Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Wewe ni kumer
Makidee haina haja ya matusi, humu tunataniana na kutambiana ili kunogosha tu ile ladha ya ushabiki.
Mtu yoyote anaetukana hovyo hua anaudhaifu fulani ambao hua anajaribu kuufichia kwenye kutukana, ila kinyume chake matusi hua yanauanika wazi huo upungufu mtu anaojaribu kuuficha.
Waungwana hua tunataniana, tunatambiana, tunakejeliana lakini sio kutukanana.
 
Manchester haiwezi kumsajili Osimhen kwanza bei yake tu ni kufuru.

Kama Napoli walimsajili kwa millioni 80 unadhani sasa hivi wanaweza kumwachia kwa pesa ndefu kiasi gani ?

Napoli hawawezi kumwachia chini 150-200.
Bei yake ni €115M. Hakutakuwa na ushindani sokoni majira ya kiangazi labda tusimtake. United ndio timu pekee inayoweza ku-afford gharama zake.

PSG wana Mbappe, City wana Halaand, Chelsea hawezi kufuzu UEFA msimu ujao - hivyo FFP itawabana kwenye usajili wa majira ya kiangazi. Madrid wanamlenga Bellingham lazima kibubu hapa kipasuke.
 
Yani nyiee!!😂😂😂

Ngoja nilale tu maana ya dunia mengi!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…