Manchester United (Red Devils) | Special Thread

We jamaa umenikumbusha, skauti/afisa mmoja pale United aliwahi kusema waliwahi kumpendekeza De Jong na De Legit kusajiliwa kwenye academy ya United, wakubwa pale United wakakataa
 
Sitaki kuamini kuwa baada ya sisi kushindwa kupata mafanikio this season tumebadilika na kuwa wanawake na Liverpool kuwa wanawume.

Waikati Liverpool wanastrggle kama tunavyostruggle sisi sasa hawakukata tamaa kiasi cha kujiita wanawake kama tunavyotaka kujivisha sisi.
Tusikate tamaa kiasi hiki

Naamini mmeona wanaume wanavyopiga kazi

Sisi tumebaki kuwalipa wapuuzi mishahara mikubwa tu bila kutatua matatizo yetu ya msingi
 
Unaumia nn sasa au ndiyo nyie mechi ya kwanza mlikuwa mnashangillia barca
 
Ndio hivyo mkuu, ndio maana mimi siku zote ninalia na wafanya maamuzi waliopo juu
Uongozi wa juu ni tatizo pale United.

Hakuna haja tena ya kuwalaumu makocha kama uongozi utabaki uleule.

Kufukuzwa kwa Mourinho na kufunguka kwa LVG ndo mashabiki wamejua kila kitu kuhusu uongozi wa juu wa timu yao.

Glazers ni cancer, sijui tufanyaje tuwatoe.

We need a new CEO and experienced DoF.
 
Ni kweli mtuu timu ya ushindani ya muda mrefu yajengwi kwa kununua wachezaji wengi au wote ambao Ni world class,
*Bei zao Ni kubwa mno kwa soko la sasa hivi
*Wengi wako kimaslahi zaidi kuliko kujitoa kwa timu
*Wengi huja kujawa na majivuno(kujiona wakubwa kuliko club/kocha/wachezaji wenzao)
Hawa wanafaa unapokuwa upo desperate kushinda taji ndani muda mfupi(msimu au wa 2)

Timu zote zinazofanya vizuri kwa muda wa Kati/mrefu, wachezaji zilionao sio wote walinunuliwa wakiwa world class, Liverpool,City, Spurs, Bayern,Barca, Ajax(wanakuja vizuri), hizo zote zimejaaa wachezaji ambao ustaa wao wameupatia klabuni, japo kunawachache Sana Ni mastaa kwa kununuliwa..,...
Hehe..lakin liverpool wamedumu na kocha mmoja mda wote huo na wameenda naye taratibu. Ina mana Mou bas asingetimuliwa et mana yule ni kocha bora pia na ni mtu mweny mafanikio sana na akishika timu, lazima ktk misimu yake kombe abebe
Mou Ni kocha mzuri wa kuleta matokeo ya haraka/ndani ya muda mfupi, Hata Ed Woodward naaamini alimleta kwa malengo hayo kuipatia utd kombe kubwa(EPL/UEFA) ndani ya msimu au wa 2, na Mou kweli Ana rekodi nzuri Sana ya kufanya hivyo/kuchukua kombe ndani ya msimu au wa 2, hata utd kapiga kazi nzuri msimu wa kwanza Europa, wa2 utd was strong EPL title contender, wa 3 Kama kawaida akafukuzwa....

Why, huwa anapata makombe kwa kununua wachezaji waliova tayari kwenye timu zingine anawaunganisha anashinda kombe, shida kuwa wachezaji Hawa wengi huwa na viburi hivyo hugombana nao baada ya muda mfupi TU hivyo yeye kutimuliwa kwa timu kupata matokeo mabaya.....

Mtizamo wangu,
*utd walikuwa sahihi kumuajiri Mou, walifanya makosa kumuongeza kandarasi, pia walikuwa sahihi kumfukuza.....
*Utd itafute director of sport/football mzuri, pamoja na kocha mzuri..
*Utd ijipe msimu 2 ya kungeneza timu kwa kufanya mpango mzuri wa kusajili(kuachana na habari ya matop player kwa sasa) ijikite kwenye kununua potential talents, kidoooooogo baadae ndo inunue top/world class kuziba mapengo machache (
Kama walivyo fanya city na Liverpool, wamekuja kununua wachezaji wa Bei ghari kuziba mapengo machache TU,(liver beki na kipa)

Otherwise, kwa ubovu wa timu ya UTD sahivi hata ikitumia
350m, kwenye usajili huu kwa kusafaka top/world class itambulia wachezaji 3, ambao hawataleta mabadiliko makubwa kwenye kikosi kushindana na city na liver next season, hivyo kuishia kuleta mikwaruzano na kocha na wachezaji wengine, na kuomba kuondoka mwishoni mwa msimu, Hivyo tatizo linarudi pale pale pale, Bora itumie hata
250m kutafuta wachezaji ambao hawaanza kuwa mastaa ila wa vipaji na wanaweza endana na falsafa ya timu, tukipata Hawa 4/5, then mwakani ndo timu ingalie mapengo yapo wapi iliyazibwe na hao top class 2/3....
 
kikosi cha pesa ndogo sana wachezaji wote wametokea timu ndogo lakini kazi yao nzuri.
Liverpool kikosi cha pesa ndogo? Hapana aisee usisahau van djik 75m, kipa katoka roma 65m, keita 52m, kuna salah 43m kina chamberlein 35m, mane 30m, fabinho 43m etc hao tu ni zaidi ya 300m.

Usisahau msimu uliopita wamespend kushinda hata sisi.
 
Liverpool kikosi cha pesa ndogo? Hapana aisee usisahau van djik 75m, kipa katoka roma 65m, keita 52m, kuna salah 43m kina chamberlein 35m, mane 30m, fabinho 43m etc hao tu ni zaidi ya 300m.

Usisahau msimu uliopita wamespend kushinda hata sisi.

Lakini hao wachezaji walinunuliwa misimu tofauti
 
Umeandika point.
Kocha mzuri saiv unamtoa wapi? Unampata wapi?
 

Unaongelea 3-4 year project:

Year 1: assess the current squad

Year 2: recruit, assemble and get rid of the mediocre players

Year 3: continue-to recruit and make reinforcements

Year 4: fine tuning/reinforcements

Year 5: turn the quality squad into a contender and start challenge for the titles

Hiyo ndio blueprint of Jurgen Klopp’s project

The issue is: do you have such patience????
 
Bila keita ni 170m, ukimuweka keita ambaye hela ilitoka january ni zaidi ya 220m kwa msimu uliopita tu.

Compare na Timu nyengine isiyo Man city/Man u nyie ni spenders wakubwa tu.

Spurs wamespend 0 msimu uliopita.

Sawa mkuu
Basi mleteni mchumi Arsene Wenger mzee wa kubana matumizi
 
Bila keita ni 170m, ukimuweka keita ambaye hela ilitoka january ni zaidi ya 220m kwa msimu uliopita tu.

Compare na Timu nyengine isiyo Man city/Man u nyie ni spenders wakubwa tu.

Spurs wamespend 0 msimu uliopita.
And still Tot wapo nusu fainal uefa na top 4 wana uhakika. United ni yuropa na matokeo yetu ya kuunga unga
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…