Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Sasa Kaka Charlin C kwan mi nimesema nataka kumfata Mou kule Spurs?
Mi nimesema hatupati point 3 pale kwa Anc, tukishinda sana ni tumefungwa goli 1 tu!
Muda hakimu!
 

Well naona una point mimi sina shida martial akiwa benchi. Dogo akifunga nashangilia ila kuna vitu anakera sana unaona bora apumuzike mtu ambaye harembi aanze.


Mechi na Everton Ighalo akitumia krosi za James na Bruno vyema mbona namba yake inakuwa hatihati.


Na nataka ighalo aanze ili dogo ajifunze ili siku nyingine ajitume zaidi.
 

Tumekuelewa mzee. Binafsi nilikuwa shabiki wa Martial ila baada ya hizi kero za kibrazameni doh! Ukizingatia viungo wanarusha ball sana inabidi tuwe na mtu fighter kingine anaonekana Amejaa upepo yule.

Tumefurahi ameumia ili kutoa nafasi kwa ighalo akipiga mpira mkubwa dogo atajifunza na ataweza kujituma.


Martial anatusaidia lakini anajiona yeye ndio Striker pale Utd so leo kupumzika Jumapili Ighalo akipiga mpira wa kueleweka dogo atajituma sasa.

Tunataka wanaojituma.

Mbona Shaw tulikuwa hatumtaki ila siku hizi tunamkubali.

Lingard baada ya kocha kumkazia unaona japo katoa assist uchoyo kapunguza.

Ndio hivyo hivyo tunataka kila mchezaji awe challenged sio kujiona wewe ndio timu.

Bruno Kafanya Kelele za Pogba kuhama tuzipe go ahead. Imagine Bruno asingekuwapo tunasuasua kiungo Pogba angezidi kichwa yule.


Akirudi Pogba atajituma tu maana anajua ustaa wake unamezwa na Bruno mnyama.
 
Unamchukia AM9, then akiwa anafunga goli la ushindi/kusawazisha unajisahau unashangilia hadi koo linakukauka. Aiseee!

Sent using Jamii Forums mobile app

Ndio mpira bana ila jamaa huwa muda mwingine anakera na migrovu yake. Hata Ole kasema anatafuta mtu ambaye yupo tayari kuvunjika pua akipigania timu.

Kufurahia Ighalo kuanza ni kutoa challenges kwa dogo ili muda mwingine ajitume zaidi.

Tulikuwa tunafurahia Brandon Williams kuanza badala ya Shaw matokeo yake Shaw kaacha ubishoo now anafight maana anajua akizingua Brandon anamkwapua namba hiyo ndio tunataka kwa Martial ajue yeye sio striker pekee ili asivimbe aendelee kujitumaa.

Safi sana Ole piga benchi vichwa vigumu hadi vijitume akija Rashford akileta unaa piga benchi.

Fanyia mabishoo kama ulivyofanyia Perreira na Lingard ili akili ikae sawa.



Hatuwaombei mabaya bali tunataka wawe challenged ili Man U iwe moto kila eneo.
 
Hahaha sure huwa sometimes anajifanya brazameni

But uwepo wake utaimarisha sana safu ya ushambuliaji na itatupa options nyingi tunapoliface goal la Everton.
Sent using Jamii Forums mobile app
 
martial amenza mechi 8 against everton, Amewafunga goli 5 na assist 2, ana zaidi ya contribution 1 ya goli in 90 minutes,
 
martial amenza mechi 8 against everton, Amewafunga goli 5 na assist 2, ana zaidi ya contribution 1 ya goli in 90 minutes,

Ighalo akimuwekea pressure huenda akawa na 2 goal in 90. Tatizo sio kwamba hatumtaki bali tunataka awe challenged ili apambane zaidi, akipambana zaidi means Man U tunakuwa fire.
 
DE GEA SOKONI


DAVID De Gea mlinda mlango wa Manchester United huenda akauzwa ili kuiongezea timu yake mkwanja wa kufanyia usajili msimu huu.
De Gea mwenye miaka 29 raia wa Hispania amekua akifanya makosa ya mara kwa mara ambayo yanaigharimu timu yake kushindwa kupata matokeo mazuri.
Juventus na PSG zinapewa nafasi ya kuinasa saini ya nyota huyo wa Manchester United.
Mkataba wake ndani ya United unatarajiwa kumeguka mwaka 2023.

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Inabidi tuwabomboe Sheffield united msimu ujao wawe na adabu, rudisha Henderson
 
Japokuwa it'll be very painful process kumuachia golikipa mzuri na mwenye uzoefu kama David De Gea ila itakuwa ni busara zaidi kumuachia aondoke kama kweli kuna watu watajipendekeza kumtaka. Binafsi namuona kama ubora wake unashuka kwa takribani misimu miwili mfululizo na amekuwa ni golikipa mwenyewe makosa sana kwa sasa hasa hasa akiwa exposed under pressure.

Pia wachezaji wengi kupitia mawakala wao wanatumia sana mshahara wake na wa Alexis Sanchez kama reference angle for re-negotiations mfano mzuri Anthony Martial na Marcus Rashford. Madhara ya kuwa na mishahara mikubwa kwa timu inawaminya kuwa na uwezo wa ku-accomadate exceptional talents nyingi kwa wakati mmoja kila mtu atataka alipwe kama fulani. Mwisho wa siku mnajikuta mishahara ya wachezaji watano wa juu inazuia vipaji vingine vitano kuwepo ktk timu vyenye uwezo sawa au zaidi ya hivi tunavyo vilipa pesa nyingi.

Unajua kwa nini Real Madrid waliweza kuwa na galacticos wengi miaka ya nyuma kwa wakati mmoja? Au kipindi kile tunachukua treble mwaka 1999 timu ikiwa chini ya Peter Kenyon? Au mwaka 2008 chini ya Gill? Tulikuwa na vipaji vingi kwa wakati mmoja. Before salary bubble bursted (thanks to people like Ed for screwing up salaries structure), All of them had one thing in common, secret policy of capping salaries beyond insanity.
 
Mkuu angalau tufurahi anapowekwa benchi ila siyo anapoumia. Hivi kwa mfano ighalo akashindwa Ku deliver ktk hyo game na martial kaumia tutafanyaje ilihali rashford nae hajarudi!? Au ndo greenwood?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…