Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Kati ya Lampard na Ole nani mkali?
Nazungumzia lampard.. nazungumzia chelsea. Sijamzungumzia ole. Usijaribu kuhamisha mada.

Lampard hachezi mpira.. unamtupia lawama zote wkt wachezaji kule hawaonyeshi hata bidii.
Angalia barcelona walivyo. Yule kocha si wa viwango vyao.. lakin wachezaji ndio wanaibeamba ile timu japo kwa shida.
 
Nimeshtuka sana alipomjumuisha Mason Greenwood hapo ktk maoni yake. Hawa ni aina ya mashabiki ambao hata timu ikiwa inafanya vibaya hawaangalii mpira.

Huwa nikimuangaliaga huyu dogo nafarijika sana kuwa tuna kipaji kama kile kikubwa sana kikosini kwetu.
 
Hahahahahahaa
 
Hasa hasa Anthony Martial huyu ana mbadala eneo analocheza kwangu mimi huyu hapaswi kuwepo kikosi cha kwanza. Huyu anapaswa agombee namba na Rashford upande wa kulia.

Kwa maoni yangu mimi kwa sasa inapaswa pale mbele wacheze Rashford Cavani Greenwood. Upande kushoto Rashford hana mshindani sahihi kwa wachezaji tulionao pale kikosini kwa sasa.

Upande wa kulia endapo kocha atatumia viungo wawili wa kukaba basi Paul anaweza kuanza mbele ya Mason. Option nyingine ni Mata eneo hili la kulia.
 
Hahahaaaa, mzee wa statistics, yn Mkwawa akikuambia kitu usibishe mana ni lazima atakuletea stats zake from Taured
 
Cha kushangaza ni kwamba huyu mtoto hachezi hovyo na wala hapotezi mipira anaficha mpira na hana maringo, akipata nafasi huwa anafunga tena wkt mwingine ni angle ngumu ila bado anakwambia eti ni hovyo, anataka kumpa majukumu makubwa mtoto mdogo, anataka awe anafunga kila mechi pasipo kujiuliza anacheza nafasi gn.

Jamaa wa ajabu sana.
 
Chelsea muwe mabingwa. Pale top 4 wakiwa wamelala au ? Fikieni top 4 kwanza. Unataka top 4 uko nafasi ya 8.
Huu msimu nakwambia tunabeba hili kombe ..amini kwamba
Angalia liverpool anatobolewa kwake ..wewe ukifika mwisho wako wa kutamba ..naanza mimi ..nikianza mimi ndo hadi mwisho kisha nanyanyua kwapa...

Naona Chelsea bingwa msimu huu 20/21 nani anabisha??
#CFC
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…