Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Njooni Chelsea enyi wa unyumbuni musumbukao na kuteswa na kijimtu kama olesendeka gunna kinachong'ata na kupuliza. Ninyi mizigo yenu yote tutaibeba mabegani mwetu na kuhakikisha munaishi kwa furaha tena.
CFC
 
Michezo mitano ya ligi inayofuata itaamua hatima ya Bwana Ole pale Carrington.
Nimeichungulia ratiba yetu ya mechi zijazo imenibidi nikubaliane na unachokisema kwa njia ya maandishi, lakini kuna jambo moja laziba tuliweke vichwani mwetu.

Ole wa sasa ana kundi kubwa sana la wachezaji wenye uwezo wa kumpa huduma ya magoli pengine kuliko kocha mwengine yeyote pale England, na hii ndio silaha yake kubwa itakayoendelea kumweka mjini kama ataendelea kuchanga karata zake vyema.

Ukitaka kupima ubora wa Ole kiufundishaji na si kimatokeo basi subiria mechi atakayofanya mabadiliko ya kikosi kwa kuwaweka nje key players hususani bruno fernandez, kwa mfano nimeona mechi ya leo akizungumzia mpango wake wa kufanya mabadiliko ndani ya kikosi kwa kuwapa nafasi wachezaji wengine kama lingard, mata, telles, elanga n.k

tukumbuke kuna timu hazibadiliki kiuchezaji hata kama zitatumia wachezaji wa kikosi cha pili, timu ni hizo ni man city, liverpool, leeds, chelsea, brighton.

je pattern ya kiuchezaji itabaki vile vile au itaathiriwa na mabadiliko ya wachezaji?
bila ya shaka jibu tutalipata usiku wa leo na hapo ndipo tutakapofahamu rasmi Ole ni kocha wa aina gani.
 
hain
haina hata haja ya kuwa na wasiwasi Ole ni mweupe tu kimbinu anafundisha mpira mwepesi sana kama hesabu za jumlisha.
 
Akibadili leo tutakua na mechi ya hovyo sana nadhani, jamaa wakiweka kile kikosi chao vilevile tunaweza kuaga kombe la kwanza leo ngoja tuone.
 
Mimi ndio nazaliwa huo mwaka jamaa ndio linaanza kuupiga mwingi ..haya maisha hata dah!

Ila Skozy alizingua sana kucheza unyumbuni.
Daaah kumbe ndomaana mnatusumbua, nilikuwa najiuliza hivi huyu jamaa ni mtu mzima kweli? Sasa nimejua .


Olachuga bwana😃.
 
Westham come on...!


Kwa sisi tunaoangalia mpira live ndio tunajua maajabu anayoweza kufanya westham
 
Endapo Westham wakiamua kuanza na kikosi chao cha kwanza na sisi tukatumia wachezaji wa akiba dhidi yao,hakika tutakuwa na wakati mgumu.
Kna uwezekano leo bwana Jones akapata dakika kadhaa dhidi ya westham wakati Bwana Bailly akiwa hajui ni lini atacheza kikosi cha kwanza.
 
Mdau mpaka leo ujajua ole ni kocha wa aina gani???

Ilo jasho tutakalotolewa leo kwa kikosi icho utakuja kumkataa hapa waziwazi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…