Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Imagine timu yetu ina Luke shaw/William na awb halafu wao wana kimmich na Davies. Mbele wana lewa,muller,sisi tunajiandaa kuanza ligi na rashford pamoja na martial. Namuunga mkono jamaa Ugiligili kwenye hoja yake hapo juu.
Yaani jamaa wana full mziki..
 
Team haiwezi kuacha kwenda kwenye mashindano kisa haijasajili

Lyon na Liepzig wanakikosi kuzidi united ?
Bahati hazikosekani lakn kwanini uende kwa kubahatisha na si kushindana?

UCL ni muhimu sababu ya mapato ,lkn kwa klabu kubwa kariba ya Man u anatakiwa aende kushindana ,sio kufika 16 bora.

Ndio hoja ya jamaa hapo , Kina Leipzig , Lyon nadhan wamejitahidi kufika hapo , Safari yao imeiva
 
Team haiwezi kuacha kwenda kwenye mashindano kisa haijasajili

Lyon na Liepzig wanakikosi kuzidi united ?
Man United inabidi tuende UEFA tukawashe moto bila kubahatisha..hao Lyon kufika tu robo fainali ni mafanikio kwao

Point ya jamaa ni kuwa muda wa kujipanga upo,why hatufanyi sajili na tuna mapungufu kibao?

Kama Ole anahisi timu ipo vizuri basi acha tusubirie msimu uanze

Personally naona tunahitaji;

✓Striker
✓CDM
✓Full back(who is good going foward)
✓CB kitasa na anayeweza kucheza na mpira
✓RW


Tusajili basi hata watatu kwenye hiyo list basi

Na kuna wapuuzi kibao wakuwaondosha kwenye timu..wanatufanya tuonekane kama Newcastle

United inabidi iwe na list A na B zilizoshiba kabisa
 
Muda wa usajili mpaka mwezi October huko haraka ya nini ?

Tutasajili tu lakini kusajili peke yake hakukupi kikosi imara unahitaji kutengeneza chemistry ya team ambayo it takes time.

Man United last season tulifika quater final kwa kikosi dhaifu kuliko hiki sasa hiki.

Tukumbuke pia timu za germany zimepata muda mrefu wa kujiandaa kuliko zingine kwa sababu ya kumaliza ligi mwezi wa sita huko.
 
Recruitment team ya United ina matatizo ndiyo maana mimi huwa sishobokei usajili tena.

Nasubiri siku wakitangaza ndiyo najua tumesajili wasiposajili pia poa tu tunaenda kwenye ligi hivyo hivyo.

Kujenga kikosi imara ni process ndefu unahitaji misimu miwili mpaka mitatu vinginevyo kubahatisha tu.

Hata sasa hivi mafanikio tutaanza kuyaona msimu wa 2021-2022 kama hatutaanza a new project

Otherwise ni kujipa stress isiyo na tija
 
Jamani Bayern pale mbele na katikati wapo moto sana ila wakicheza na timu inayoshambulia sana na wapo makini, nawaona kama Bayern wana defence mbovu ni kwa sababu so far bado defence yao haijapata serious test. Mabeki wao wa kati (David & Jerome) sio wazuri sana wana makosa sana ni vile wamecheza na watu walio-flop kwa sasa.

Nimeona kuna mtu anasema kwa nini tusichokonoe kwa Alphonso Davies, kwenye timu yetu huyu jamaa hawezi kutufaa ni mzuri sana offensively but not defensively unless tuwe tayari na timu inayoweza kukaa na mpira zaidi. Kwa uchezaji wetu hawezi kutufaa maana huwa mara nyingi hatukai na mpira sana, sisi tunahitaji aina ya wachezaji ambao wapo comfortable hata tunapokuwa hatuna mpira kwa muda mrefu.

Luke Shaw hofu yangu kwake ni injury prone tu ila anaweza kui-prove zaidi akijengwa vizuri. Bissaka anahitaji kupewa training chache tu za kushambulia ila namuona amekamilika sana akijua tu kuucheza mpira hasa hasa akivuka mstari wakati ni bonge la fullback, mapungufu yake ana mchango mdogo muda tukiwa na mpira hasa tunapovuka mstari wa wakati timu ikiwa inashambulia kutokea upande wake.

Binafsi naamini tunahitaji wachezaji watatu tu kwa sasa, Beki wa kati wa maana ambaye anapaswa kuiongoza ile safu yetu ya ulinzi acheze na Harry, kiungo wa chini wakucheza nyuma ya Bruno na Paul ile nafasi ya Nemanja. Mwisho ila sio lazima sana tunahitaji mshambuliaji wa kuja kuongeza nguvu pale mbele. Mimi kwa sasa ningependa hata tupate mkongwe mmoja kwa muda wakati tunaji-fix kupata longterm target kwa sasa tumchukue mtu kama Edin Dzeko. Deal la Sancho linapoteza focus ya kujenga timu, kuna wachezaji wazuri sana kama tukiamua kufuata other options sio lazima tumkomalie yeye tu.
 
Binafsi, nashawishika kusema dili la Jadon Sancho ni bora tuachane nalo tu, naona kama hatufaai tena. Tunapoteza focus ya kujenga timu muda huu mchache tulio nao.

Laiti kama tukihamisha nguvu kutafuta vipaji vingine nje ya huyu Jadon, naona kabisa tuna nafasi kubwa sana ya kubeba ligi msimu unaoanza mwezi ujao ni vile timu yetu inaongozwa na watu wazembe (Ed pamoja na washikaji zake) wanaopenda kutoa excuse kila muda. Tunakomaa na mtu mmoja tena nafsi ambayo sio mapungufu yetu halisi kwa sasa.
 
Mkuu lazima tutasajili, tujipe mda.
Soko ni gumu kwa kuzingatia Jina la timu yetu kila mtu anawaza kututapeli tu.....
Wachezaji wakawaida ila kwa kuwa ni Man U basi tunatajiwa pesa ndefu.
 
Dah! Man U kweli miyeyusho mbona kuna wachezaji wazuri wa kufatilia muda huu. Kama Upemecano kwa beki ya kati yuko vizuri.

Dah! Namtamani Alphoso Davies hata kuwachokoza Bayern hatuwezi?

Kukomaa na Sancho ufala huo
Hapo kuna mchango mkubwa wa kocha na timu. Bayern inasajili wachezaji wa kawaida ila huwa wanakuwa brilliant blaa
 
United ya sasa sio ya kina David Gill.

Dirisha litafungwa na hakuna jipya utakaloletewa.
 
Mkuu lazima tutasajili, tujipe mda.
Soko ni gumu kwa kuzingatia Jina la timu yetu kila mtu anawaza kututapeli tu.....
Wachezaji wakawaida ila kwa kuwa ni Man U basi tunatajiwa pesa ndefu.
Kwanini David Gill hakutapeliwa?

Kwanini Madrid na Bayern wasitapeliwe?

Watu wanaohusika na recruitment ni viazi pale United.

Tuna pesa na Utajiri sawa na hizo timu mbili hapo juu, ila sisi kwenye usajili kwanini tupigwe tu?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…