Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Hahah nakuelewa mkuu ila kuna EFL kuna UCL kuna FA na hii EPL. Sasa tukisema tuchezeshe wachezaji walewale watachoka mapema watashindwa kupafom.
Nachotaka kusema ni kwamba mtu akiwa below average na tumekaa nae kwa muda mrefu na analipwa hela ndefu hatupaswi kumfuga eti kisa depth..tunafagia na kuleta vipaji vipya.
 
Tunaweza kusajili DM na tusione faida yeyote kubwa ya kiuchezaji kutoka kwake kwa sababu ya tatizo kubwa la ukosefu wa structure ya kiuchezaji hususani tunapokwenda mbele, tupo slow sana kwenye buildup hususani tunapotaka kuvuka mstari(progressive) wa midfields kwa pasi na kuingia rasmi eneo la adui.

mimi naamini timu bora kiuchezaji ni ile yenye uwezo wa kuficha makosa ya wachezaji waliopo jambo ambalo tuchel ameweza kulifanya kwa muda mfupi pale chelsea huku Ole akishindwa kufanya hivyo, tutake tusitake hakuna mchezaji aliyekamilika ila mwalimu ndiye muwajibikaji wa kutengeneza mfumo wa kumsaidia mchezaji husika.

Hivi rudiger, harvetz, jorginho wa tuchel wanafanana na wa lampard?
Hivi fred wa brazil analingana na wa kwetu sisi?
Hawezi kulingana kwa sababu structure ya Brazil inamfichia makosa yake.

kwa ufupi nimeanza kupoteza imani na mwalimu kiuchezaji na si kimatokeo ya uwanjani.
 
Nachotaka kusema ni kwamba mtu akiwa below average na analipwa hela ndefu hatupaswi kumfuga eti kisa depth..tunafagia na kuleta vipaji vipya.
Ni kweli ila nahisi Man U ina big minds wanaotazama ishu kama hizi.. Cha msingi ni tuamini tu maamuzi yao ya kubakiza wachezaji kama Martial
 
Nimeanza kuiangalia game yetu kuanzia dakika ya 61. Siwezi kusema kuhusu makosa ya sancho wala James kila nilichokiona ni mfumo mbovu wa utengenezaji nafasi za kupasiana tokea kwa kiungo kwenda kwa washambuliaji.

Wiki iliyopita wachambuzi Eric laurie pamoja na malama (sijui kama nimepatia jina),hawatakuwa na kazi kubwa sana kuichambua hii mechi zaidi ya copy na ku paste walichofaka wiki jana.

Kwa uchezaji wa city,Liverpool pamoja na Chelsea,united tutaendelea kugombea top 4.

So sad
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…