Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Haya maneno nimeshindwa kuamini kama ni Mourinho mwenyewe. Kweli kiburi na majivuno vina mwisho. Amerudi kuwa mdogo, mwanafunzi, na anakiri wazi kuwa yeye ni school boy kwa pep na clop! Maajabu haya.
 
Maneno ya Moyes yanaumiza sana.
 
jose mourinho ameamua kurusha tena jiwe zito kwenye nyumba ilee iliojengwa kwa matofali pale jijini manchester.
"In my next job I will not be starting a conversation without knowing exactly what the club wants and what the club has to give in terms of structure and the club objectives."
kila la kheri bwana wewe katika harakati zako za kutafuta ajira mpya, tokea ulipotuacha mpaka muda huu bado hatujaweza kuwa na mfumo rasmi wa kiuchezaji, tumekuwa hatuna tofauti na wafugaji kutoka kabila la wamasai.
 
Haya maneno nimeshindwa kuamini kama ni Mourinho mwenyewe. Kweli kiburi na majivuno vina mwisho. Amerudi kuwa mdogo, mwanafunzi, na anakiri wazi kuwa yeye ni school boy kwa pep na clop! Maajabu haya.
henderson, james milner pamoja na dejan lovren ndio wachezaji pekee wanaocheza mara kwa mara pale liverpool kikosi cha kwanza ukiwaondoa sturridge, lallana pamoja na alberto moreno ambao mustakabali wao pale liverpool haueleweki kwa sasa, jose anamaanisha ya kwamba jurgen klopp ameruhusiwa kujenga emperor yake mwenyewe bila ya kuingiliwa kimaamuzi hivyo hivyo kwa upande wa josep guardiola.

hakuna sehemu aliyoonyesha heshima kwa jurgen klopp ambaye hajashinda chochote mpaka muda huu.
madai ya jose mourinho kwa asilimia 60 yapo sahihi na asilimia 40 hayupo sahihi kwa uoni wangu.
 
Toka sir Alex Ferguson aondoke man u imetupa pesa nyingi sana bila mafanikio yoyote.

Moyes alisajili wachezaji wake kati ya hao hakuna hata mmoja aliyekuwa consistent kikosini walau kwa mechi kumi tu.

Luis van Gal naye alifanya usajili ila cha kushangaza mchezaji pekee wa luis van gal ambaye alifanya vizuri ni Daley Blind ambaye nae hayupo wengine wote hawakuwahi kucheza walau ten games consistently

Mourinho naye ni vile vile kakusanya watu wake ni pogba tu ndiyo yuko fit naye kwa madoido kishenzi.

Tatizo la Man u Woodward hajui anachopigania .
 
Kuepekea dirisha la usajili mwezi wa 7 timu kubwa kama Madrid, Juve, Barca (centre back) Man city (defensive midfielder na left back) , Bayern, zitakuwa zinataka kufanya usajili wa uhakika na mkubwa kiasi (overhaul) ukitoa city na Barca, Sijajua matumaini yetu yanalala wapi ila tukisema tuegemea kwenye top players basi yanaweza kurudi ya Mourinho... Solskjaer atimize ahadi yake ya young prospect wenye potential kubwa ya kuja kutubeba
 
Aliyeijenga Man U ndio aliyeibomoa. Hapa namzungumizia Alex Ferguson. Ferguson hakuiacha timu katika hali nzuri. Wachezaji waliochukua EPL 2013 ndio walikuwa wanamalizia ubora wao (Carrick, Vidic, Ferdinand, Van Persie nk.) baada ya hapo timu ilihitaji reform ya hali ya juu. Ferguson hakuandaa mrithi anayejua Man U inataka nini au mrithi ambaye ataendana na falsafa ya Man U. Baada ya kuchukua ubingwa tu akaiacha timu na kumpa mscotish mwenzake Moyes ambaye kimsingi alimpa kwakuwa alikuwa anam challenge sana wanapokutana na Everton au Moyes kipindi hicho.
 
Sir Alex Ferguson kam aliweza kwenda na falsafa za team kwann wengne washindwe na kuandaa mrithi wake hyo sio lazma kam aliijenga united bas wengne waijenga wwnavyojua wao ila wactoke falsafa za united uongozi wenyew sas hv haujui unataka nn ndio mana tunaenda tu ili mrad na kutumia uzoefu bas.

Sas hv hatuna malengo yeyote yale na vikombe tucheze tuingie top 4 bas shughul imeisha, Ferguson alishafanya yake yameshapita tusimlaum eti katuacha pabaya hakutuandalia mrith wake mzur hyo sio kazi yake
 
Majirani.......Majirani......wazima lakini mnajisikiaje na hali.........Hali zenu zinaendeleaje
 
De Lima hana mbwembwe za Dribbling ? humjui Ronaldo de Lima wewe2
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…