Wakati CR7 anashangilia kutufunga, usisahau kuwa kocha wetu alikuwa Mourinho.Basi mimi ninachoamini ni kwamba CR alikitenganisha hiki kitu Man U na mtu Sir Alex Ferguson! Na inawezekana kabisa mtu akamheshimu Ferg na asiiheshimu timu. Na ninachoamini CR asingeshangilia kamwe goli la kuifunga United kama timu ingekuwa chini ya Fergie na yote hiyo nini kwa sababu anamheshimu zaidi.
Enzi zile Mourinho akiwa Chelsea(miaka ya 2004-2007) alikuwa anamwambia CR7 kuwa anajidai kufunha sana timu wakati hakusoma.
Na hata Mourinho alipokwenda Madrid na kukutana na CR7 huko, nadhani mwisho wa siku Mourinho hakuwa na maelewano na baadhi ya wachezaji kama vile Casilas na huenda hata Ronaldo.
Hitimisho langu, CR7 hakushangilia kwa kuifunga Manchester United bali kwa kumfunga Mourinho.