Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Hata mechi na L.City walikuwa na counter attacks za hatari sana.

Maguire hana mbio kwa hiyo nategemea ataelekezwa kuachana na utaratibu wa kupanda.

Hawa walitutoa FA Cup wakati ndio lilikuwa tegemeo msimu uliopita.
Endeleeni kujidanganya tu , Jana Pedro na mbio zake kama Ferrari alikuwa anaishia miguuni Mwa Harry Maguire na kuanzisha kama si kutapanya mipira kulia kwa Bisaka au Au kushoto kwa Bwana Luke Shaw..


Endeleeni kuchoma ubani.
 
Kwahiyo hoja yako ya mwanzo imekufa kifo cha mende siyo ?
 
Daaa wakuu hii timu pamoja na kushinda goli nyingi dhidi ya timu ngumu na kubwa Chelsea Mimi bado sioni kama kuna mabadiliko yoyote ya kiuchezaji tofauti na msimu ulopita.

Timu hii itaendelea kuingia na uwoga pale itapocheza na big 4 au six kama kawaida yake kitu ambacho naamini siyo sahihi. Timu hii ikiendelea kucheza kama ilivyocheza na Chelsea bado itaendelea kutumia vibaya resource zake kwa maana wachezaji ilionao na mfumo wanaocheza ni tofauti.

Kama itaendelea kucheza kama ilivyocheza na Chelsea basi nitaamini Ole hana uwezo Wa kufundisha mpira na atafukuzwa mapema. Nilitamani sana Chelsea ilivyokuwa inacheza ndiyo iwe Man U.

Pogba ni miongoni mwa wachezaji walocheza hovyo sana ktk ile mechi. Na sioni mabadiliko yoyote toka kwake kama nilivyotarajia. Utoto mwingi kiasi kwamba akiendelea vile ataigharimu sana timu. Uchezaji na jukwaa ushapitwa na wakati.

Wan Bisaka alicheza vema sana ila Harry Maguire akiendelea vile basi haraka sana apewe kitambaa cha unahodha
 
Hiyo "nyuma sana" umezidisha. Scot ni mwepesi kulinganisha na Matic. Mm nna confidence na midfielder trios ya Pogba, Scott na Pereira. Wataimpruvu tuu
Holding Midfield pace ni added advantage sio key quality ya eneo hilo tofauti na maeneo kama center Forward ambako pace ni key quality

Scott utamweka level moja na Wilfred Ndidi wa Leicester kwenye kukaba ?
 
Unasema pogba alicheza vibaya? Ww unaangalia mechi gani?
Pogba amepangwa na mctominay ambaye hakuwa na msaada mkubwa sana kwake.. alipoteana pogba akawa amebaki kama yuko mwenyewe.. halaf unlaumu huku kiungo kilizidiwa.

Pogba ataonekana timu ikisajili kiungo mwenye uzoefu wa kucheza nae. Otherwise tutaendelea kuwa average.
 
Umesema kuwa ulitamani sisi United tucheze kama Chelsea...ina maana muda huu tungekuwa tunaugulià maumivu ya kufungwa 4-0 sio??..kama chelsea walicheza vizuri,why walishindwa kutufunga??..tuangalie mechi zijazo ndo tutajudge vizuri

Tuipe hii timu muda,ndo mwanzo wa msimu jamani..
 
Jamaa ametoa assist mbili ila bado anaonekana bado..first half nakubali pogba alikuwa sloppy na timu nzima pia ilokuwa sloppy...ila second half jamaa kacheza poa tu IMO..
 
Tunataka watu kama hawa wenye Technical eyes kwenye mpira well said Mr.
 
Holding Midfield pace ni added advantage sio key quality ya eneo hilo tofauti na maeneo kama center Forward ambako pace ni key quality

Scott utamweka level moja na Wilfred Ndidi wa Leicester kwenye kukaba ?
Kukaba Sana sio sifa ya malegend vile vile, ukimtoa makelele na kidogo ngolo kante Ni nadra Sana kumkuta huyo mkabaji akiwa mchezaji mzuri Sana.

Juventus wanacheza na pirlo Kama no 6 Wala hakabi, Man U wanacheza na Carrick Kama no 6 Wala sio mkabaji Sana Kama Ndidi, bosquet wa Barcelona anapitwa na Ndidi ukabaji etc

Kuna wachezaji hawakabi ila Wana uwezo wa kuread mchezo, Wana instincts za kuzuia mashabulizi Bila kutumia minguvu, Wana control mechi hata Kama wapo nyuma etc.

Baada ya kusema hayo ukija kwenye stats website ya premier league Mc tominay ana tackling success 86% na Ndidi ana 65%, hivyo wachezaji Hawa wawili MCtominay ana chance kubwa ya kumpokonya adui mpira, sema Tu Ndidi amecheza mechi nyingi zaidi pengine ndio maana percentage zake Ni ndogo, ila still MCtominay si wa mchezo mchezo, alitoka na 100% tackle rate against Barcelona,
 
Endeleeni kujidanganya tu , Jana Pedro na mbio zake kama Ferrari alikuwa anaishia miguuni Mwa Harry Maguire na kuanzisha kama si kutapanya mipira kulia kwa Bisaka au Au kushoto kwa Bwana Luke Shaw..


Endeleeni kuchoma ubani.
Maguire hana shida ya kukaa,ila mbio hana.
 
Una haki ya kuona hivyo na wengine kuona tofauti
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…