Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Kwanza nitofautiane na wewe kuhusu Rijkard.
Rijkard katika kipindi chake alichukua UCL 2006, akatwaa Laliga na mara mbili na UCL.

Kilichotokea 2007 baada ya kutwaa UCL wachezaji wengi sana muhimu waliondoka Edmilson, Van Bomel, Van Bronqhost, Saviola, Giuly, Belleti na wengine wengi akaingiza wachezaji wapya saba Henry, Eric Abidal, Yaya Toure, na Zambrota na wengineo hivyo alihitaji muda kuweka sawa japokuwa tatizo lilikuja wachezaji hao walihitaji muda mrefu sana kukaa sawa kwenye kikosi ambacho tayari kilikuwa kimeondokewa na wachezaji wengi na wengine kama Henrik Lasson wakiwa wamezeeka.

Kumbuka katika misimu yake mitatu Guardiola pale hakufanya usajili mkubwa zaidi ya kumsajili Ibrahimovic, Gerrad Pique, Javier Mascherano , David villa na Adriano na hawa ilikuwa msimu wa pili wa Guardiola.

Kikosi cha kwanza kilichompa mafanikio Guardiola ni alichokitengeneza Rijkard.

Ni ngumu Mwalimu kutengeneza succession plan nzuri baada ya Squuad kuishiwa makali ndiyo maana unaona Rijkad kaichukua Barcelona 2003 mpaka 2008 hapo kati alichukua UEFA.
 
Lampard alikuta Chelsea ambayo imetoka kuchukua Epl na Europa League kutoka kwa Conte na Mauricio Sari lakini ilikuwa imezuiwa kufanya usajili.

Msimu wake wa pili alifanya usajili ilihitajika muda kuiassemble squad yake.

Lakini kumbuka Chelsea ni timu yenye football culture tofauti kuliko vilabu vyote EPL ni timu ambayo huwa inaadapt haraka sana mabadiliko ya benchi la ufundi ndiyo karibu kila kocha aliyefundisha Chelsea Post Mourinho alipata mafanikio ukiondoa Scolari, Boas na Lampard tu.
 
Kuhusu Zidane hakuna sehemu yoyote niliposema ni mbaya ila nilichosema alikuta Squad iliyokamilika kila idara.
 
Nature ya kikosi tulichonacho pia inawatisha baadhi ya waalimu kuikubali united katikati ya msimu maana italazimu kuondoa wachezaji wengi wa kikosi cha kwanza kitu ambacho tunaaminishwa kuwa ni world class
Kwamba hatuna wachezaji wazuri?
 
Mourinho aliwasajili
11. Christiano Ronaldo
12. Karim Benzema
Kumbukumbu zangu ziko tofauti na zako.

Kwamba Mourinho aliwasajili Karim Benzema ba Chrisriano Ronaldo? Hawa si walisajiriwa Madrid mwaka 2009? Mourinho mwaka huo wanasajiriwa si alikuwa Inter Milan na msimu huo wa 2009/2010 ndipo akachukua UCL akiwa na Inter?
 
Yes nimerekebisha kule juu lakini walisajiliwa na Manuel Pellegrin
 
Asanteni sana wadau kwa kunikumbuka


Hatimae yametimia ilikua ni miaka miwili ya masimango kejeli kuchekwa na kujikuta nipo peke yangu kwenye hii harakati lakini leo hatimae nimeondoka na kijiji humu😀😀😀😀


simamia unachokiamini maana ipo siku tu kitakuletea mafanikio


BADO HAJAFUKUZWA TU😀😀😀
 
Hio ndio culture yetu sisi na tumefanikiwa kwa kiasi kikubwa

Sasa iga kunya kwa tembo
uchanike msamba
 
Ndio,wengi hawana hadhi ya kuichezea united chini ya kocha anayetaka makombe
wachezaji wengi manutd wako vizuri, tatizo hawajapa walimu kuwa drill brain zao. walimu wamekomalia physical fitness tu, mtu kama martial, Rashford, Pogba, sasa na Maguire wana serious mental problems, na hawana mtu wa kuwasidia kuover come challenges zao.

Rashford na Martial.... ni wachezaji waliokuwa wamebeba matumaini makubwa sana ya mashabiki na management na wanalipwa pesa mingi, sasa wanataka kufunga magoli kwa lazima, then wanasahau kuna wenzao uwanjani n.k this is a serious problem.

same applies to Pogba, yeye as long ana perform National team, anaona tatizo labda ni jezi na tayari anajiona hakubaliki na mashabiki.
 


Mzee mzee...sherehe ipo wapi sasa??
 
Nadhani ieleweke kwamba kuna makocha uwezo wao ni wa kawaida yaani anaweza kuitoa timu say level C akaiweka level B na hapo ndiyo mwisho wake hawezi kuipeleka level A hata umpe misimu mingapi na resources za aina gani. Aina ya makocha hao ni kama Lampard na Ole. Sio kwamba walikuwa wanapenda matokeo mabovu lakini uwezo wao wa kufundisha umefika mwisho pale. Watakuwa bora pengine huko mbeleni lakini sio kwa sasa. Chelsea isingemfukuza Lampard ingeendelea kuwa kama ilivyokuwa sababu Lampard mwenyewe aliwahi kusema Chelsea kuchukuwa makombe makubwa au kugombea makombe makubwa ni kuanzia 2023/2024. Leo hii tumeona mabadiliko ambayo Tuchel kayafanya chini ya mwaka toka aipokee timu sahau kuhusu kombe la UCL na Super Cup ila unaiona kabisa hii timu ipo kwenye level inayopaswa kuwepo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…