radika,
Nimeona hapo juu kuna mahala umehamaki sana Bayern kumtaka mchezaji kama Callum Odoi labda kama ulikuwa unatania ila kama ulikuwa serious kuna kitu kikubwa sana ambacho unachanganya yaani mchezaji wa kuja kujenga timu vs mchezaji wa kuja kuongeza hamasa ya timu (au morali). Mchezaji wa hamasa ktk timu mara nyingi hununuliwa kwa kufanya head hunting hii ni direct approach benchi la ufundi linasema tunamtaka mtu fulani yupo mahala fulani hii ndiyo njia hutumika sana kibiashara na ndiyo hufurahisha mashabiki kwa timu zenye fan base kubwa kama Manchester United mara nyingi huleta watu wenye majina zaidi.
Na njia ya pili ni scouting-appproach based strategy hii unawapa assignment watafuta vipaji wenu kila kona kuleta majina kadhaa kwa pecking order kwa nafasi husika kwa sifa ambazo benchi la ufundi limependekeza. Hii njia kwa uchunguzi wangu binafsi ndiyo njia bora zaidi maana mnasajili watu wenye sifa sahihi zaidi haina business motivatives wala kufurahisha mashabiki ila inaleta wachezaji watakao fanya vizuri zaidi uwanjani. Manchester United tulifanikiwa sana na hii njia kwa miaka yote tokea Fergie awe kocha tulipofanya head hunting mara nyingi hatukufanikiwa (mf. Sebastian Veron), mara nyingi tulisajili wachezaji kwa recommendations za ma-scout na walifanya vizuri sana mf. Ronaldo, Ruud Van Nestrooy, Carlos Tevez, Chicharito, Vidic, Evra wote hawa wamekuja kujulikana zaidi Manchester United ila kabla ya hapo hawakuwa wachezaji wa kutisha sana au mvuto wa kibiashara.
Nikirudi kwenye mfumo wa usajili wa Bayern, hawa wapo kama Liverpool nilishaandika juzi jinsi Liverpool walivyo kwa sasa, yaani wanafanya strategic move sokoni wanaangalia wapi pana mapufungu na wanafukia kwa kuangalia sifa zaidi ya mtu anayenunuliwa kwa nafasi husika na sio jina la mtu anayefanya vizuri ktk nafasi fulani. Na ndio maana utaona Liverpool na Bayern hawafanyi sajili ambazo zitauza magazeti ila wanalenga capacity deliverance ya mchezaji na sio kufahamika kwake kama sisi tunavyoingia sokoni japo na wao huwa wanachanganya na head huting pia. Ndio maana utaona sisi tume-stuck na Jadon Sancho kwa ssb tunatumia head-hunting approach wa kati in reality kuna wachezaji wengi sana duniani wapo wenye vipaji kumzidi huyu dogo ila hawana media coverage mf. mchezaji kama Haaland amefahamika baada ya kucheza UEFA mwaka mmoja na nusu uliopita.