The best 007
JF-Expert Member
- Oct 6, 2019
- 42,480
- 98,527
Wapinzani wanavyoona tunamkosoa Maguire au Bissaka basi wanadhani ni wabovu kiivyo kumbe cvyo, lkn ukweli wanaujua but wanachotaka man u iwa suck hao wachezaji zen waanze kukashifu, mfano Lukaku wapinzani waliongoza kwa kumsema vby leo hii ameondoshwa hao hao wanakuja kutucheka eti tumemfukuza fundi, huwa nacheka snHivi watu wanatoa wapi ujasiri wa kuwaita Harry Maguire na Aaron Bissaka mabeki mabovu? Kuna watu wananifanya nitilie mashaka uwezo wa kuangalia ubora wa wachezaji. Hawa wachezaji sio wabovu tunapowakosoa haimaanishi ni wabovu ila tunahitaji wafanye zaidi ya hapo maana tumewekeza pesa nyingi kwao na tunaamini wana uwezo wa ku-deliver zaidi ya hapo.
Harry ameongoza ukuta uliofungwa magoli machache zaidi msimu huu nyuma ya Liverpool(33) na Manchester City(35) na sisi tulifungwa goli 36 tu pamoja na clean sheet 12 . Maana yake tumezidiwa goli tatu tu na bingwa. Msimu wa 2018/19 tulifungwa goli 54 na tulipata clean sheet 7 tu kabla ya Harry na Aaron kuja.
Mimi ni moja ya watu ninayetaka tutafute beki wa kati, kwa muda mrefu nimekuwa nikiona kama bado tunakosa mtu anayeongoza ule ukuta wetu. Harry tatizo lake kubwa huoni akiwaongoza wenzake uwanjani kuanzia kama nahodha wa timu wala kama kiongozi wa ulinzi muda mwingi utaona anacheza as if hana majukumu ya kiuongozi huoni akiwapanga wenzake wala huoni akionyesha kukemea mtu akifanya ujinga unaogharimu timu.
Mfano mzuri tafuta ile mechi tuna sare na Southampton au ile Chelsea (tulifungwa) au ile ya Everton(sare) na hata ile ya Sevilla(tulifungwa). Hizi ni mechi ambazo msimu uliopita tulipoteza kwa kukosa kiongozi uwanjani utaona ni kama hamna mtu mwenye authority ndani ya uwanja. In long, kama tunahitaji makombe kuna muda unahitaji kiongozi uwanjani hasa hasa mtu huyo anapendeza awe anacheza hapo hapo eneo la ulinzi hata kama sio captain ila mtu mwenye uchungu pale ujinga unapofanyika hutaona tukifungwa vigoli soft soft vinavyoigharimu timu.