Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Kipindi cha kwanza wamecheza vizuri vijana, kipindi cha pili kocha amuweke Eriksen mapema kwenye base ya midfield ili tuongeze ubunifu zaidi wa kwenda mbele
 
McTomminay hua nnamkubali kwa mashuti yake tu ya nje ya box.
Ila ana faulo za kijinga sana kisha analeta ubabe wake wa kipumbavu.
Masikitiko yangu makubwa ni pale mbele, kama ETH hataona umuhimu wa kusajili striker msimu huu basi tutapitia kwenye kipindi kigumu sana.
 
Kuna jambo moja linaniudhi sana unakuta Foul ya kawaida tu ila mtu anavyogalagala utafkr kakatwa mguu mbaya zaidi unakuta mpira ulikua ushafika lango la adui So unaamua kusimama...ivi awa wanaangaliaga game za Bundasliga hasa za bayern??

Jambo linalofanya bayern kumchukua mane nahisi moja ya sababu ni majeruhi yaani mpaka uje umuone mane injury ujue kaumia aswaa tena kaumia pakubwa tu ndo sasa wale kina Sengbe kwenye game zao unaweza kuona mtu kamkata rafu ila majamaa yanasonga tu...sasa ndomaana wakamvuta na mane kwenye fainali UCL kuna kiatu alipigwa na Carvajal nkasema uyu hanyanyuki ila mwamba akanyanyuka akaendelea kusakata kama kawa bayern inapenda sana wachezaji dizaini hii..


ila uku kina rashford,Elanga ukimgusa kidgo tu analala kusubiri atengewe foul Tabia inakera sana hii
 
wameregea wamekutana na wanaume hapa kazi haijaanza
 
martial,rashford,elanga na Mctominay wote miyayusho
 
Man united inafeli kutokana na ubishoo wa wachezaji, kujiangusha hovyo na kupenda kulalamika kwa refa ndio kitu inayonifanya nisimkubali kiviiile Bruno Fernandez, na huu upuuzi tayari ameshawaambukiza wachezaji wengi wa United.
Timu imejaa umama sana na kupenda kudekezwa hovyo.
 
naona kichapo ni cha muhimu kuliko tungeshinda tungejiona tunaingia kwenye ligi tupo bora kumbe amna kitu.

Nilichokiona mbele kwenye ufungaji bado tuna legalega nadhani imetukosti kufatana na sancho kukosekana pale mbele.

Ila bado wakuu tunaitaji sana strike pale mbele.
 
Dunia kwasasa haina CF

Kina Nunez wanaootea msimu mmoja unauziwa €100m

Yule Abraham aliyefukuzwa pale Chelsea bila €80m humpati


Unamtaka CF GANI?

Cr7 anawasumbueni
 
Huo Ubishoo ndo unaponza kwakweli Fred,MCtomminay na hata Cr7 wajitafakari hasira zao wasubiri mpira uishe Fred kakanyaga mtu vbaya sana na Red card juu...Felix analijua goli vizuri achana na foward zetu zinavyofeli pamoja na yote ERICKSEN ni MASHINE acha ETH azibe Ufa kesho kikosi kinabadilika pakubwa ngoja tuone itavyokua....
FT 0-1 goli ambalo uwezi kumlaumu beki yoyote coz mwanzo walipata chance nyingi sanaaa wakazichezea..ATM deserve a win ....mara ya mwisho kuwafunga ATM wema alikua bado bikra
 
Benni McCarthy will become a first-team coach for #mufc.
He speaks four languages and has been working as a manager in South Africa’s top division at Cape Town City and Amazulu.

AndyMitten

____________
ukitajiwa jina la benny mcCarthy kwa mshabiki wa manchester united unavuta kumbukumhu zako kwenye mchezo wa UEFA dhidi ya FC PORTO mnamo mwaka 2004.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…