Mpaka sasa tungekuwa title contender iwapo recruitment department ingekuwa inatatua matatizo sahihi ya United badala ya kufanya patchwork.
Kama walikuwa wameshamsajili Bruno Fernandez hawakuwa na sababu yoyote ya msingi ya kumsajili Donny kwa sababu ni midfielders ambao hawana ball retention capacity wanapocheza, japokuwa Donny na Bruno wote ni wachezaji wazuri na wanatofautiana quality lakini wana weakness inayokaribiana hawatunzi mpira timu inapokuwa nao tatizo hili linakuwa kubwa zaidi ukizingatia pia Fred na Scot hawana uwezo mkubwa wa possession pia.
Mpaka sasa United inahitaji usajili tena wa wachezaji watatu muhimu ili timu iweze kuwa na balance nzuri.
Wing ya kulia, Center back mmoja na Central Midfielder au Holding atakaye complement weakness za Bruno na Donny.
Pogba anaweza kufanya hiyo kazi ya CM lakini anahitaji holding midfielder makini na mpambanaji sawa na Ng'olo Kante, Joshua Kimmich, Goretzeka au Fernandinho.
Center backs wetu kuendelea kuwa pazia msimu huu ni ishara kuwa either hawaendani kiuchezaji au wanauzembe unaofana.
Tuendelee kuupa muda nafasi huenda ukatupa mwanga zaidi juu ya mwelekeo wa timu yetu.