baada ya kufanya operation safisha mji (darmian, valencia, young, sanchez, fellaini, smalling) pamoja na kuleta wachezaji wengine wanne (ambao ni
wan bissaka japokuwa sifurahishwi na style yake ya kiuchezaji kwenye ulimwengu huu wa kisasa,
maguire amekuwa kiongozi mzuri sana kwa wachezaji,
daniel james huyu natumai kilio changu cha mwanzoni wa msimu kitafanyiwa kazi na ole msimu ujao ambapo sikupendelea huyu dogo awe mchezaji wa kikosi cha kwanza, bila ya kumsahau
bruno fernandez) hao wote kwa pamoja wameweza kuleta utofauti mkubwa kwenye kikosi chetu kwa muda mfupi zaidi.
ni matumaini yangu dirisha la tatu la usajili chini ya ole gunnar (tutamaliza biashara ya rebuilding kwa kutafuta wachezaji wengine sahihi hususani eneo la winga wa kulia) ila tatizo kubwa litakalobaki ni ubora wa mwalimu mwenyewe kututhibitishia ubora wake kimbinu, kiupande wangu bado namuona ole hajapevuka kimbinu ukimlinganisha na makocha wengineo wanaofundisha timu pinzani mfano jurgen klopp, carlo ancelotti, josep guardiola isala.
kuna nyakati sir alex alikuwa na kundi bora la wachezaji na hatimaye akafanikiwa kulitawala soka la england (1999, 2008-2009 na wapinzani wake wakasema anabebwa na timu bora pamoja na bajeti), vile vile kuna nyakati sir alex alikuwa na kundi la wachezaji wenye viwango vinavyotabirika (2010.-2012) kabla ya kuingia uwanjani ila pia alifanikiwa kulitawala soka la england na cha ajabu zaidi aliweza kucheza robo fainali ya ligi ya mabingwa takribani mara tatu ndani ya miaka minne kama nitakuwa nipo sahihi.
Hivyo basi ubora wa rebuilding unaofanywa na mwalimu hautoshi kuthibitisha ubora wake katika kuongoza timu kubwa kama manchester united (ole gunnar anapaswa kupevuka zaidi kama anahitaji kudumu man utd kwa muda mrefu zaidi, mfano mdogo tumeshacheza na wolves takribani mechi sita kwa siku za karibuni lakini mpaka leo tumeshindwa kupata tiba ya kimbinu dhidi yao).
sote hatufahamu anachokiwaza ed woodward (mzee wa suprise) kwenye mtindio wa ubongo wake, tukumbuke mara nyingi amekuwa akitamka hadharani ya kwamba klabu itaendelea kufanya kazi na ole msimu ujao kwa sababu ya kuvutiwa na mipango yake ndani ya klabu, hata nyakati za louis van gaal alimpaka mafuta kwa mgongo wa chupa na mwisho wa msimu akavunja mkataba wake licha ya kubeba ubingwa wa FA dhidi ya crystal palace na sababu kubwa anayoiangalia zaidi ni tiketi ya UEFA.
kivyovyote itakavyokuwa mwalimu yeyote atakayekuwepo msimu ujao atakuwa amebakiwa na kazi ndogo sana ya kukamilisha rebuilding ya kikosi chetu ambayo imeanza kufanywa na ole gunnar solskjaer...... ni mwendawazimu pekee ndiye atakayekuja na mkakati mpya wa kujenga timu na kuutelekeza huu uliopo.
- david degea au dean henderson
- wan bissaka + ( dalot au Ethan Laird )
- luke shaw + brandon williams
- eric bailly + lindeloff + tuanzebe
- harry maguire
- scott mctominay + nemanja matic (man of the match wa mechi yetu dhidi ya everton kwa mtazamo wangu)
- fred + paul pogba
- bruno fernandez
- marcus rashford
- anthony martial
- daniel james + greenwood + juan mata