Kusema kweli usajili wetu unafuata uelekeo unaokera sana. Hadi sasa tumesajili wachezaji 3 na wote wana asili ya UK. Sawa inawezekana ole kaangalia uwezo na ari sikatai ila kwenye soko hili kuna wachezaji wana uwezo na ari kubwa kuliko hawa tulioletewa endapo utafanya ulinganifu.
Kwa nafasi ya DJ kuna mtu kama ziyach,neres na sane asiyetulia pale city ambao wana uzoefu na mikiki ya cl na ligi kubwa barani ulaya.
Kwa upande wa Maguire (naamini atakuwa wetu ndani ya siku 2 hizi),kuna wachezaji kama varane na koulibaly. Bila kupepesa maneno,chaguo sahihi alikuwa koulibaly kama kigezo ni uwezo,kwa Maguire tunacheza kamari zaidi kuliko kuwa na uhakika wa performance yake. Unyumbani unatuua united.
Wan bisaka sitaki kusema sana muda utatuambia vizuri zaidi. Kama kweli tunamtaka longstaff kwenye nafasi ya kiungo wakati tumemuacha tielimani aende Leicester inatia shaka kidogo.
Sitaki kuisingizia scouting team yetu kuwa imelala ila naweza kusema inafanya kulingana na maelekezo toka juu. Lengo likiwa biashara zaidi ya ubora uwanjani. Katika mazingira kama Haya,Dof atafanyaje kazi yake kwa ufanisi?
Ngoja nicheki afcon na wanangu wa super eagles hapa kwanza kupunguza machungu.