goli haswa tuone tuone atacholeta Hojlund ila hatoshi kwa sababu hatafunga kila mechi so partner wake pale mbele lazima afunge hilo silioni kwa Antony na Rashford.

Nadhani Greenwood akirudi akiwa fiti physical & mentally tunaweza tukawa na watu wawili wa kuwategemea huku Rashford naye akizingua taratibu Garnacho anadevelop na kwa umri wao na potential tunaweza kuona kitu kizuri baadae kwenye utatu wa Garnacho-Hojlund-Greenwood

Hapa eneo la kiungo linahitaji rebuild Casemiro muda wa kula pensheni umefika ila kwa msimu huu aletwe partner wake leo nimeona tetesi za Veratti japo sijawahi kumfuatilia uwezo wake.
 
Mi nakuuliza tu, captain wako huwa analalamika nini hasa? Kila wakati akionyeshwa huwa ni kulalamika tu.
Kulalamika kwake kushawahi kufuta goli tulilofungwa pia kushawahi kutupa goli letu lililokataliwa,ishu ni timing.

Kwangu hizo ni charms sio kuwa na jitu limezubaa kama Maguire hata moment of unfair linajitenga mbali kabisa
 
Hivi tuna uhakika aliyecheza jana na Spurs ni Man Utd na sio Kitayose Fc?
Shabiki wa kweli wa Man Utd unatakiwa ubishane mpk mwisho kua jana Utd haikua uwanjani, tunachojua sisi timu yetu inacheza tarehe 26Aug dhidi ya Nottingham Forest.



Poor Rashidi.
 
Huyu jamaa anasubiri aanze kutukanwa matusi ya kibaguzi tena aanze kutafuta huruma kwa mashabiki round hii sijui atasema ana jeraha gani!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…