Manchester United (Red Devils) | Special Thread

wachejazi wanakata upepo mapema sana, ningekuwa kocha, nafasi ya greenwood angekuwa anacheza elanga kuanzia mechi zijazo, yani dogo ana ubinafsi unaowafanya wenzake watoke mchezoni pale mbele, hebu fikiria dogo hakabi then nafasi chache zinazopatikana anashindwa kutoa pasi, anapiga kishuti mtoto, inatia hasira sana kucheza na mchezaji wa aina yake, huo ujinga anatakiwa kuufanya timu inaongoza hata goli nne bila sio kipindi timu inapambana kuteka mechi, this kid needs a harsh treatment mpaka akili imsogee
 
Waingereza wa Manchester United huwaambii kitu kuhusu wachezajii wao! Ni wabovu ila kutwa kuwavimbisha mibichwa.
 
Kuangalia mechi za Man Utd siku hizi inahitaji uwe na moyo mgumu

Timu zinakuja Old Trafford halafu zina dominate game na kutukimbiza mwanzo mwisho

Sijui ni mfumo wa kocha hauleweki, au kocha mwenyewe hafai au wachezaji hawakidhi vigezo vya kucheza Utd
 
Tatizo ni wachezaji, timu imekuwa kama Ac Milani inachukua wachezaji wazee
 
Tatizo ni kocha, System yake ya uchezaji.Wachezaji ni wale wale walio kochiwa na Carrick kabla ya kocha huyo Kutua.Mbona wakati wa Carrick walikuwa hawapotezi mipira?
 
Nikiangalia lists ya wachezaji walioachwa na josep guardiola pale kwa majirani miaka miwili ya mwanzoni ya utawala wake then uwalinganisha na hawa waliopo kwetu nabaki na mshangao dhidi ya wale wanaomnyooshea kidole mwalimu juu ya uwezo wake, hivi jurgen klopp alisafisha wachezaji wangapi mpaka alipojenga timu yenye kuogopesha.kwa timu kubwa mfumo ni wachezaji, Tuchel thomas alipata bahati ya mtende kwa kurithi timu iliokuwa na udhaifu wa kukosa nidhamu ya ushindi lakini kuhusu ubora wa wachezaji ulikuwepo kwa maeneo mengi ya uwanja.
 
nitajie hiyo mechi tafadhali nikaiangalie tena. Tusipende kujificha kwenye 4-2-2-2 isiotumika kwa kumuangushia lawama mwalimu.
Mwalimu Hana mbinu.Ana technique Moja tuu ambayo wanafunzi wameshindwa kuielewa yeye ana force tuu,Kocha asiforce aangalie na aina ya wachezaji alio nao.Kwanini Rb Leipzig walifit mfumo wake vizuri na Man UTD wanaonekana kuto kufit??? Kaangalie mechi za Leipzig wakati RR ni kocha,mipira ilikuwa haipotei potei ovyo,mpira safi unao vutia,mwendo wa kupress tuu.

Mechi za Carrick zilikuwa dhidi ya Villarreal Arsenal.
 
unataka abadilike vipi tena haliyakuwa kuna mechi tumecheza 4222, jana tumecheza 4231, mechi ya wolves tulicheza 442 na kipindi cha pili tukacheza na beki watatu, jukumu lililotekelezwa na matic.
 
Carrick hatetewi.Sema imetolewa mfano.Mbona Kwa mechi zake kadhaa na ya Sasa iliyopo Kulikuwa na tofauti??? Wewe hujiulizii??
ndio nikakuomba unitajie mechi tuliocheza vizuri, tulicheza na villareal, chelsea na arsenal. Nazungumzia performance na si matokeo. Ashukuriwe david de gea kwenye hizo mechi
 
ndio nikakuomba unitajie mechi tuliocheza vizuri, tulicheza na villareal, chelsea na arsenal. Nazungumzia performance na si matokeo. Ashukuriwe david de gea kwenye hizo mechi
Timu ilicheza vizuri na Villarreal kipindi Cha pili na Ilicheza vizuri dhidi ya Arsenal kipindi Cha pili,
 
Timu ilicheza vizuri na Villarreal kipindi Cha pili na Ilicheza vizuri dhidi ya Arsenal kipindi Cha pili,
baada ya kuwafunga goli la pili, mechi ya arsenal ilikuwa wazi kwa kila upande, kilichowagharimu ni kujilinda kwao baada ya kupata goli, mechi yetu bora msimu huu ni dhidi ya leeds na dakika 30 za crystal palace
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…