radika
JF-Expert Member
- Jul 15, 2014
- 20,450
- 32,290
si kwamba tunafurahia hapana ukiangalia mwenendo wa timu na usajili na makocha waliopita ni ngumu sana kupata flow ya timu hasa kocha wetu si mzoefu kuna muda tunamlaumu afukuzwe je anaekuja itakuwaje?Na angefungwa manchester united dhidi ya manchester city hii iliojichokea moto ungelizidi(sina furaha na mwenendo wetu)
kitu pekee nilichokiona jana ni pasi nyingi zilizoanzishwa na de gea, maguire, lindelof, scott then bruno pindi anaposhuka chini na tukifika maeneo ya adui hatuna ubunifu wowote baraka ya kurudisha tena mpira nyuma.
ukweli usemwe tunacheza ovyo, sielewi ni kwa sababu gani mpaka leo timu kubwa zina dominate possession dhidi yetu halafu bado tunafurahia haliyakuwa kibajeti tunalingana
Hii timu haiwez kuwa sawa hiv karibuni ni suala la muda simpend kocha ila kuna muda namuonea huruma alikuwa akiwataka watu wa kufanya nao kazi hakupata kwa hiyo kalazimika kutafuta plan b vipi kama angepata watu kama jack na sancho? Ubunifu ungekuwepo wala wakina greenwood tusingekuwa tunawalaum hao tunawapoteza kwa kuwa wanapewa majukum makubwa
Namuangalia sana jack wa aston villa kama angepatikana na sancho tungekuwa mbali sana