Mmeona sasa Malacia ni mtu zaidi ya shaw, Martinez nae anafanya shughuli ndio tunasema Ten Haag jivike mabomu tumia watu wako achana na waliofukuzisha makocha.
Ronaldo hizo ndizo dakika zake za kuingia kuwascare wapinzani
Leo nimekubali kocha kaja na mbinu. Aendelee hivyo hivyo ukiboroga benchi mpaka akili ikae sawia.
Diogo Dalot amepewa kisu ameambiwa leo jukumu lake ni moja tu la kumenya Kiazi.
Bruno ni katika kirusi ambacho mashabiki hawakizungumzii sana ila anaigharimu timu kwa kiwango kikubwa, anapoteza mipira sana na kujiangusha hovyo, inatakiwa atafutiwa hata timu ya mkopo aende akajinoe tena kama itashindikana kuuzwa.