Manchester United (Red Devils) | Special Thread

yes wamelipa paundi millioni 30 kwa usajili wa benjamin parvard.
tetesi zetu zimejaa vituko kama anavyosema Daud1990
tetesi za kumhitaji bruno fernandez zimeshazikwa
Kweli Mkuu , watu wanadhani usajili utakuwa nje ya hizo tetesi .. Haiwezi tokea hata siku moja ...


Kama watu wanabisha tuorodheshe wachezaji 30 ambao united inahusishwa kuwasajili halafu mwezi wa nane tuje hapa kuangalia wachezaji waliosajiliwa .. Lazima utakuta walikuwemo kwenye hiyo orodha ya wachezaji 30...



Ndio maana husikii tetesi za kusajiliwa Debruyne , Hazard , aubamayang au Salah... Hawa hutakuja kuwasikia wamesajiliwa united ... Ila wote wanaosikika kwenye tetesi lazima hata Wawili watasajiliwa.
 
Roy Keane: ''You look at Matthijs de Ligt, he’s captaining Ajax at 19 years old earning a modest wage. Meanwhile Rashford is scoring 10 goals a season, killing disabled fans in wheelchairs with his free kicks earning £100k & Lingard is earning £120k to be an Instagrammer.”
Love him or hate him, Roy Keane always tells it like it is.
 
Jana nilikuwa nawaza kama wewe mkuu. Tukitaka kutoka tulipo tuanze na usajili wa moderate players, tukikimbilia super stars tutapigwa tena hela halafu tutabaki kulalamika.
 

Mkuu ni kweli wachezaji wote wana viwango vya juu,na wataweza ku add quality katika team.
Tatizo langu mimi ni umri mchezaji akifikisha umri wa 30 napata tatizo kubwa kumsajili ukiondoa nafasi ya kipa.Toby ni mzuri lakini 30 years ni tatizo kubwa ambalo Jose alililea na kuharibu team pakubwa.

Ni kwanini tusisajili baki wa kati mwenye umri wa kati ya 20 hadi 27 mwisho ?.Ebu nishawishi walau kiduchu mchezaji wa 30 tunampeleka wapi zaidi ya kwenda kuzipa vipaji vya akina Tuazabe na ......
 

Leon Bailey na Kai ni combo nzuri sana pale Leverkusen.
 
Roy keane huwa anafurahisha Interview zake.

Nimepitia Magazeti ya Udaku ya Michezo England.

Daily mirror "Linasema Rashford muda smrefu atakuwa akipokea £ 300K Mshahara"

Rashford Itabidii atiee bidii sana katika upigaji wa Faulo/adhabu/Mipira iliyokufa,Bado anakazi kubwa yakufanya,Anatumia nguvu sana kupiga mpira huku shabaha yake ikiwa ndogo.

Hahaha Roy Wakati Mwingine Naona anashindwa kupokea Mabadiliko ya soka ya karne ya 21, (Wahafidhina hawapendagi mabadiliko).

Maisha ya karne ya 21 Wachezaji kukwepa mitandao ya kijamii ni ngumu kwa kiasi,Wengine hutengeneza pesa pia nje ya Uwanja kupitia Social Network/Media.

Lingard anabrand yake ya nguo
 
Mkuu unataka beki wa kati ya 20-27 kama nani kwa mfano ambaye yupo sokoni

Kati ya mabeki ninaotamani waje United ni Koullibally, lakini Napoli wanam rate kwa £130 million (Kuna watu hapa watasema hela zinaniuma kwani zinanihusu nini mimi, bila kujua itaathiri bajeti ya kununua ma winger, ma midfielders na mabeki wa pembeni wazuri). Tunahitaji kuimarisha pia maeneo mengine uwanjani.

De Ligt (£60+ million) ana bei nzuri lakini Juve, Bayern, Barca wanamtolea macho. United hana uwezo wa kugombania mchezaji na hizo timu kwa kuwa hashiriki UCL.

Skriniar amesaini mkataba mpya na Inter juzi juzi, hivyo tumsahahu kumsaini msimu huu

Aldewered anaweza kutusaidia japo kwa misimu miwili wakati tunamlea Tuanzebe na wakati tunajipa muda wa kutafuta beki kisiki lakini si kwa bei ya kupigwa
 
Kitu ambacho kinaendelea huko Ulaya ni kutumia United katika kukuza thamani ya mchezaji, almost kila mchezaji mzuri anatajwa kutakiwa na United

Ma agents wanawakuza Wachezaji wao ili kupandisha mishahara yao

Club zinaitaja United ili mchezaji wao anunuliwe na timu kwa bei kubwa

Nimeanza kuwa na wasiwasi na Sky Sport maana kila English, young, hungry and "talented" player wanasema Man United wanamtaka kisa OGS aliwahi kusema kitu kama hicho

Wengine hata sio talented lakini wanatajwa kuja United
 


Mkuu nadhani tukianza kusajili wachezaji wa umri wa 30 ni sawa na kupiga hatua 2 mbele na kurudi hatua 5 nyuma halafu ukajisifu kwamba umesonga mbele.Tofauti ya Toby na Smalling ni ndogo sana tena tutakuja mtukana Ole kwa uzembe wa kusajili baki wa kati mzee ambae hawezi kasi ya EPL.Kama angekuwa free labda tungejaribu lakini kutoa mpunga kwa mchezaji anayemalizia soka lake mimi naona ni risk kubwa sana.
 
Mkuu pale United hakuna beki anayefikia uwezo wa Toby

Nimesema akinunuliwa yeye sio mbaya kutokana na mazingira tuliyonayo kwa sasa, ni temporary measure endapo tutakosa mtu sahihi

Sitashawishika kufurahi kusajili beki wa kati kwa £100+million

Kwa inflation ya sasa ukipata mchezaji kama Toby kwa hicho kiasi ni hela ndogo sana, can you imagine mwaka mmoja uliopita Dany Levy alikuwa anataka kuikamua United £75million kwa huyu huyu Toby, na inasemekana United walikuwa tayari kutoa £50million?

Tumewahi kununua wazee na wakatusaidia pale United, Cantona, Teddy Sherigham, Van De Sar n.k
 


Nadhani tukienda France au Ureno na 25 m tutapata beki mzuri na mwenye umri mdogo.
 
Unamtoa erick Bailey unamwacha smaling! Unamwacha jones! Unamwacha young! Unamwacha lingard!
Anaondoka hereira anabaki rashford

What a joke!
 
Maguire ni pancha hilo.Muda utaongea
 
Unamtoa erick Bailey unamwacha smaling! Unamwacha jones! Unamwacha young! Unamwacha lingard!
Anaondoka hereira anabaki rashford
What a joke!
Herrera ndo ameikataa United na sio United kumkataa Herrera.

Herrera alipewa mkataba wa paundi 150k kwa wiki kwa miaka minne amekataa.

mind you, Herrera ana miaka 29 katikati ya mwaka huu kama sio mwishoni atakuwa na miaka 30 kamili.

kwahiyo tujue kuna kunyimwa mkataba, mfano; Valencia, na kuna kukataa mkataba kama Herrera.
 
Mkuu naheshimu mawazo yako lakini hivi unaona pale mbele hivi vitoto rashford,lingard, martial vitatupeleka hata top four next season!

Kwanini kocha anashindwa kuwatransform Wachezaji wawe bora
Gadiola na klop wameweza kupandisha viwango vya Wachezaji lkn kocha wetu naona anacheka Cheka tu na kina rashford

Sometimes napata hasira nataman kuchana hizi United kit
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…