Ndugu yangu hakuna ambaye yupo ndani ya club kati yetu, lakini ni mambo mangapi ya ndani tunaongea kuhusu kinachoondelea pale United? Sources zetu za info ni zile zile, Tv kubwa na article kubwa kutoka kwa vyombo kama BBC, Sky n.k. Pia kupitia akaunti za social media za watu maarufu wanaojihusisha na soka.
Vinginevyo tungekuwa hatuongei mpaka tusubiri club i confirm flani kasajiliwa au flani kaachwa. Kwa hiyo sio pale zinapotajwa habari zinazopendwa ndio tujidai tunajua habari za nyuma ya pazia na details nyingine, ila kama habari hatuipendi ndio tujidai kwamba hatuwezi kujua habari zilizopo nyuma ya pazia.
Kuhusu kutoa hela hovyo bila kujali wage structure si jambo la busara lakini si ndio Ed alitoa £500,000 kwa Alexis? Au hiyo ipo kwenye structure ya wage bill ya United?
Lakini labda nikuulize je unajua kwanini sasa hivi Mata, Herrera na Degea wataka dau kubwa katika mkataba wao. Sababu ni simple tu, katika negotiation wana upper hand dhidi ya United, yaani kwa kuchelewa kuwapa mkataba United amekuwa kwenye upande wa kubanwa katika mazungumzo.
Ina maana mazungumzo yangefanywa hata miaka 2 kabla ya mkataba kuisha wasingetaka dau kubwa kama sasa na wangetaka dau kubwa United angekuwa na options zaidi tofauti na sasa (mfano kuwauza kwa bei nzuri na kutafuta mbadala).
Na kwa mtazamo wako kwamba kitakachofuata ni nini? Ni kumuaza Degea kwa hasara (maana mkataba utakuwa umebaki chini ya Mwaka) au kumpa mkataba anaotaka (kitu ambacho Ed anagomea sasa hivi). Kwa Herrera na Mata itakuwa either kuwapa mkataba wanaotaka au waondoke bure na Man United atafute £ 80+ kuziba nafasi zao hao jamaa wawili na kuwapa mshahara mnono hao wachezaji wageni.
Anacholaumiwa Ed ni kuchelewa ku settle mambo ya mikataba mapema kiasi cha kwamba wachezaji wanaweza kuondoka bure na kuziba nafasi zao kuwa tabu.
Kumbuka kwa sasa Man anahitaji almost £250 million kuimarisha kikosi (bila akina Herrera kuondoka) lakini hao jamaa wakiondoka itawalizimu kutumia zaidi ya £300 ili kuziba mapengo na kuimarisha kikosi, je huyo Ed yupo tayari kutoa huo mpunga? Na akitoa huoni kama gharama waliyoikwepa kwa mlango huu wanaikubali kwa mlango mwingine?
Halafu mfano wa Arsenal ni mfano wa ajabu sana. Yaani kwa kuwa Ramsey anaondoka bure na sisi tuige kwao. Arsenal walifanya makosa kwa Sanchez akaondoka, kwa Ozil (bahati nzuri wakamsainisha mwishoni, lakini kwa hela aliyotaka) na sasa kosa limejirudia kwa Ramsey. Kosa ni lile lile la kusubiri mkataba upo mwishoni ndio mnaanza kukimbizana kwenye mazungumzo.
Ed ni mzigo kwenye football side japo anajitahidi kwenye biashara na tukumbuke yeye na Glazers siblings wanachotaka ni timu kuingia top four tu ili timu itinge UCL kwa ajili ya biashara, sasa sisi tunaopenda kuchukua vikombe kazi kwetu
Sent using
Jamii Forums mobile app