Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Ukimtoa fabinho na shaqir si walicheza final ya europa hao au?
 
Hakufeli wao ndo waliokuwa wakipinga kwa mfano tobby na magure walikuwa wanataka kuja bodi ikazuia leo aliezuia akikuwepo uwanjani goli zimefungwa kwa njia zile zile

Mkuu Nataka Nikwambie kitu! Unajua Mara Nyingi unapozozana Kihoja na wale Member Wa Mou-Out Mimi huwa napotezea.

Lakini Ni Kwamba ushafika Muda Wa Kuwa Uukubali Ukweli!! Chanzo cha yote Haya Ni Kwamba "Mourinho Amepoteza Control ya Dressing Room".

Ni Sawa na Conte last Season!! Mtazame Sarri sasahivi wachezaji Ni Walewale Wa Conte lakini Wanaperform vizuri kwasababu bado anaudhibiti Wa Dressing Room.
 
Hilo nimekubali la kupoteza control ya dressing room post yangu ipo hapo mourinho kubak pale kutagawa timu japo kuna watu nyuma yake wamemuangusha kwa mfano kwa sasa kuirudisha timu ktk mentality ya ushind ni vigum sana hii maana yake kama angepata watu wake aliokuwa akiwataka haya mambo yangetatulika taratibu ila kwa sasa ni ngumu kocha mwenyewe hana imani na safu yake ya ulinz
 

Hapo tumeelewana
 
Hivi radika unayakumbuka Maneno Haya ya Mourinho aliyoyasema Baada ya Mechi vs Liverpool kwenye Preseason tour? ↓↓

"We started the game with a lot of players who will not be in our squad on August 9. This is not my squad, not even half, not even 30% of my squad. So don't look to this."

Unadhani Kocha hasa anayeithamini Kazi Yake anaweza sema Maneno hayo?
Sasa Kwa Maneno Hayo Wale Vijana aliikwenda Nao Marekani Unadhani Watamuelewaje Mourinho?
 

In any sport, When a coach loses the dressing room there’s only one solution.
He has to go!!!
 
Mkuu hayo maneno yana maana sana alishafanya maombi toka mwezi wa nne hadi anakwenda pre season kampata fred tu dalot kachukuliwa aligoma kutia mkataba na porto united ikatumia mwanya huo so ukiangalia kocha alishapagawa hajui itakuwaje ligi ikianza ni kikos kipi atakuwa nacho kwamba angel gomes aje acheze kumi?
 
Hii ndio point mkuu radika anashindwa kuikubali kwa 100%.Hakuna solution kwa sasa zaidi ya Mou kufukuzwa..

Kocha mzoefu huwezi kutamka hadharani huna Imani na wachezaji wako..Au nimeshindwa Sababu sijaletewa A,B,C.
Kocha hufanya kazi na wachezaji ulio nao huku ukiwabadilisha polepole.

Mourihno analalamika wakati zaidi ya wachezaji 7 kawasajili yeye.Huwezi kubadili wachezaji 9 kwa wakati mmoja.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu radika hakuna mtu aliyemuangusha Mourihno zaidi yake mwenyewe na mbinu zake mbovu.Amesajiliwa wachezaji wangapi mpaka sasa?

Hakuna kocha anayetimiziwa mahitaji yake kwa 100%..Wengine hawalalamiki ndio maana huwasikii.Hawa wachezaji waliopo wakipata kocha mpya watabadilika sana.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Naheshimu maoni yako mkuu huenda unachoongea kina ukweli point kabisa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…