Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Bora hata wewe unaelewa kuliko wenzio🤣🤣🤣
 
WAMEBANDULIWA SABA

© Dr Beatus Chikoti

1.
Ligi soka zinasonga,
siku zaenda si haba
ni ndefu kama mkonga,
wapambana majibaba
kileleni wapo sawa,
wanazimimina shaba
Mashetani wameloa,
wamebanduliwa saba.

2.
Watu wanajiuliza,
kwani ndiyo nini saba
nami nipo kuwajuza,
maana hasa ya saba
hadi watapojifunza,
na kuifahamu namba
Mashetani wameloa,
wamebanduliwa saba.

3.
Kwa bashasha nawajibu,
sakramenti ni saba
jitafutieni jibu,
juma lina siku saba
Mrema aliadhibu,
baada ya siku saba
Mashetani wameloa,
wamebanduliwa saba.

4.
Bado niko kanisani,
mapaji nayo ni saba
ukizama najisini,
utakaso siku saba
Msamaha wa sabini,
kigawo chake ni saba
Mashetani wameloa,
wamebanduliwa saba.

5.
TANU ilipozaliwa,
ilikuwa saba saba
Mwalimu alitwaliwa,
umri sabina saba
Karume aliuliwa,
siku ya tarehe saba
Mashetani wameloa,
wamebanduliwa saba.

6.
Maajabu ya dunia,
yale ya kale ni saba
Na kule kwa malkia,
shetani kaloa saba
Liva wanajivunia,
kumpata mahabuba
Mashetani wameloa,
wamebanduliwa saba.

7.
Imekuwa siku njema,
kenge kupigwa kiroba
Na sasa wamechutama,
kuugulia shuruba
Jina lao linasoma,
ni soda ya juu saba
Mashetani wameloa,
wamebanduliwa saba.
 
🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣
 
Sure kilichomuua Ten Hag ilikuwa ni kutowaheshimu Liverpool, umeshapigwa tatu na bado umezidiwa kwenye kila eneo halafu unatoa Fred unaingiza Garnacho.

Unprofessionalism ya hali ya juu.
 
Sasa mbona unataka kusajili wachezaji zaidi ya watano idadi kubwa kuliko niliyoweka hapo ?
 
Sure kilichomuua Ten Hag ilikuwa ni kutowaheshimu Liverpool, umeshapigwa tatu na bado umezidiwa kwenye kila eneo halafu unatoa Fred unaingiza Garnacho.

Unprofessionalism ya hali ya juu.
Unamweka benchi Wan Bissaka unamchezesha Dallot. Scholes hajamumunya maneno kasema wazi huyu Dallot na Weghorst hawana quality ya kucheza utd. ETH Kajifunza kitu jana kuhusu mechi kubwa ugenini hasa kwenye EPL! Asipobadilika atafata mkondo ule ule wa waliomtangulia
 
Hivi Weghost ana goli ngapi kwenye ligi?

Nataka ni compare na stats zake za magoli 2 ndani ya mechi 20+ akiwa Burnley.
 
Wenye matumain na ten hag atawafikisha nchi ya ahad ,siwaelewi
 
Dah walilinda pride anyway tumejifunza
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…