🤣🤣🤣🤣ameamka kwani?Dalot ana wasalimia
Bora hata wewe unaelewa kuliko wenzio🤣🤣🤣Ingawa 7 ni nyingi lakini bado zinatoa point tatu kama anayeshinda 1-0 tu. Arsenal,man city,liverpool,n.k zimeshinda kwao nasi tumeshinda kwetu.
Mtizamo wa kwanza kabisa kwa EtH ilikuwa kufahamu anaenda kucheza away kwa Liverpool ili achukue tahadhali ya kutosha kwa maana ya kupata walau droo tu. Matokeo ya arsenal kwao na City kwao yalitosha kumwambia timu huwa na sura tofauti kwenye uwanja wa nyumbani maana hii ni EPL na sio Eredisie ambapo Ajax anashinda popote anapotaka kwa idadi ya magoli anayotaka.
Rotation ya wachezaji imekua ni shida kubwa sana hasa nafasi za ushambuliaji na kiungo. Mfano mzuri ni Bruno,amekuwa hapumzishwi mechi hadi mechi matokeo yake jana alikuwa anapiga pasi kama amejikwaa vile. Hii wengi wetu tutasema sababu ya kikosi kidogo lakini kuna mechi walau dakika 10-15 za mwisho weka wale madogo wa akademi wakajaribu kutushangaza pia.
Pamoja na kwamba ratiba imechangia sisi kufungwa kwenye hii mechi kwa 50%,ila fomu yetu nzuri ya ushindi imepelekea sisi kupoteza hii game kirahisi na kwa kudhalilika hivi. Tangu mwanzo wa mechi Peter Drury anasema De gea anaonyesha kuanza kupoteza muda ndani ya dakika 10 za mwanzo. Kwamba Man utd walijua watulize presha ya liverpool mwanzoni halafu muda wao wa kushinda mechi utafika wakati wowote. Hii kujiaminia muendelezo mzuri ukafanya tufungwe maana tuliamini bahati bado iko upande wetu siku zote.
Conversion rate ya Rashford inatia huzuni sana. Ana rekodi nzuri siku za hivi karibuni ila bado inategemeana ameamkaje siku ya mechi ili kukupa kiwango stahiki. Tunamhitaji striker wa maana kama msimu ujao tunataka kupambania ndoo kubwa kubwa na wenzetu na wala sio kumtegemea Rashford kwa kazi ya kuzalisha magoli.
Lesson learned and we move forward.
GGMU.
🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣WAMEBANDULIWA SABA
© Dr Beatus Chikoti
1.
Ligi soka zinasonga,
siku zaenda si haba
ni ndefu kama mkonga,
wapambana majibaba
kileleni wapo sawa,
wanazimimina shaba
Mashetani wameloa,
wamebanduliwa saba.
2.
Watu wanajiuliza,
kwani ndiyo nini saba
nami nipo kuwajuza,
maana hasa ya saba
hadi watapojifunza,
na kuifahamu namba
Mashetani wameloa,
wamebanduliwa saba.
3.
Kwa bashasha nawajibu,
sakramenti ni saba
jitafutieni jibu,
juma lina siku saba
Mrema aliadhibu,
baada ya siku saba
Mashetani wameloa,
wamebanduliwa saba.
4.
Bado niko kanisani,
mapaji nayo ni saba
ukizama najisini,
utakaso siku saba
Msamaha wa sabini,
kigawo chake ni saba
Mashetani wameloa,
wamebanduliwa saba.
5.
TANU ilipozaliwa,
ilikuwa saba saba
Mwalimu alitwaliwa,
umri sabina saba
Karume aliuliwa,
siku ya tarehe saba
Mashetani wameloa,
wamebanduliwa saba.
6.
Maajabu ya dunia,
yale ya kale ni saba
Na kule kwa malkia,
shetani kaloa saba
Liva wanajivunia,
kumpata mahabuba
Mashetani wameloa,
wamebanduliwa saba.
7.
Imekuwa siku njema,
kenge kupigwa kiroba
Na sasa wamechutama,
kuugulia shuruba
Jina lao linasoma,
ni soda ya juu saba
Mashetani wameloa,
wamebanduliwa saba.
Tulia wewe matanga badoFabrice Hawkins, RMC]
Qatar bid for Manchester United is in pole position. INEOS have tabled another offer but Qatar are willing to go over £5b
Sure kilichomuua Ten Hag ilikuwa ni kutowaheshimu Liverpool, umeshapigwa tatu na bado umezidiwa kwenye kila eneo halafu unatoa Fred unaingiza Garnacho.Wakongwe kina Scholes wanasema enzi zao chini ya SAF walikua wakienda ugenini kwenye mechi kubwa wanacheza 4-5-1, lazima uheshimu timu kubwa huwezi force kwenda nao toe to toe. Wanaosema fatigue sikubaliani nao, shida ni choice of players na formation
Sasa mbona unataka kusajili wachezaji zaidi ya watano idadi kubwa kuliko niliyoweka hapo ?Mna sajili team nzima?
Liva inahitaji wachezaji wanne tu
RB kumpa challenge Trent,hapo atakuja Benjamin Heirinch wa Leipzig
Nahitaji beki wa kati kijana kucheza na Konate baadae,hapo atakuja Gvadiol wa Leipzig
Nahitaji mido 2 za maana sana hapo anakuja Belligham wa Dortmond na James Ward Prowse wa Southampton
Nakupiga 9-0 Sept
Unamweka benchi Wan Bissaka unamchezesha Dallot. Scholes hajamumunya maneno kasema wazi huyu Dallot na Weghorst hawana quality ya kucheza utd. ETH Kajifunza kitu jana kuhusu mechi kubwa ugenini hasa kwenye EPL! Asipobadilika atafata mkondo ule ule wa waliomtanguliaSure kilichomuua Ten Hag ilikuwa ni kutowaheshimu Liverpool, umeshapigwa tatu na bado umezidiwa kwenye kila eneo halafu unatoa Fred unaingiza Garnacho.
Unprofessionalism ya hali ya juu.
Hivi Weghost ana goli ngapi kwenye ligi?Unamweka benchi Wan Bissaka unamchezesha Dallot. Scholes hajamumunya maneno kasema wazi huyu Dallot na Weghorst hawana quality ya kucheza utd. ETH Kajifunza kitu jana kuhusu mechi kubwa ugenini hasa kwenye EPL! Asipobadilika atafata mkondo ule ule wa waliomtangulia
Wenye matumain na ten hag atawafikisha nchi ya ahad ,siwaelewiUnamweka benchi Wan Bissaka unamchezesha Dallot. Scholes hajamumunya maneno kasema wazi huyu Dallot na Weghorst hawana quality ya kucheza utd. ETH Kajifunza kitu jana kuhusu mechi kubwa ugenini hasa kwenye EPL! Asipobadilika atafata mkondo ule ule wa waliomtangulia
Ila Arteta atawafikisheni hiyo nchi ya ahadi?Wenye matumain na ten hag atawafikisha nchi ya ahad ,siwaelewi
Dah walilinda pride anyway tumejifunzaWakongwe kina Scholes wanasema enzi zao chini ya SAF walikua wakienda ugenini kwenye mechi kubwa wanacheza 4-5-1, lazima uheshimu timu kubwa huwezi force kwenda nao toe to toe. Wanaosema fatigue sikubaliani nao, shida ni choice of players na formation
Tulia wewe man7Ila Arteta atawafikisheni hiyo nchi ya ahadi?
Usimfananishe na Super Mikel na huyo ten hagIla Arteta atawafikisheni hiyo nchi ya ahadi?