Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Takwimu hazidanganyi mkuu.
 
Majinga ayo yatajuaje

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Man Utd ipo on fire.

Chelsea nao wanazidi kujizatiti.

Man City wao wanakimbiza mwizi kimya kimya.

Tottenham wao hawajabadilika kabisa.

Everton anachukua nafasi ya Arsenal.

Liverpool siwapi matarajio kabisa.

Arsenal ndo wakuonewa huruma kabisa.
 
Kwa hiki wanacho kifanya MADRID sio kitu kizuri kabisaa. Sisi tuliwapa CR7 wenyewe wanatunyima MORATA.
Tumeamua kumchukua ROMELU AMBROSI LUKUMBESA BOLINGO LUFUFU. Bila ya kupenda lilikuwa chaguo la Z.
Wallah kuanzia leo tunasema tunahamia BARCELONA.

Asee watu bhana
 
morata wala, chelsea wenyewe inawauma kumkosa lukaku,

Sent using Jamii Forums mobile app
 
nimebahatika kuangalia mechi zote mbili tulizocheza nchini marekani ila ninashangazwa na suala la mourinho kumtumia fundi andreas perreira kama ni deep play maker,kiukweli bado nimebaki najiuliiza masuali mengi sana kuhusiana na mustakabali wa kijana huyu

  1. je ina maana jose mourinho anataka kutuonesha sisi mashabiki na wapenzi wa manchester united ya kwamba perreira ndio mrithi wa michael carrick?
  2. au anataka kutuonyesha ya kwamba hizi kelele zetu tunazopiga juu ya kutaka amsajili nainggolan ambaye ni kiungo wa AS ROMA kwake yeye si kitu na anamuona andreas perreira anaweza kuwa ni bora zaidi ya nainggolan?
  3. au ameamua kuachana na mpango wa kumsajili kiungo wa ulinzi kama matic na dyer kutokana na soko la usajili kuwa ni gumu sana?
  4. au ni kwa sababu itakuwa ni vigumu kwa perreira kupata namba kama kiungo mchezeshaji kutokana na kuwa na wachezaji kama pogba, mata, mkhitaryan, lingard, herrera.
  5. au anataka kumfanya awe strong kama alivyomfanya herrera msimu ulopita?
 

Sijaona kelele zako juu ya Tuanzebe kuchezeshwa namba 6, mechi ya Wigan mwaka jana alimchezesha hapohapo.
Kumchezesha namba 6 sio kwamba ndio namba yake ni anamkuza kiakili kukabiliana na presha ya timu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…